Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 6

Daudi Hakuwa Anaogopa

Daudi Hakuwa Anaogopa

Unazoea kufanya nini wakati unaogopa?— Pengine unamukimbilia mama yako ao baba yako ili akusaidie. Lakini kuko mutu mwengine mwenye anaweza pia kukusaidia. Mutu huyo iko na nguvu kushinda watu wote. Unajua mutu huyo ni nani?— Ni Yehova Mungu. Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya kijana mumoja anayeitwa Daudi. Kijana huyo hakuwa anaogopa kwa sababu kila siku alijua kama Yehova atamusaidia.

Tangu wakati Daudi alikuwa mutoto mudogo, wazazi wake walimufundisha kumupenda Yehova. Hilo lilimusaidia asikuwe anaogopa, hata wakati mambo fulani yenye kuogopesha sana yanamufikia. Daudi alijua kama Yehova ni Rafiki yake na atamusaidia. Siku moja, Daudi alikuwa anachunga kondoo, kisha simba moja mukubwa ikatokea. Ile Simba ikakamata kondoo moja katika kinywa chake! Unajua Daudi alifanya nini? Alifuata ile simba na akaiua. Na inaonekana aliua ile simba kwa mikono yake tu! Tena wakati nyama yenye kuitwa dubu ilishambulia kondoo zenye Daudi alikuwa anachunga, Daudi aliua pia ile dubu! Unawaza ni nani alimusaidia Daudi kuua wale wanyama?— Ni Yehova.

Kuna siku ingine Daudi alionyesha kama hakuwa anaogopa. Waisraeli walikuwa wanapigana na watu wanaoitwa Wafilistini. Soda mumoja wa Wafilistini alikuwa wa kabambi sana, na murefu kabisa! Jina lake Goliati. Ule soda alikuwa anamuchekelea Yehova na kuchekelea wasoda wa Waisraeli. Goliati aliwaambia wasoda wa Waisraeli kwa zarau hivi: ‘Kama muko na nguvu mukuye tupigane.’ Lakini Waisraeli wote waliogopa sana kuenda kupigana naye. Daudi alisikia maneno hayo ya Goliati. Akamuambia Goliati hivi: ‘Miye nitapigana na weye! Yehova atanisaidia, na nitakushinda!’ Unaona, Daudi hakuwa anaogopa, si vile?— Hakuwa anaogopa. Unapenda kujua ni nini ilitokea kisha?

Daudi alikamata kombeo ao mujeledi wake wa kutupa majiwe, na akachagua majiwe tano. Kisha akaenda kupigana na Goliati. Wakati Goliati aliona kama Daudi ni kijana mudogo tu, alimuchekelea sana! Lakini Daudi akamuambia hivi: ‘Weye unakuya na upanga ili kupigana na miye, lakini miye ninakuya kwako na jina la Yehova!’ Sasa akatia jiwe moja ndani ya mujeledi wake, akakimbia kwenye Goliati iko, na akamutupia ile jiwe. Ile jiwe ikamupiga Goliati katikati ya macho! Goliati akaanguka chini, na akakufa! Wakati Wafilistini waliona vile, wakaogopa sana na wakakimbia. Namna gani kijana mudogo kama Daudi aliweza kumushinda ule mutu wa kabambi sana?— Yehova alimusaidia Daudi. Kwa hiyo, Yehova alikuwa na nguvu mingi sana kuliko ule soda wa kabambi sana!

Daudi hakuwa anaogopa juu alijua kama Yehova atamusaidia

Hadisi ya Daudi inakufundisha nini?— Yehova iko na nguvu mingi sana kushinda watu wote. Pia Yehova ni Rafiki yako. Kwa hiyo, siku fulani ukisikia woga, kumbuka kama Yehova anaweza kukusaidia pia ili uwe na nguvu!

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO