Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 3

Yehova Anafunua Kusudi Lake

Yehova Anafunua Kusudi Lake

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Yehova anafunua na kuelewesha kusudi lake hatua kwa hatua.Lakini, anafanya hivyo kwa wale tu wanaomuogopa

1, 2. Namna gani Yehova amewafunulia watumishi wake kusudi lake?

WAZAZI wenye kupenda watoto wao wanazungumuza mambo ya familia pamoja nao. Hata hivyo, wazazi waangalifu hawatawaambia watoto wao mambo yote mara moja. Lakini, watazungumuzia tu mambo yanayofaa watoto wao kwa wakati huo.

2 Vilevile, hapa duniani Yehova amewafunulia watumishi wake kusudi lake hatua kwa hatua. Lakini amefanya hivyo tu wakati aliona kwamba huo ndio wakati unaofaa. Tuchunguze sasa kwa kifupi namna katika historia Yehova amefunulia watumishi wake kweli mbalimbali juu ya Ufalme.

Sababu Gani Iliomba Kuwe Ufalme?

3, 4. Yehova amepanga kimbele mambo yanayowapata wanadamu? Fasiria jibu lako.

3 Mwanzoni, Yehova hakukusudia kuwe Ufalme wa Masiya. Sababu gani? Kwa sababu Mungu hakupangia kimbele mambo yanayowapata wanadamu. Zaidi ya hilo, aliwaumba wanadamu na uhuru wa kuchagua. Wakati aliumba Adamu na Eva, aliwaambia kusudi lake juu ya wanadamu. Aliwaambia hivi: ‘Muzae, muwe wengi, mujaze dunia na kuitiisha.’ (Mwa. 1:28) Tena, Yehova aliwaomba watii kanuni zake za mema na mabaya. (Mwa. 2:16, 17) Adamu na Eva walikuwa na uhuru wa kuchagua ikiwa watabakia waaminifu kwa Mungu ao hapana. Kama wao na watoto wao wangebakia waaminifu, hatungekuwa na lazima ya Ufalme unaongozwa na Kristo ili kutimiza kusudi la Mungu. Leo, dunia yote ingejaa watu wakamilifu wenye kumuabudu Yehova.

4 Uasi wa Shetani, wa Adamu, na wa Eva, haukumuzuia Yehova aendelee na kusudi lake la kufanya dunia ijae familia ya wanadamu wakamilifu. Alitafuta njia ingine ili kutimiza kusudi hilo. Kusudi lake si kama treni (gari-moshi) ambayo inapaswa tu kufuata njia ileile ili kufika mahali fulani ao ambayo inaweza kuanguka kwa sababu watu wabaya wameondoa vyuma vya njia yake ao wameweka kizuizi fulani. Kisha Yehova kusema kusudi lake, hakuna kitu ao mutu katika ulimwengu anayeweza kuzuia lisitimizwe. (Soma Isaya 55:11.) Kama kwenye njia hii kunakuwa jambo ao kitu kinachotaka kuzuia kusudi lake, Yehova anatumia njia ingine. * (Kut. 3:14, 15) Na wakati anaona inafaa, ndio wakati anawajulisha watumishi wake waaminifu juu ya njia mupya atakayotumia ili kutimiza kusudi lake.

5. Wakati uasi ulitokea katika Edeni, Yehova alikusudia kufanya nini?

5 Wakati uasi ulitokea katika Edeni, Yehova alikusudia kuanzisha Ufalme. (Mt. 25:34) Wakati ilionekana kwamba hakuna tumaini lolote kwa wanadamu, ndio wakati Yehova alifunua chombo ambacho atatumia ili kurudishia wanadamu hali yao ya kwanza; na pia kuondoa matatizo yote ambayo Shetani aliletea wanadamu kwa sababu ya tamaa yake ya kutafuta kunyanganya mamlaka. (Mwa. 3:14-19) Hata hivyo, Yehova hakufunua habari zote mara moja juu ya Ufalme huo.

Yehova Anaanza Kufunua Kweli Mbalimbali Juu ya Ufalme

6. Yehova aliahidi nini, lakini hakufunua nini wakati huo?

6 Kupitia unabii wa kwanza kabisa, Yehova aliahidi kwamba kutakuwa na “uzao” fulani ambao utamuponda ule nyoka. (Soma Mwanzo 3:15.) Hata hivyo, kwa wakati huo Yehova hakufunua ni nani atakuwa uzao wa mwanamuke na ni nani uzao wa ule nyoka. Kwa kweli, kulipita miaka 2000 hivi mbele Yehova aanze kuwapatia watumishi wake habari zaidi juu ya uzao huo. *

7. Sababu gani Mungu alimuchagua Abrahamu, na hilo linatufundisha nini?

7 Kisha, Yehova alimuchagua Abrahamu na akafunua kwamba uzao ulioahidiwa utakuja kupitia Abrahamu. Abrahamu alichaguliwa kwa sababu alikuwa ‘anasikiliza sauti ya Yehova.’ (Mwa. 22:18) Habari hiyo inatufundisha jambo hili la maana sana: Yehova anafunua kusudi lake kwa wale tu wanaomuogopa na kumuheshimu.​—Soma Zaburi 25:14.

8, 9. Ni habari gani za maana juu ya uzao ulioahidiwa Yehova alifunulia Abrahamu na Yakobo?

8 Yehova alizungumuza na rafiki yake Abrahamu kupitia malaika. Wakati huo, Yehova alifunua kwa mara ya kwanza habari ya maana sana juu ya uzao ulioahidiwa. Alionyesha kama uzao huo utakuwa mwanadamu. (Mwa. 22:15-17; Yak. 2:23) Lakini, namna gani mwanadamu huyo angemuponda ule nyoka? Nyoka huyo ni nani? Habari zingine ambazo Mungu alifunua kisha zingesaidia kupata majibu ya maulizo hayo.

9 Yehova aliamua kwamba uzao ulioahidiwa utokee kupitia Yakobo, mutoto wa mutoto wa Abrahamu. Yakobo alimuamini Mungu sana. (Mwa. 28:13-22) Yehova alifunua kupitia Yakobo kwamba Yule Aliyeahidiwa atatokea katika uzao wa Yuda, ambaye ni mutoto wa Yakobo. Yakobo alitabiri kwamba yule ambaye atatokea katika uzao huo wa Yuda atapokea “fimbo ya enzi.” Fimbo hiyo, inaonyesha mamlaka ya ufalme. Tena alitabiri kwamba ‘vikundi vya watu vitamutii yeye.’ (Mwa. 49:1, 10) Kupitia maneno hayo, Yehova alionyesha kwa mara ya kwanza kwamba Yule Aliyeahidiwa atakuwa mutawala, ni kusema, mufalme.

10, 11. Sababu gani Yehova alifunulia Daudi na Danieli kusudi lake?

10 Miaka 650 hivi kisha kufa kwa Yuda, Yehova alimufunulia Mufalme Daudi, aliyezaliwa katika uzao wa Yuda, habari zaidi juu ya kusudi lake. Yehova alionyesha kwamba Daudi ni ‘mutu anayekubalika kwa moyo wake.’ (1 Sam. 13:14; 17:12; Mdo. 13:22) Kwa sababu Daudi alimuheshimu Mungu na kumuogopa, Yehova aliamua kufanya agano naye. Alimuahidi kwamba mumoja kati ya wazao wake atakuwa mutawala milele.​—2 Sam. 7:8, 12-16.

11 Kisha miaka 500 hivi, kupitia nabii Danieli Yehova alifunua ule mwaka wenye Mutiwa-mafuta, ni kusema, Masiya atatokea duniani. (Dan. 9:25) Yehova alimuona Danieli kuwa ‘mutu mwenye kuheshimiwa sana (ao wa maana sana).’ Sababu gani? Kwa sababu Danieli alikuwa anamuheshimu Yehova sana na alimutumikia siku zote.​—Dan. 6:16; 9:22, 23.

12. Nabii Danieli aliambiwa afanye nini, na sababu gani?

12 Ni kweli kwamba Yehova alitumia manabii waaminifu kama vile Danieli ili kuandika habari nyingi juu ya uzao ulioahidiwa, ni kusema, Masiya. Hata hivyo, wakati wa Yehova ulikuwa haujafika ili watumishi wake waelewe kabisa maana ya mambo ambayo roho yake iliwaongoza kuandika. Kwa mufano, kisha Danieli kupewa maono ya wakati Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala, aliambiwa afunge kitabu hicho cha unabii kwa muhuri mupaka wakati uliotiwa na Yehova. Wakati huo utakapofika ndipo ujuzi wa kweli “utakuwa mwingi.”​—Dan. 12:4.

Yehova alitumia manabii waaminifu kama vile Danieli ili kuandika habari nyingi juu ya Ufalme wa Masiya

Yesu Anafunua Kusudi la Mungu

13. (a) Uzao ulioahidiwa ni nani? (b) Namna gani Yesu alifunua waziwazi unabii ulioandikwa katika kitabu cha Mwanzo 3:15?

13 Yehova alionyesha wazi kwamba Yesu ndiye uzao ulioahidiwa; alizaliwa katika uzao wa Daudi na ni yeye atakuwa Mufalme. (Lu. 1:30-33; 3:21, 22) Wakati Yesu alianza kazi yake ya kuhubiri, ilikuwa kama vile jua limetokea ili kuangazia wanadamu kujua kusudi la Mungu. (Mt. 4:13-17) Kwa mufano, Yesu alionyesha waziwazi ni nani “ule nyoka” aliyetajwa katika andiko la Mwanzo 3:14, 15. Alimuita Ibilisi huyo kuwa ni “muuaji” na ‘baba wa uongo.’ (Yoh. 8:44) Kupitia Ufunuo ambao Yesu alimupatia Yohana, Yesu anaonyesha kwamba “yule nyoka wa zamani” ni “yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani.” *(Soma Ufunuo 1:1; 12:9.) Katika ufunuo huohuo, Yesu alionyesha namna yeye ambaye ni uzao ulioahidiwa, atatimiza unabii ambao Yehova alitabiri katika bustani ya Edeni, ni kusema, kumuponda Shetani ili asikuwe tena.​—Ufu. 20:7-10.

14-16. Wafuasi wa Yesu walikuwa wanaelewa kabisa mara moja maana ya kweli mbalimbali ambazo Yesu alikuwa anawafunulia? Fasiria jibu lako.

14 Kama tulivyoona kwenye Sura ya 1, Yesu alisema mambo mengi juu ya Ufalme. Hata hivyo, hakuwa anatoa habari zote ambazo wanafunzi wake walipenda kujua. Hata kama aliwatolea mafasirio fulani, alifanya hivyo nyuma, ni kusema, kisha miaka mingi ndipo wafuasi wa Kristo walianza kuelewa kabisa maana ya kweli mbalimbali ambazo Bwana wao alikuwa amewafunulia. Acha tukamate mifano fulani.

15 Katika mwaka wa 33, Yesu alionyesha waziwazi kwamba wale ambao watatawala pamoja na Mufalme wa Ufalme wa Mungu watatoka duniani na kwamba watafufuliwa na kuwa viumbe vya kiroho na kuenda mbinguni. Wanafunzi wake hawakuelewa mara moja habari hiyo. (Dan. 7:18; Yoh. 14:2-5) Katika mwaka uleule, Yesu alitumia mifano ili kuonyesha kwamba angepanda kwanza mbinguni, na kisha miaka mingi kupita, ndipo Ufalme ungeanza kutawala. (Mt. 25:14, 19; Lu. 19:11, 12) Wanafunzi wake hawakuelewa fundisho hilo la maana, na ndio sababu wakati Yesu alifufuka, walimuuliza hivi: “Unarudishia Israeli ufalme wakati huu?” Yesu aliona si vizuri kuwatolea habari yoyote ya zaidi wakati ule. (Mdo. 1:6, 7) Yesu alifundisha pia kwamba, kutakuwa “kondoo wengine,” ambao hawatakuwa katika “kundi ndogo” la wale ambao watatawala pamoja naye. (Yoh. 10:16; Lu. 12:32) Wanafunzi wa Kristo walielewa vizuri tofauti kati ya vikundi hivyo viwili kisha Ufalme wa Mungu kuanza kutawala katika mwaka wa 1914.

16 Yesu alikuwa na mambo mengi ambayo angeweza kuwaambia wanafunzi wake wakati alikuwa hapa duniani. Lakini alijua kwamba hawangeweza kuyaelewa wakati ule. (Yoh. 16:12) Ni kweli kwamba wakati wa mitume, ujuzi fulani juu ya Ufalme ulifunuliwa. Lakini, wakati ulikuwa haujafika ili ujuzi huo uwe mwingi.

Katika “Wakati wa Mwisho” Ujuzi wa Kweli Unakuwa Mwingi

17. Tunapaswa kufanya nini kama tunataka kuelewa kweli mbalimbali za Ufalme, lakini inaomba tena nini?

17 Yehova alimuambia Danieli kwamba “wakati wa mwisho,” watu wengi “wataenda huku na huku, na ujuzi wa kweli” wa kusudi la Mungu utakuwa mwingi. (Dan. 12:4) Wote wanaopenda ujuzi huo wanapaswa kufanya nguvu ili kuupata. Kitabu kimoja kinasema kwamba neno la Kiebrania linalotafsiriwa na maneno ‘kuenda huku na huku’ linatoa wazo la mutu anayechunguza kitabu mwanzo mupaka mwisho kwa uangalifu sana. Hata kama sisi tunaisoma Biblia mwanzo mupaka mwisho, hatuwezi kabisa kuelewa kweli mbalimbali kuhusu Ufalme ikiwa Yehova hatusaidie kuzielewa.—Soma Mathayo 13:11.

18. Namna gani wale wanaomuogopa Yehova walionyesha kwamba wana imani na unyenyekevu?

18 Yehova alifunua kweli mbalimbali juu ya Ufalme hatua kwa hatua katika kipindi kilichoongoza kwenye mwaka wa 1914. Vilevile anaendelea kufanya hivyo katika kipindi hiki cha mwisho. Sura ya 4 na ya 5 ya kitabu hiki inaonyesha kwamba katika miaka 100 iliyopita, wakati fulani watu wa Mungu walilazimika kubadilisha namna walikuwa wanaelewa mafundisho fulani. Je, jambo hilo linaonyesha kama Yehova haunge mukono watumishi wake? Hapana! Tofauti na hilo anawaunga mukono. Sababu gani tunasema hivyo? Kwa sababu wale ambao wanamuogopa Yehova wameonyesha sifa mbili ambazo Mungu anapenda, ni kusema, imani na unyenyekevu. (Ebr. 11:6; Yak. 4:6) Watumishi wa Yehova wanaamini kwamba ahadi zote zenye kuandikwa katika Neno lake zitatimia. Wanaonyesha kama wao ni wanyenyekevu wakati wanakubali kwamba hawakuelewa vizuri namna ahadi hizo zingetimia. Hali yao ya unyenyekevu ilionyeshwa katika habari iliyotolewa katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 3, 1925, ambalo lilisema: “Tunajua kwamba Bwana yeye mwenyewe ndiye anafafanua Neno lake, na kwamba atalifafanulia watu wake namna anavyopenda na kwa wakati anaona kwamba unafaa.”

“Bwana . . . anafafanua Neno lake kwa watu wake namna anavyopenda na kwa wakati anaona kwamba unafaa”

19. Yehova amefanya tuelewe nini leo, na ni sababu gani?

19 Wakati Ufalme ulianza kutawala katika mwaka wa 1914, watu wa Mungu hawakujua kabisa namna unabii mbalimbali unaozungumuzia Ufalme ungetimia. (1 Kor. 13:9, 10, 12) Kwa sababu tulikuwa na hamu sana ya kuona utimizo wa ahadi za Mungu, kuna wakati tulikosea katika kuelewa mambo fulani. Kwa miaka mingi, hekima ya maneno mengine ambayo yanapatikana katika fungu la Munara wa Mulinzi ambao tumetaja hapo, imeonekana wazi. Habari hiyo ilisema hivi: “Inaonekana kuwa hiyo ndio kanuni nzuri kabisa ya kufuata. Kwamba tunaweza tu kuelewa unabii ukisha kutimia ao wakati unapotimia.” Kwa sababu sasa tumeingia sana katika wakati wa mwisho, unabii mbalimbali juu ya Ufalme umekwisha kutimia na unaendelea kutimia. Kwa sababu watu wa Mungu ni wanyenyekevu na wanakubali kurekebishwa, Yehova amefanya waelewe vizuri zaidi kusudi lake. Ujuzi wa kweli umekuwa mwingi!

Mafasirio Mapya Yanafanya Watu wa Mungu Wajaribiwe

20, 21. Sababu gani tunasema kwamba maelezo mapya yalikuwa jaribu kwa Wakristo wa wakati wa mitume?

20 Wakati Yehova anatusaidia tuelewe kweli vizuri zaidi, hali ya moyo wetu inajaribiwa. Imani yetu na unyenyekevu vitatuchochea tukubali mafasirio hayo mapya? Wakristo ambao waliishi wakati wa mitume walikutana na jaribu kama hilo. Kwa mufano, wazia unaishi wakati huo, na wewe ni Mukristo Muyahudi. Unaheshimu sana Sheria ya Musa na unajivunia kuwa Muisraeli. Kisha unapata barua iliyoandikwa na mutume Paulo kwa uongozi wa roho takatifu. Barua hiyo inasema kwamba si lazima tena kutii Sheria na kwamba Yehova amekataa Waisraeli wa kimwili na anapendelea sasa kukusanya Waisraeli wa kiroho. Kikundi hicho kinafanyizwa na Wayahudi na pia watu wasio Wayahudi. (Rom. 10:12; 11:17-24; Gal. 6:15, 16; Kol. 2:13, 14) Ungekubali mafasirio hayo mapya?

21 Wakristo wanyenyekevu walikubali mafasirio hayo ya mutume Paulo ambayo yaliongozwa na roho takatifu na walibarikiwa na Yehova. (Mdo. 13:48) Wengine walikataa kubadilisha namna walivyoelewa mambo na walipenda kubakia tu na mawazo waliyokuwa nayo mbele. (Gal. 5:7-12) Ikiwa watu hao wangekataa kubadilisha mawazo yao, wangepoteza pendeleo ambalo walikuwa nalo la kutawala pamoja na Kristo.​—2 Pet. 2:1.

22. Unayaona namna gani maelezo mapya juu ya kusudi la Mungu?

22 Katika miaka ya hivi karibuni, Yehova amefanya tuelewe vizuri zaidi kweli ya Ufalme. Kwa mufano, ametusaidia kujua vizuri zaidi ni wakati gani wale ambao watatawaliwa na Ufalme, ni kusema, watu walio mufano wa kondoo, watatenganishwa na wale wanaokataa kubadilika, ni kusema, wale walio mufano wa mbuzi. Yehova ametufundisha pia ni wakati gani hesabu ya watu 144000 itaenea. Tena ametusaidia kuelewa maana ya mifano ambayo Yesu alitoa juu ya Ufalme, na ni wakati gani mutiwa-mafuta wa mwisho atafufuliwa na kuenda mbinguni. * Unafurahia mafasirio hayo mapya? Imani yako inatiwa nguvu? Unaona mafasirio hayo kuwa ni ushuhuda wa kwamba Yehova anaendelea kufundisha watu wake wanyenyekevu? Habari ambazo zinapatikana katika kitabu hiki zitakufanya uamini kabisa kwamba Yehova anaendelea kufunua kusudi lake hatua kwa hatua kwa wale wanaomuogopa.

^ fu. 4 Jina la Mungu linatokana na neno la Kiebrania linalomaanisha “kuwa.” Jina Yehova linamaanisha kwamba yeye ni Mutimizaji wa ahadi zake. Soma kisanduku “Maana ya Jina la Mungu,” kwenye ukurasa 43.

^ fu. 6 Hata kama miaka hiyo inaweza kuonekana kuwa mingi sana leo, tukumbuke kwamba wakati huo ilikuwa kawaida watu kuishi miaka mingi sana; hivyo ni vizazi ine tu ambavyo viliishi kuanzia Adamu mupaka Abrahamu na kila kizazi kiliishi pamoja na kingine kwa wakati fulani. Adamu aliishi kwa wakati fulani pamoja na Lameki baba ya Noa. Lameki aliishi kwa wakati fulani pamoja na Shemu mwana wa Noa. Shemu aliishi kwa wakati fulani pamoja na Abrahamu.​—Mwa. 5:5, 31; 9:29; 11:10, 11; 25:7.

^ fu. 13 Jina “Shetani,” linapatikana mara 18 katika Maandiko ya Kiebrania. Lakini, katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, jina “Shetani” linapatikana zaidi ya mara 30. Inaonekana kwamba Maandiko ya Kiebrania hayakuzungumuzia sana Shetani, lakini yalikazia juu ya Masiya ili kumutambulisha. Wakati Masiya alifika, alimufunua Shetani waziwazi. Habari hiyo inaandikwa katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

^ fu. 22 Kama unapenda kuelewa namna mupya ya mafundisho fulani, soma habari ambazo zinafuata za Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 1995, ukurasa 23-28; wa tarehe 15 Mwezi wa 1, 2008, ukurasa 20-24; wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2008, ukurasa 17-21; wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2013, ukurasa 9-14.