Hamia kwenye habari

Je, Kuteseka Kutawahi Kuisha?

Je, Kuteseka Kutawahi Kuisha?

Je, ungesema . . .

  • ndio?

  • la?

  • labda?

BIBLIA HUSEMA HIVI

“Mungu . . . atayafuta machozi yao yote, maana hakutakuwako tena na kifo, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu.”​—Ufunuo 21:3, 4, Habari Njema kwa Watu Wote.

FAIDA ZA KUAMINI JAMBO HILO

Uhakikisho wa kwamba Mungu hasababishi matatizo yetu.​—Yakobo 1:13.

Faraja kutokana na kujua kwamba Mungu anaelewa kabisa tunavyohisi tunapoteseka.​—Zekaria 2:8.

Tumaini la kwamba kuteseka kote kutaisha.​—Zaburi 37:9-11.

JE, KWELI TUNAWEZA KUAMINI KILE AMBACHO BIBLIA HUSEMA?

Ndiyo, kwa angalau sababu mbili:

  • Mungu huchukia mateso na ukosefu wa haki. Hebu wazia jinsi Yehova Mungu alivyohisi watu wake katika nyakati za Biblia walipoteswa kikatili. Biblia inasema kwamba alifadhaika kwa sababu ya “wale waliowatesa.”​—Waamuzi 2:18, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

    Mungu hafurahishwi hata kidogo na wale wanaowaumiza wengine. Kwa mfano, Biblia inasema kwamba anachukia “mikono inayomwaga damu isiyo na hatia.” —Methali 6:16, 17.

  • Mungu anatujali tukiwa mtu mmoja mmoja. Kila mmoja wetu anajua “mateso yake mwenyewe na maumivu yake mwenyewe” lakini hata Yehova anayajua maumivu hayo!2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30.

    Kupitia Ufalme wake, hivi karibuni Yehova ataondoa mateso yanayomkabili kila mtu. (Mathayo 6:9, 10) Kwa sasa, anawafariji kwa wororo wale wanaomtafuta kwa moyo wote.—Matendo 17:27; 2 Wakorintho 1:3, 4.

JAMBO LA KUFIKIRIA

Kwa nini Mungu anaruhusu watu wateseke?

Biblia inajibu swali hilo kwenye WAROMA 5:12 na 2 PETRO 3:9.