Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 27

Maktaba ya Jumba la Ufalme Inaweza Kutusaidia Namna Gani?

Maktaba ya Jumba la Ufalme Inaweza Kutusaidia Namna Gani?

Israeli

Jamuhuri ya Cheki

Benini

Visiwa vya caïmans

Unapenda kutafuta habari ili ujue Biblia muzuri zaidi? Unapenda kujua mambo mingi juu ya andiko fulani ao mutu fulani, mahali fulani, ao kitu fulani chenye kuzungumuziwa mu Biblia? Ao, umekwisha kujiuliza ikiwa Neno la Mungu linaweza kukusaidia kupiganisha mahangaiko fulani yenye uko nayo? Kama ni vile, unaweza kutumia maktaba (bibliothèque) ya Jumba la Ufalme.

Iko na vyombo vya kutusaidia kutafuta habari. Pengine hauna vichapo vyote vya Mashahidi wa Yehova vyenye kutegemea Biblia vyenye kupatikana mu luga yako. Lakini maktaba ya Jumba la Ufalme iko na vichapo mingi vya sasa. Tena, inaweza kuwa na tafsiri mbalimbali za Biblia, kamusi ya muzuri, na vitabu vingine vyenye vinaweza kutusaidia kutafuta habari. Unaweza kutumia maktaba mbele ya mikutano na kisha mikutano. Kama mu maktaba muko ordinatere, inaweza kuwa na Watchtower Library. Watchtower Library ni programu ya kielektroniki yenye kuwa na vichapo vyetu vya mingi. Na iko na sehemu yenye unaweza kutumia kwa vyepesi ili kutafuta habari juu ya jambo fulani, neno fulani, ao andiko fulani.

Inasaidia wanafunzi wa Mukutano Utumishi na Maisha. Unaweza kutumia maktaba ya Jumba la Ufalme wakati unatayarisha migao yako. Ni mwangalizi wa Mukutano Utumishi na Maisha njo mwenye anasimamia ile maktaba. Anapaswa kuangalia ikiwa vitabu vya mupya vimewekwa katika maktaba na kama vinapangwa muzuri. Yeye ao ndugu mwenye anakufundishaka Biblia anaweza kukuonyesha namna ya kutafuta habari yenye uko nayo lazima. Lakini, hakuna mutu mwenye anaruhusiwa kukamata vichapo vya maktaba ya Jumba la Ufalme na kuenda navyo. Na tena, hatupaswe kuviharibisha na hatupaswe kutia alama ao kuandika ndani.

Biblia inasema kama ili ‘kupata ujuzi juu ya Mungu,’ tunapaswa kuwa tayari kutafuta ujuzi huo “kama hazina zenye kufichwa.” (Mezali 2:1-5) Maktaba ya Jumba la Ufalme inaweza kukusaidia uanze kutafuta ujuzi huo.

  • Ni vyombo gani vya kusaidia kutafuta habari vyenye kupatikana katika maktaba ya Jumba la Ufalme?

  • Ni nani wanaweza kukusaidia ujue namna ya kutumia muzuri ile maktaba?