Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 9

Yeremia Hakuacha Kuwatangazia Watu Habari ya Yehova

Yeremia Hakuacha Kuwatangazia Watu Habari ya Yehova

Watu hawa wanamusirikia Yeremia juu ya nini?

Yehova alimuokoa Yeremia

Wakati tunawatangazia watu habari ya Yehova, kuko wakati wanatuchekelea ao kutusirikia. Ile inaweza kutufanya tuache kuwatangazia watu habari ya Mungu. Kuko wakati weye pia umejisikia vile?— Katika Biblia muko hadisi ya kijana mumoja mwenye alimupenda Yehova. Kijana ule anaitwa Yeremia. Wakati fulani Yeremia alitaka kuacha kuwatangazia watu habari ya Yehova. Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya kijana Yeremia.

Wakati Yeremia alikuwa angali kijana tu, Yehova alimuambia kama anapashwa kuwaelezea watu waache kufanya matendo mabaya. Yeremia alijisikia kama hataweza kufanya ile kazi. Kwa hiyo, aliogopa kabisa. Yeremia alimuambia Yehova hivi: ‘Sijue kabisa kusema. Miye ningali mutoto tu.’ Lakini Yehova akamuambia hivi: ‘Usiogope Yeremia. Miye nitakusaidia.’

Wakati Yeremia alisikia vile, akaanza kuwatangazia watu habari ya Yehova. Aliwaambia watu hivi: ‘Kama hamubadilishe matendo yenu, Yehova atawaazibu.’ Unawaza watu walibadilisha matendo yao kama vile Yeremia aliwaambia?— Kuliko kubadilisha matendo yao, watu walimuchekelea Yeremia na kumusirikia sana. Wengine hata walitaka kumuua! Kwa hiyo, unawaza Yeremia alijisikia namna gani?— Yeremia aliogopa, na alianza kusema: ‘Sitawatangazia watu tena habari ya Yehova.’ Lakini, unawaza aliacha kabisa kuwatangazia watu habari ya Yehova?— Hakuacha. Yeremia alimupenda sana Yehova, kwa hiyo, haingewezekana aache kuwatangazia watu habari ya Yehova. Na Yehova aliendelea kumulinda Yeremia, juu Yeremia hakuacha kuwatangazia watu habari ya Yehova.

Kwa mufano, siku moja, wanaume fulani wabaya walimutupa Yeremia mu shimo yenye kuwa na matope mingi. Katika ile shimo, Yeremia hakuwa na chakula ao maji. Wale wanaume walimuacha Yeremia katika ile shimo ili akufie mule. Lakini, Yehova alimusaidia, na Yeremia hakukufa!

Mufano wa Yeremia unakufundisha nini?— Hata kama wakati fulani Yeremia aliogopa, hakuacha kuwatangazia watu habari ya Yehova. Weye pia watu wanaweza kukuchekelea ao kukusirikia wakati unawaambia habari ya Yehova. Unaweza kusikia haya na unaweza hata kuogopa. Lakini usiache hata kidogo kuwaambia watu habari ya Yehova. Kila siku, Yehova atakusaidia kama vile alimusaidia Yeremia.