Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 1

‘Ufalme Wako Uje’

‘Ufalme Wako Uje’

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Inazungumuzia mambo ambayo Yesu alifundisha juu ya Ufalme wa Mungu

1, 2. Yehova aliwaambia mitume watatu wa Yesu nini, na ni nini inaonyesha kwamba walitii maneno hayo?

IKIWA Yehova Mungu anakuomba ufanye jambo fulani, utakubali ao utakataa? Bila shaka, utakuwa tayari kutii kila jambo ambalo anakuomba ufanye, sivyo?

2 Siku fulani kisha Pasaka ya mwaka wa 32, mitume watatu wa Yesu, ni kusema, Petro, Yakobo na Yohana, walisikia sauti ya Yehova, ambayo iliwaomba wafanye jambo fulani. (Soma Mathayo 17:1-5.) Siku hiyo walikuwa na Bwana wao kwenye ‘mulima murefu,’ na katika maono, waliona namna Yesu atakavyokuwa katika utukufu wakati atakuwa Mufalme huko mbinguni. Petro aliona jambo hilo kuwa jambo la kweli kabisa, kwa hiyo akaomba wajenge mahema matatu mahali hapo. Wakati Petro alikuwa angali anasema, wingu liliwafunika. Petro na wenzake walipata pendeleo la kusikia waziwazi sauti ya Yehova mwenyewe. Ni watu wadogo sana ndio waliokuwa wamepata pendeleo kama hilo. Yehova aliwahakikishia kwamba Yesu ni Mwana wake, na kisha akawaambia waziwazi hivi: ‘Mumusikilize yeye.’ Mitume hao walitii maneno hayo. Walisikiliza mafundisho ya Yesu, na waliwatia wengine moyo kufanya hivyo.—Mdo. 3:19-23; 4:18-20.

Yesu alizungumuzia sana habari ya Ufalme wa Mungu kuliko habari zingine zote

3. Sababu gani Yehova anapenda tumusikilize Mwana wake, na ni habari gani ya maana tutachunguza?

3 Maneno haya: ‘Mumusikilize yeye,’ yaliandikwa katika Biblia kwa faida yetu. (Rom. 15:4) Sababu gani tunapaswa kumusikiliza Yesu? Kwa sababu Yesu ndiye Musemaji wa Yehova na kila wakati Yesu alikuwa anafundisha, alikuwa anasema maneno ambayo Baba yake alipenda sisi tujue. (Yoh. 1:1, 14) Yesu alizungumuzia sana Ufalme wa Mungu, ni kusema, serikali ao guvernema ya mbinguni ambayo itaongozwa na Masiya. Katika serikali hiyo, Yesu Kristo atatawala na watu 144000. Yesu alizungumuzia sana habari ya Ufalme wa Mungu kuliko habari zingine zote. Itakuwa vizuri kabisa tuchunguze habari hiyo ya maana. (Ufu. 5:9, 10; 14:1-3; 20:6) Kwa hiyo, acha tuchunguze kwanza sababu gani Yesu alizungumuzia sana Ufalme wa Mungu.

‘Kinywa Kinasema Yanayojaa Katika Moyo’

4. Ni nini inaonyesha kwamba Ufalme ndilo jambo la maana sana kwa Yesu?

4 Yesu aliona Ufalme kuwa jambo la maana sana. Ni nini inaonyesha hilo? Kwa kawaida, maneno tunayosema yanaonyesha yale yaliyo katika moyo wetu, ni kusema, maneno yetu yanaonyesha jambo ambalo tunapenda sana. Yesu mwenyewe alisema hivi: ‘Kinywa kinasema yanayojaa katika moyo.’ (Mt. 12:34) Kila mahali alipokuwa na watu, Yesu alizungumuza juu ya Ufalme. Katika vitabu ine vya injili neno Ufalme linarudiliwa zaidi ya mara 100. Yesu ndiye alirudilia neno hilo mara nyingi. Kichwa cha mahubiri yake kilikuwa ni Ufalme. Alisema hivi: ‘Ni lazima nihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa sababu nilitumwa kwa ajili hiyo.’ (Lu. 4:43, Biblia Habari Njema) Hata kisha kufufuka kwake, Yesu aliendelea kuwaelezea wanafunzi wake habari za Ufalme. (Mdo. 1:3) Bila shaka, moyo wa Yesu ulijaa na furaha sana kwa ajili ya Ufalme. Na hilo lilimuchochea kuzungumuza sana na watu juu ya Ufalme.

5-7. (a) Ni nini inaonyesha kwamba Ufalme ndilo jambo la maana sana kwa Yehova? Toa mufano. (b) Kila mumoja wetu anaweza kufanya nini ili kuonyesha kwamba Ufalme ndilo jambo la maana sana kwake?

5 Yehova pia anaona Ufalme kuwa jambo la maana. Sababu gani tunasema hivyo? Kumbuka jambo hili: Yehova alimutuma Mwana wake muzaliwa wa pekee katika ulimwengu; yote ambayo Yesu alisema na kufundisha yalitoka kwa Yehova. (Yoh. 7:16; 12:49, 50) Habari zote ambazo zinazungumuzia kazi ya kuhubiri na maisha ya Yesu ambazo zinapatikana katika vile vitabu ine vya injili zilitoka pia kwa Yehova. Hauone kwamba hilo ni jambo la maana sana?

6 Tuchukue mufano huu: unapenda kutia picha katika albumu yako. Una picha nyingi na unapaswa kuchagua ni picha gani utatia ndani ya albumu hiyo, lakini albumu hiyo ni ndogo. Utafanya nini? Bila shaka, utachagua kutia kwanza picha ambazo unapenda sana. Katika maana fulani, vitabu vya injili ni kama albumu hiyo ya picha. Vitabu hivyo vinatusaidia kumujua Yesu vizuri. Yehova hakuwaongoza waandikaji wa injili kuandika kila jambo ambalo Yesu alisema na kufanya wakati alikuwa hapa duniani. (Yoh. 20:30; 21:25) Roho ya Yehova iliwaongoza waandike tu maneno na matendo ya Yesu ambayo yanaweza kutusaidia tuelewe kusudi la kazi yake [Yesu] ya kuhubiri, na kuelewa pia mambo ambayo Yehova anaona kuwa ya lazima sana. (2 Tim. 3:16, 17; 2 Pet. 1:21) Kwa hiyo, kwa sababu vile vitabu ine vya injili vinajaa mafundisho ya Yesu juu ya Ufalme, tunaweza kusema bila kudanganyika kwamba Yehova anaona Ufalme kuwa jambo la maana sana. Fikiria jambo hili: Yehova anapenda wewe pia ujue kwamba Ufalme ni jambo la maana sana!

7 Kwa hiyo, kila mumoja wetu anapaswa kujiuliza hivi: ‘Je, mimi pia ninaona Ufalme wa Mungu kuwa jambo la maana sana?’ Ikiwa jibu letu ni ndiyo, tutapenda sana kusikiliza mambo ambayo Yesu alisema na kufundisha juu ya Ufalme, ni kusema, namna gani na wakati gani Ufalme utakuja, na sababu gani Ufalme ni jambo la maana.

‘Ufalme Wako Uje’—Utakuja Kufanya Nini?

8. Ni mambo gani Yesu alieleza kwa kifupi ili kuonyesha sababu gani Ufalme ni jambo la maana sana?

8 Acha tuzungumuzie ile sala ya mufano. Katika sala hiyo Yesu alitumia maneno mepesi lakini ya maana sana. Yesu alieleza kwa kifupi sababu gani Ufalme ni jambo la maana sana; alionyesha mambo ambayo Ufalme huo utatimiza. Sala hiyo inazungumuzia mambo saba. Mambo tatu ya kwanza yanazungumuzia kusudi la Yehova: 1) kutakaswa kwa jina la Yehova, 2) kuja kwa Ufalme, na 3) kutimizwa kwa mapenzi ya Mungu duniani kama mbinguni. (Soma Mathayo 6:9, 10.) Mambo hayo tatu yanazungumuzia jambo hili: Ufalme wa Masiya ni chombo ambacho Yehova atatumia ili kutakasa jina lake [Yehova] na kutimiza mapenzi yake.

9, 10. (a) Ufalme wa Mungu utafanya nini wakati utakuja? (b) Ni ahadi gani unatamani sana kuona zinatimia?

9 Ufalme wa Mungu utafanya nini wakati utakuja? Wakati katika sala yetu tunaomba kwamba ‘Ufalme wako uje,’ hilo linamaanisha, tunaomba kwamba Ufalme huo utende jambo fulani la maana. Wakati Ufalme huo utakuja, utaeneza mamlaka yake duniani pote. Utaondoa ulimwengu huu muovu, na serikali zote za wanadamu, na pia utaanzisha ulimwengu mupya wenye haki. (Dan. 2:44; 2 Pet. 3:13) Kisha, Ufalme huo utaifanya dunia yote kuwa paradiso. (Lu. 23:43) Watu waliokufa na ambao wanapatikana katika kumbukumbu la Mungu, watafufuliwa na kukaribishwa na watu waliowapenda. (Yoh. 5:28, 29) Wanadamu watiifu watakuwa wakamilifu na watafurahia kuishi milele. (Ufu. 21:3-5) Mwisho wa yote, kutakuwa na upatano kabisa kati ya mbingu na dunia. Hayo ndio mapenzi ya Yehova Mungu! Bila shaka, unatamani sana kuona namna ahadi hizo za Mungu zitatimizwa, sivyo? Usisahau jambo hili: kila wakati unasali kwamba Ufalme wa Mungu uje, hilo linamaanisha unaomba ahadi hizo zitimie.

10 Kuna mambo ambayo yanaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu ‘haujakuja’ ili kutimiza ile sala ya mufano. Kwa mufano, serikali za wanadamu zinaendelea kutawala na hatujaona ule ulimwengu mupya wa haki. Hata hivyo, tuna habari njema hii: Ufalme wa Mungu umekwisha kuanza kutawala mbinguni. Tutazungumuzia jambo hilo katika sura inayofuata. Lakini, acha kwanza tuzungumuzie yale Yesu alisema ili kujua ni wakati gani Ufalme huo ungeanza kutawala na ungekuja wakati gani.

Ufalme wa Mungu Ungeanza Kutawala Wakati Gani?

11. Ni nini Yesu alionyesha kuhusu wakati Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala?

11 Yesu alionyesha wazi kwamba Ufalme haungeanza kutawala wakati alikuwa hapa duniani, hata ikiwa mitume wake wengine walitumaini hivyo. (Mdo. 1:6) Tuchunguze mufano ambao Yesu alitoa katika mwaka wa 31 na ule ambao alitoa katika mwaka wa 33.

12. Sababu gani mufano wa ngano na magugu unaonyesha kwamba Ufalme haungeanza kutawala wakati Yesu alikuwa duniani?

12 Mufano wa ngano na magugu. (Soma Mathayo 13:24-30.) Yesu aliwatolea wasikilizaji wake mufano wa ngano na magugu, katika mwaka wa 31, (pengine kuanzia mwezi wa 3 mupaka mwezi wa 6). Kisha alifasiria wanafunzi wake maana ya mufano huo. (Mt. 13:36-43) Maana ya mufano huo na wazo kubwa ni hili: Kisha kufa kwa mitume, Shetani angepanda magugu (watu wanaojidai kuwa Wakristo) katikati ya ngano (“wana wa Ufalme,” ni kusema, Wakristo watiwa-mafuta). Bwana wa shamba aliacha ngano na magugu yakomalie pamoja mupaka wakati wa kipindi cha mavuno, ni kusema, ‘umalizio wa mufumo wa mambo.’ Kisha kipindi cha mavuno kuanza, magugu yangekusanywa. Kisha, ngano ingekusanywa pia. Kwa hiyo, mufano huo ulionyesha kwamba Ufalme haungeanza kutawala wakati Yesu alikuwa duniani, lakini ungeanza kutawala tu mwisho wa kipindi cha kukomaa kwa ngano pamoja na magugu. Mambo yalitokea hivi: katika mwaka wa 1914, kipindi cha kukomaa kilifikia mwisho wake na kipindi cha mavuno kikaanza.

13. Ni mufano gani Yesu alitoa ili kuonyesha kwamba hangewekwa kuwa Masiya-Mufalme mara moja tu kisha kurudi mbinguni?

13 Mufano wa mina. (Soma Luka 19:11-13.) Yesu alitoa mufano huo wa mina katika mwaka wa 33; alikuwa katika safari yake ya mwisho ya kuenda Yerusalemu. Wasikilizaji wake wengine walifikiri kwamba Yesu ataanza kutawala katika Ufalme wake kisha tu wao kufika Yerusalemu. Lakini, Yesu aliwasaidia waone kwamba mawazo yao hayakuwa ya kweli na kwamba kungepita muda murefu mbele ya Ufalme kuanza kutawala. Kwa hiyo aliwatolea mufano wa mina. Katika mufano huo alijilinganisha na ‘mutu fulani wa ukoo mashuhuri (ao ukoo wa kifalme)’ ambaye alifanya safari na kuenda ‘inchi ya mbali ili apewe mamlaka ya kifalme.’ * Katika mufano huo, ‘inchi ya mbali’ ambako Yesu alienda ili Baba yake amupatie Ufalme ilikuwa ni mbinguni. Lakini, Yesu alijua kwamba hatawekwa kuwa Masiya-Mufalme mara moja tu kisha kurudi mbinguni. Alijua kwamba alipaswa kwanza kukaa kwenye mukono wa kuume wa Mungu na kungojea mupaka wakati uliowekwa. Mambo yalitokea hivi: Kungojea huko kulichukua miaka mingi.—Zab. 110:1, 2; Mt. 22:43, 44; Ebr. 10:12, 13.

Ufalme wa Mungu Utakuja Wakati Gani?

14. (a) Ni jibu gani Yesu aliwapatia wanafunzi wake ine? (b) Kutimizwa kwa unabii wa Yesu kunatusaidia kujua nini juu ya kuwapo kwake na juu ya Ufalme?

14 Siku kidogo mbele ya Yesu kuuawa, mitume wake ine walimuuliza hivi: ‘Ni nini itakayokuwa ishara [alama] ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mufumo wa mambo?’ (Mt. 24:3; Mk. 13:4) Katika jibu lake, Yesu aliwatolea unabii ambao unapatikana katika Mathayo sura 24 na 25, na aliwaelezea namna unabii huo ungetimia kwa kiasi kikubwa. Yesu aliwaelezea kwa kirefu matukio mbalimbali ambayo yanapaswa kutokea katika ulimwengu. Matukio hayo yangeonyesha kwamba tunaishi kipindi cha “kuwapo” kwake. Kwa hiyo, mwanzo wa kipindi cha kuwapo kwake ndio wakati Ufalme pia ungeanza kutawala; na mwisho wa kipindi cha kuwapo kwake ndio wakati Ufalme utakuja kutawala dunia yote. Mambo mengi yanasadikisha kwamba unabii wa Yesu umeanza kutimia tangu mwaka wa 1914. * Kwa hiyo, mwaka huo ulitia alama ambayo inaonyesha kwamba kipindi cha kuwapo kwa Yesu kimeanza na kwamba Ufalme umeanza kutawala.

15, 16. Maneno “kizazi hiki” yanazungumuzia watu gani?

15 Sasa, ni wakati gani kabisa Ufalme wa Mungu utakuja? Yesu hakusema kabisakabisa ni siku gani Ufalme huo utakuja. (Mt. 24:36) Lakini, kuna jambo fulani alisema ambalo linatuhakikishia kwamba Ufalme huo unakaribia sana. Yesu alisema kwamba Ufalme huo ungekuja kisha “kizazi hiki” kuona utimizo wa alama ambayo alitabiri. (Soma Mathayo 24:32-34.) Maneno “kizazi hiki,” yanazungumuzia watu gani? Acha sasa tuchunguze maneno hayo ya Yesu.

16 “Kizazi hiki.” Je, maneno “kizazi hiki” yanamaanisha watu wasioamini? Hapana. Fikiria ni nani waliokuwa wasikilizaji wa Yesu wakati huo. Yesu alikuwa anaelezea unabii huo mitume wake ine ambao ‘walimukaribia faragani [peke yao].’ (Mt. 24:3) Kisha muda kidogo mitume wangetiwa mafuta kwa roho takatifu. Angalia pia maandiko mengine ya unabii huo. Mbele ya Yesu kusema juu ya “kizazi hiki,” alisema hivi: ‘Basi jifunzeni jambo hili kutokana na mutini kama mufano: Mara tu tawi lake changa linapokuwa jororo [teketeke] na kutoa majani, munajua kwamba kiangazi [majira ya jua kali] kiko karibu. Vilevile ninyi pia, wakati munaona mambo yote hayo, mujue kwamba iko karibu milangoni.’ Ni wafuasi watiwa-mafuta tu, ndio wangeona mambo ambayo yalitabiriwa na kuelewa maana ya mambo hayo, ni kusema, kuelewa kwamba Yesu ‘iko karibu milangoni.’ Lakini watu wasioamini hawangeelewa mambo hayo. Kwa hiyo, wakati Yesu alitumia maneno “kizazi hiki” alikuwa anafikiria wafuasi wake watiwa-mafuta.

17. Neno “kizazi” na maneno “mambo yote hayo” yanamaanisha nini?

17 ‘Hakitapita kamwe mupaka mambo yote hayo yatokee.’ Maneno hayo yangetimia namna gani? Ili kujibu ulizo hilo, tunapaswa kwanza kujua mambo mawili: 1) maana ya neno “kizazi;” na 2) maana ya maneno “mambo yote hayo.” Mara nyingi neno “kizazi” linamaanisha watu wa miaka tofauti, ambao maisha yao yanapatana katika kipindi fulani cha wakati. Kwa kawaida kizazi hakichukue muda murefu kupita kiasi, na kina mwisho wake. (Kut. 1:6) Maneno “mambo yote hayo,” yanamaanisha matukio yote ambayo yalitabiriwa kwamba yatatokea wakati wa kipindi cha kuwapo kwa Yesu, ni kusema, kuanzia mwanzo wa kipindi hicho katika mwaka wa 1914 mupaka mwisho wa ile ‘ziki kubwa.’—Mt. 24:21.

18, 19. Namna gani tunaweza kuelewa maneno ya Yesu kuhusu “kizazi hiki,” na kwa hiyo tunaweza kusema nini?

18 Kwa hiyo, namna gani tunaweza kuelewa maneno ya Yesu kuhusu “kizazi hiki”? Kile kizazi kinachozungumuziwa ni vikundi viwili vya Wakristo watiwa-mafuta ambao maisha yao yanapatana katika kipindi fulani cha wakati. Kikundi cha kwanza ni wale watiwa-mafuta ambao waliona mwanzo wa utimizo wa alama katika mwaka wa 1914. Na kikundi cha pili ni wale watiwa-mafuta ambao wakati fulani waliishi kipindi kimoja na kikundi hicho cha kwanza. Hata hivyo, wamoja kati ya wale watiwa-mafuta wa kikundi cha pili wataona mwanzo wa ile ziki kubwa. Vikundi hivyo viwili vinafanyiza kizazi kimoja kwa sababu wakati fulani viliishi katika kipindi kimoja. *

19 Tuseme nini basi? Tunajua kwamba alama ya kuwapo kwa Yesu katika Ufalme inaonekana wazi katika dunia yote. Pia, tunaona kwamba wale Wakristo watiwa-mafuta, ambao wangali wazima na wanaofanyiza sehemu ya “kizazi hiki” wamezeeka. Lakini, hawatakufa wote mbele ya ziki kubwa kuanza. Kwa hiyo, tunaweza kusema kwamba karibuni kabisa Ufalme wa Mungu utakuja na kutawala dunia yote! Tutakuwa wenye furaha sana kujionea utimizo wa maneno haya: ‘Ufalme wako uje’! Maneno yanayopatikana katika sala ambayo Yesu alitufundisha.

20. Katika kitabu hiki tutajifunza habari gani za maana sana, na sura ya pili itazungumuzia mambo gani?

20 Basi, tusisahau hata kidogo yale maneno ambayo Yehova mwenyewe alisema kutoka mbinguni. Alisema hivi kuhusu Mwana wake: ‘Mumusikilize yeye.’ Kwa sababu sisi ni Wakristo wa kweli, tuko tayari kutii maneno hayo ya Mungu. Tunapendezwa sana na kila neno ambalo Yesu alisema na kufundisha juu ya Ufalme wa Mungu. Katika kitabu hiki tutajifunza habari za maana sana. Tutajifunza mambo ambayo Ufalme huo umekwisha kutimiza na mambo utatimiza wakati unaokuja. Sura ya pili itazungumuzia mambo yaliyotokea wakati Ufalme wa Mungu ulizaliwa huko mbinguni.

^ fu. 13 Pengine mufano wa Yesu uliwakumbusha vizuri wasikilizaji wake kuhusu Arkelao, mwana wa Herode Mukubwa. Mbele ya Herode kufa, alimuchagua Arkelao kuwa muriti wake ili kutawala Yudea na maeneo mengine. Hata hivyo, mbele ya Arkelao kuanza kutawala, alipaswa kwanza kufanya safari murefu ya kuenda Roma ili kupata ruhusa ya Kaisari Augusto.

^ fu. 18 Mutu yeyote ambaye alitiwa-mafuta kisha kufa kwa mutiwa-mafuta wa mwisho wa watiwa-mafuta wa kikundi cha kwanza, ni kusema, kikundi cha wale watiwa-mafuta walioona “mwanzo wa maumivu ya taabu” katika mwaka wa 1914, yeye hangeonwa kuwa mumoja wa “kizazi hiki.”​—Mt. 24:8.

Kila mumoja wetu anapaswa kujiuliza hivi: ‘Je, mimi pia ninaona Ufalme wa Mungu kuwa jambo la maana sana?’