Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 14

Ufalme Wenye Utatawala Dunia Yote

Ufalme Wenye Utatawala Dunia Yote

Unawaza tunataka kuzungumuza juu ya Ufalme gani?— Tutazungumuza juu ya Ufalme wa Mungu wenye utarudisha paradiso duniani. Unapenda kujifunza mambo mengi juu ya Ufalme wa Mungu?—

Kila ufalme uko na mufalme mwenye kutawala. Na mufalme huyo anatawala watu wenye kuishi katika inchi yake. Unajua ni nani Mufalme wa Ufalme wa Mungu?— Ni Yesu Kristo. Anaishi mbinguni. Karibuni atatawala kila mutu mwenye kuishi duniani! Unawaza tutateseka tena wakati Yesu atakuwa Mufalme juu ya dunia yote?—

Uko na hamu ya kuona nini katika Paradiso?

Tutafurahi sana! Mu Paradiso watu hawatapigana tena, wala kuenda kwenye vita. Watu wote watapendana. Hakuna mutu atakuwa mugonjwa, wala hakuna mutu atakufa. Watu wenye kuwa vipofu wataona, na watu wenye hawasikie watasikia. Watu wenye kuwa vilema wataruka-ruka na kukimbia. Kila mutu atakuwa na chakula mingi. Na wanyama watakuwa marafiki kati yao na watakuwa marafiki yetu. Watu waliokufa wataishi tena. Wanaume na wanawake wengi wenye tumesemea katika kitabu hiki kidogo, kama vile Rebeka, Rahabu, Daudi na Eliya, wataishi tena! Na weye utapenda kukutana na watu hao?—

Yehova anakupenda na anataka ukuwe na furaha. Kama unaendelea kujifunza habari za Yehova na kumutii, utaishi milele mu paradiso ya muzuri sana! Hii habari inakufurahisha?—