Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 4

Binti Aliyemufurahisha Baba Yake na Pia Yehova

Binti Aliyemufurahisha Baba Yake na Pia Yehova

Yefta anamupatia Yehova ahadi gani?

Hata kama haikukuwa mwepesi, binti wa Yefta alitimiza ahadi yenye baba yake alimupatia Yehova

Unamuona binti huyu ku picha hii?— Ni mutoto wa bwana moja anayeitwa Yefta. Biblia haitaje jina lake, lakini tunajua kama alimufurahisha baba yake na pia Yehova. Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya binti huyu na baba yake.

Yefta alikuwa mutu muzuri. Alikuwa anapitisha wakati mwingi na mutoto wake ili kumufundisha habari za Yehova. Yefta alikuwa pia mutu mwenye nguvu na kiongozi muzuri. Siku fulani, Waisraeli walimuomba awapeleke kupigana vita na maadui wao.

Yefta alimuomba Mungu amusaidie ili ashinde vita hiyo. Yefta alimuambia Yehova hivi: ‘Nikishinda vita hiyo, wakati nitarudi, mutu wa kwanza mwenye atatokea mu nyumba yangu ili kunipokea, nitakupatia mutu huyo.’ Ni kusema, mutu huyo anapashwa kuishi na kumutumikia Mungu maisha yake yote ku hema ya ibada. Wakati huo, watu walikuwa wanakutana ku hema ya ibada ili kumuabudu Mungu. Habari ya kufurahisha ni hii: Yefta alishinda vita hiyo! Wakati anarudi, unajua ni nani mutu wa kwanza mwenye anatokea mu nyumba yake ili kumupokea?—

Ni ule binti wake! Yefta alikuwa na mutoto huyo mumoja tu, lakini sasa inamuomba amutume aende kuishi mbali ku hema ya ibada. Yefta anahuzunika sana. Lakini kumbuka, Yefta alikuwa amekwisha kumupatia Yehova ahadi. Bila kusita, binti wake anamuambia hivi: ‘Papa ulimupatia Yehova ahadi, kwa hiyo unapashwa kutimiza ahadi yako.’

Kila mwaka, marafiki wa binti wa Yefta walikuja kumutembelea

Binti wa Yefta, alihuzunika pia. Juu kule ku hema ya ibada, hangeolewa wala kuzaa watoto. Hata hivyo, binti huyo alipenda sana kutimiza ile ahadi ya baba yake na pia alipenda kumufurahisha Yehova. Aliona kama kufanya vile ndio jambo la maana sana kuliko kuolewa na kuzaa watoto. Kwa hiyo, aliacha nyumba yao na kuenda kuishi maisha yake yote ku hema ya ibada.

Unawaza tendo hilo lilimufurahisha baba yake na vilevile Yehova?— Tendo hilo liliwafurahisha! Ukimutii Yehova na kumupenda kama vile binti wa Yefta alifanya, weye pia unaweza kufurahisha sana wazazi wako na vilevile Yehova.