Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA 4

Yehova Analitukuza Jina Lake

Yehova Analitukuza Jina Lake

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Watu wa Mungu wanalitukuza jina la Mungu kama inavyostahili

1, 2. Namna gani Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inalitukuza jina la Mungu?

ILIKUWA Siku ya Pili, tarehe 2 Mwezi wa 9, 1947. Asubui ya siku hiyo, ilikuwa yenye baridi na anga lilikuwa na jua lenye kuangaza; kikundi kidogo cha ndugu watiwa-mafuta wa Beteli ya Brooklyn katika New York, kilianza kutimiza kazi fulani kubwa na ya maana sana. Kazi hiyo ilichukua miaka 12. Ndugu hao walifanya kazi hiyo, hata kama ilikuwa nguvu na yenye kuomba mambo mengi. Siku ya Yenga tarehe 13 Mwezi wa 3, 1960 walimaliza maandishi ya mwisho ya tafsiri mupya ya Biblia. Kisha miezi tatu, ni kusema, tarehe 18 Mwezi wa 6, 1960, mukusanyiko wenye kufurahisha sana ulifanyika Manchester, Uingereza. Kwenye mukusanyiko huo, Ndugu Nathan Knorr alitolea watu buku la mwisho la Biblia TakatifuTafsiri ya Ulimwengu Mpya. Wahuzuriaji walifurahi sana. Ndugu Knorr alionyesha vizuri namna wahuzuriaji wote walivyojisikia, wakati alisema hivi: ‘Leo ni siku ya furaha kwa Mashahidi wa Yehova katika dunia yote!’ Jambo la maana sana na ambalo lilifurahisha sana watu kuhusu tafsiri hiyo mupya, ni kwamba tafsiri hiyo inatumia sana jina la pekee la Mungu.

Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitolewa katika mwaka 1950, kwenye mukusanyiko uliokuwa na kichwa Ukuzi wa Kiteokrasi (L’accroissement Théocratique)

2 Watafsiri wengi wa Biblia wameliondoa jina la Mungu katika Biblia zao. Lakini watumishi watiwa-mafuta wa Yehova walipinga mupango huo wa Shetani wa kuvuta jina la Mungu katika akili za watu. Maneno ya utangulizi ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ambayo ilitolewa siku hiyo yalisema hivi: “Jambo la maana sana katika Biblia hii ni kwamba ilirudisha jina la Mungu mahali pake.” Kwa kweli, Biblia hiyo inatumia jina la pekee la Mungu, ni kusema, Yehova, zaidi ya mara 7000. Ni jambo la maana sana kwamba Biblia hii imelitukuza jina la Baba yetu wa mbinguni, Yehova!

3. (a) Ndugu zetu walitambua nini juu ya maana ya jina la Mungu? (b) Namna gani tunapaswa kuelewa andiko la Kutoka 3:13, 14? (Soma kisanduku  “Maana ya Jina la Mungu.”)

3 Katika ile miaka ya mwanzo, wanafunzi wa Biblia walielewa kwamba jina la Mungu linamaanisha “Mimi Niko Ambaye Niko.” (Kut. 3:14, Union Version) Kwa hiyo, gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 1, 1926, lilisema hivi: “Jina Yehova linamaanisha Yule anayeishi, . . . Yule ambaye hana mwanzo wala mwisho.” Lakini, wakati watafsiri wa Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya walianza kazi yao, Yehova alikuwa amewasaidia watu wake kuelewa kama jina lake halimaanishe tu kama yeye anaishi, lakini zaidi sana kwamba Yeye ni Mungu wa kusudi na anayetenda. Walitambua kama wakati jina Yehova linatafsiriwa neno kwa neno linamaanisha “Yeye Anayefanya Kuwa.” Ndiyo, ni yeye aliyetokeza na kufanya ulimwengu na viumbe vyenye akili kuwa, na anaendelea kufanya mapenzi yake na kusudi lake kuwa kweli. Hata hivyo, sababu gani ni jambo la maana kabisa kulitukuza jina la Mungu, na namna gani tunaweza kuendelea kulitukuza?

Kutakaswa kwa Jina la Mungu

4, 5. (a) Wakati tunasali: “Jina lako litakaswe” ni nini kabisa tunaomba? (b) Namna gani na wakati gani Mungu atalitakasa jina lake?

4 Yehova anapenda jina lake litukuzwe. Kwa kweli, kusudi lake la kwanza ni kutakasa jina lake. Hilo linaonekana wazi katika maneno ya kwanza ya sala ya mufano ambayo Yesu alifundisha. Alisema hivi: “Jina lako na litakaswe.” (Mt. 6:9) Wakati tunasali hivyo, ni nini kabisa tunaomba?

5 Kama tulivyojifunza katikaSura ya 1, sala hiyo ya Yesu inazungumuzia kwanza mambo tatu ya maana. Kwanza, kutakaswa kwa jina la Mungu. Jambo hilo linahusiana na kusudi la Yehova. Pili, kuja kwa Ufalme wake, na tatu, kutimizwa kwa mapenzi yake. (Mt. 6:10) Kama vile tunamuomba Yehova achukue hatua ya kufanya Ufalme wake uje, na mapenzi yake yafanyike, vilevile tunamuomba achukue hatua ya kulitakasa jina lake. Ni kusema, tunamuomba Yehova mwenyewe achukue hatua ya kulisafisha jina lake ambalo limechafuliwa na uasi ambao ulitokea katika Edeni. Namna gani Yehova atajibu sala hiyo? Anasema hivi: ‘Nami hakika nitalitakasa jina langu kubwa, ambalo lilitiwa unajisi [ao uchafu] katikati ya mataifa.’ (Eze. 36:23; 38:23) Kwenye vita ya Har-magedoni, wakati Yehova ataondoa mambo yote mabaya, atalitakasa jina lake mbele ya viumbe vyote.

6. Namna gani tunaweza kulitakasa jina la Mungu?

6 Tangu zamani, Yehova ameruhusu watumishi wake walitakase pia jina lake. Ni wazi kwamba hatuwezi kufanya jina la Mungu liwe takatifu zaidi. Kwa sababu sikuzote jina hilo ni takatifu katika maana kamili. Kwa hiyo, namna gani tunaweza kulitakasa jina hilo? Nabii Isaya anasema hivi: ‘Yehova wa majeshi—yeye Ndiye munapaswa kuona kuwa mutakatifu.’ Na juu ya watu wake, Yehova mwenyewe alisema hivi: ‘Watalitakasa jina langu . . . , nao watamuheshimu Mungu wa Israeli.’ (Isaya 8:13; 29:23) Kwa hiyo, tunalitakasa jina la Mungu kwa kuliona kuwa ni jina lenye halilingane na majina mengine yote, na ni jina lenye kuwa juu sana kuliko majina mengine yote. Pia tunalitakasa kwa kuheshimu kile jina hilo linaonyesha, ni kusema, sifa zake na makusudi yake. Tena tunalitakasa jina hilo kwa kuwasaidia wengine kuliona kuwa takatifu. Tunaonyesha kabisa kama tunaliheshimu sana na kuliogopa jina la Mungu wakati tunatambua kwamba Yehova ni Mufalme wetu na wakati tunamutii kwa moyo wetu wote.—Met. 3:1; Ufu. 4:11.

Walitayarishwa Kuitwa kwa Jina la Mungu na Kutukuza Jina Hilo

7, 8. (a) Sababu gani ilichukua wakati murefu mbele watu wa Mungu waitwe kwa jina lake? (b) Sasa tutazungumuzia mambo gani?

7 Katika siku zetu, watumishi wa Mungu wamelitumia jina la Mungu katika vichapo vyao kuanzia miaka ya 1870. Kwa mufano gazeti Munara wa Mulinzi la Mwezi wa 8, 1879 lilitumia jina Yehova, na pia kitabu cha nyimbo Cantiques de l’Epouse (Nyimbo za Bibi-Arusi) kilichotokea katika mwaka huohuo kilifanya hivyo. Hata hivyo, inaonekana kwamba Yehova alipenda watu wake watimize kwanza sifa fulani ili wajitambulishe mbele ya watu wote kwamba wanastahili kuwa na pendeleo hilo kubwa la kuitwa kwa jina lake takatifu. Namna gani Yehova aliwatayarisha Wanafunzi hao wa Biblia waitwe kwa jina lake?

8 Wakati tunakumbuka miaka ya mwisho ya 1800 na ya mwanzo ya 1900, tunaona namna Yehova aliwasaidia watu wake kuelewa vizuri zaidi mafundisho ya kweli na ya maana juu ya jina lake. Acha tuzungumuzie mambo tatu kati ya mafundisho hayo.

9, 10. (a) Sababu gani habari za gazeti Munara wa Mulinzi zilikazia sana juu ya Yesu? (b) Kuanzia mwaka wa 1919 ni mabadiliko gani yalitokea, na hilo lilikuwa na matokeo gani? (Soma pia kisanduku “ Namna Gazeti Munara wa Mulinzi Lilitukuza Jina la ungu.”)

9 Jambo la kwanza: Watumishi wa Yehova, ni kusema, Wanafunzi wa Biblia wa kwanza-kwanza walifikia kuelewa vizuri zaidi kwamba jina la Mungu ni la maana. Wanafunzi hao waaminifu waliona fundisho la zabihu ya ukombozi kuwa fundisho la maana sana katika Biblia. Hiyo ndio sababu mara nyingi gazeti Munara wa Mulinzi lilikazia sana juu ya Yesu. Kwa mufano, katika mwaka wa kwanza wa kutolewa kwa gazeti hilo, jina Yesu lilitumiwa mara kumi zaidi kuliko jina Yehova. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 3, 1976, lilisema kwamba Wanafunzi wa Biblia wa kwanza-kwanza “walikazia sana juu ya Yesu kupita kiasi.” Lakini, kisha muda fulani, Yehova aliwasaidia kuelewa kwamba Biblia inaliheshimu sana jina la pekee la Mungu. Hilo lilikuwa na matokeo gani kwa Wanafunzi hao? Gazeti hilohilo la Munara wa Mulinzi lilisema kwamba zaidi sana tangu mwaka wa 1919, Wanafunzi wa Biblia “walianza kumuheshimu zaidi, Baba wa Masiya aliye Mbinguni, ni kusema, Yehova.” Ndio sababu, kuanzia mwaka wa 1920 mupaka mwaka wa 1929, gazeti Munara wa Mulinzi lilitumia jina la Mungu zaidi ya mara 6500!

10 Kwa kulipatia jina Yehova heshima ambayo linastahili, ndugu zetu hao walionyesha kwamba wanapenda jina la Mungu. Walianza ‘kulitangaza jina la Yehova,’ kama vile Musa alivyofanya. (Kum. 32:3; Zab. 34:3) Yehova pia aliona kwamba wanalipenda jina lake, kwa hiyo, akawakubali kama alivyoahidi katika Biblia.​—Zab. 119:132; Ebr. 6:10.

11, 12. (a) Muda kidogo tu kisha mwaka wa 1919, vitabu vyetu vilianza kukazia nini? (b) Ni nini Yehova alikuwa anapenda kuwaelewesha watumishi wake, na ni sababu gani alifanya hivyo?

11 Jambo la pili: Wakristo wa kweli walifikia kuelewa vizuri zaidi kazi ambayo Mungu aliwapatia. Muda kidogo kisha mwaka wa 1919, ndugu watiwa-mafuta ambao walikuwa wanaongoza kazi walichochewa kuchunguza unabii wa Isaya. Kisha hapo, habari zilizokuwa katika vichapo vyetu zilianza kukazia kazi hiyo. Sababu gani kuelewa mambo hayo vizuri zaidi ilikuwa ‘chakula kwa wakati unaofaa’?​—Mt. 24:45.

12 Mbele ya mwaka wa 1919, gazeti Munara wa Mulinzi lilikuwa halijazungumuzia jambo lolote juu ya maneno ya Isaya, yenye kusema hivi: “‘Ninyi ni mashahidi wangu, ’asema Yehova, ‘mutumishi wangu ambaye nimemuchagua.’” (Soma Isaya 43:10-12.) Lakini muda kidogo tu kisha mwaka wa 1919, vichapo vyetu vilianza kukazia ujumbe huo wa Biblia, na vilitia moyo watiwa-mafuta wote kuunga mukono kazi ambayo Yehova aliwapatia, ni kusema, kutoa ushahidi juu yake. Kwa hiyo, kuanzia mwaka wa 1925 mupaka mwaka wa 1931, kitabu cha Isaya sura ya 43 kilizungumuziwa katika habari 57 zilizotolewa katika Munara wa Mulinzi. Na kila habari ilionyesha kwamba maneno hayo yanazungumuzia Wakristo wa kweli. Ni wazi kabisa, katika miaka hiyo yote, Yehova alikuwa anaelewesha watumishi wake kazi ambayo walipaswa kufanya. Sababu gani Yehova alifanya hivyo? Ni kwa sababu “wajaribiwe juu ya kufaa kwanza.” (1 Tim. 3:10) Mbele wastahili kuitwa kwa jina la Mungu, Wanafunzi wa Biblia walipaswa kuonyesha Yehova kupitia matendo yao kwamba walikuwa kabisa mashahidi wake.—Lu. 24:47, 48.

13. Namna gani Neno la Mungu linafunua jambo la maana sana ambalo linapaswa kwanza kuhangaikiwa?

13 Jambo la tatu: Watu wa Yehova walifikia kuelewa kwamba kutakaswa kwa jina la Mungu ndilo jambo la maana sana. Kati ya mwaka wa 1920 na mwaka wa 1930, walielewa kwamba kutakaswa kwa jina la Mungu ndilo jambo la maana sana ambalo linapaswa kwanza kuhangaikiwa. Namna gani Neno la Mungu lilifunua kweli hiyo ya maana sana? Tufikirie maulizo haya mawili. Ni sababu gani kubwa ambayo ilimuchochea Mungu kuwaokoa Waisraeli kutoka Misri? Yehova alisema hivi: “Ili nifanye jina langu litangazwe katika dunia yote.” (Kut. 9:16) Na ni sababu gani Yehova aliwahurumia Waisraeli wakati walimuasi? Wakati huo pia, Yehova alisema hivi: “Nilichukua hatua kwa ajili ya jina langu mwenyewe ili lisitiwe unajisi [uchafu] mbele ya macho ya mataifa.” (Eze. 20:8-10) Habari hizo na zingine zenye kuwa katika Biblia, ziliwafundisha Wanafunzi wa Biblia nini?

14. (a) Watu wa Mungu walielewa nini mwisho-mwisho wa miaka 1920? (b) Kuelewa vizuri kwamba kutakaswa kwa jina la Mungu ndilo jambo la maana sana, kuliwachochea namna gani Wanafunzi wa Biblia kuhubiri? (Soma pia kisanduku “ Sababu Yenye Nguvu Inayochochea Kuhubiri.”)

14 Mwisho-mwisho wa miaka ya 1920, watu wa Mungu walielewa maana ya maneno ambayo nabii Isaya alisema kumepita miaka 2700 hivi. Alisema hivi juu ya Yehova: ‘Hivyo uliwaongoza watu wako ili ujifanyie mwenyewe jina nzuri.’ (Isa. 63:14) Wanafunzi wa Biblia walielewa kwamba kutakaswa kwa jina la Mungu ndilo jambo la maana sana kuliko wokovu wa mutu. (Isa. 37:20; Eze. 38:23) Katika mwaka wa 1929, kitabu Prophétie (Unabii) kilizungumuzia kwa kifupi ukweli huu: “Jina Yehova ni jambo la maana sana mbele ya viumbe vyote.” Kuelewa vizuri zaidi jambo hilo, kuliwachochea watumishi wa Mungu kutoa ushahidi juu ya Yehova, na kuliondolea jina la Mungu uongo ambao Shetani alisema juu ya jina hilo.

15. (a) Mwanzo-mwanzo wa miaka ya 1930, ni mambo gani ndugu zetu walikuwa wameelewa? (b) Yehova aliona kwamba watumishi wake wanastahili nini sasa?

15 Mwanzo-mwanzo wa miaka ya 1930, ndugu zetu walikuwa wameelewa vizuri zaidi sababu gani jina la Mungu ni la maana sana, na walielewa vizuri kazi yenye Mungu aliwapatia. Pia walikuwa wameelewa vizuri sana shitaka lililotokezwa juu ya jina la Mungu, na namna litaondolewa. Sasa, Yehova aliona kwamba watumishi wake wametayarishwa ili wastahili kuitwa kwa jina lake mbele ya watu wote. Ili kujua namna jambo hilo lilifanyika, ni vizuri tuzungumuzie mambo fulani yaliyotokea zamani.

Yehova Anachagua “Watu kwa Ajili ya Jina Lake”

16. (a) Ni njia gani moja kubwa Yehova anatumia ili kulitukuza jina lake? (b) Wakati wa zamani, ni nani kwanza waliitwa kwa jina la Mungu?

16 Njia moja kubwa ambayo Yehova anatumia ili kulitukuza jina lake, ni kuwa na watu duniani ambao wanaitwa kwa jina lake. Kuanzia mwaka wa 1513 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Waisraeli walijulikana kuwa taifa la Yehova, ni kusema, watu wake hapa duniani. (Isa. 43:12) Lakini walishindwa kutii agano ambalo walifanya pamoja na Mungu. Kwa hiyo, katika mwaka wa 33, walipoteza urafiki wa pekee pamoja na Mungu. Kisha, Yehova ‘alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.’ (Mdo. 15:14) Taifa hilo mupya lilijulikana kwa jina la “israeli la Mungu,” ni kusema, wafuasi watiwa-mafuta wa Kristo kutoka mataifa mbalimbali.​—Gal. 6:16.

17. Shetani kwa udanganyifu alifikia kusudi gani?

17 Katika mwaka wa 44 hivi, wanafunzi wa Kristo waliitwa Wakristo ‘kwa uongozi wa Mungu.’ (Mdo. 11:26) Mwanzoni, jina hilo liliwatofautisha na wengine, kwa sababu ni Wakristo wa kweli tu ndio waliitwa hivyo. (1 Pet. 4:16) Lakini, kama vile Yesu alionyesha katika mufano wake wa ngano na magugu, Shetani kwa udanganyifu alifikia kusudi lake la kufanya Wakristo wa uongo watumie pia jina hilo la Wakristo. Kwa hiyo, kwa miaka mingi, ilikuwa vigumu kutofautisha Wakristo wa kweli na Wakristo wa uongo. Lakini mambo yalianza kubadilika wakati wa kipindi cha mavuno ambacho kilianza katika mwaka wa 1914. Sababu gani tunasema hivyo? Kwa sababu katika kipindi hicho, malaika walianza kutenganisha Wakristo wa kweli na Wakristo wa uongo.​—Mt. 13:30, 39-41.

18. Ni nini iliwasaidia ndugu zetu kujua kwamba ilikuwa lazima waitwe kwa jina mupya?

18 Kisha kumuweka mutumwa mwaminifu na mwenye busara katika mwaka wa 1919, Yehova aliwasaidia watumishi wake kutambua kazi ambayo aliwapatia. Walielewa haraka kwamba kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba iliwatofautisha na Wakristo wote wa uongo. Muda mufupi kisha kutambua jambo hilo, walielewa kwamba haitoshe tu kuitwa “Wanafunzi wa Biblia” ili kuwa tofauti na wengine. Kusudi lao kubwa katika maisha si kujifunza tu Biblia, lakini kutoa ushahidi juu ya Mungu, kumuheshimu, na kulitukuza jina lake. Kwa hiyo, ni jina gani liliwastahili kulingana na kazi ambayo walikuwa wanafanya? Ulizo hilo lilijibiwa katika mwaka wa 1931.

Programu ya mukusanyiko, 1931

19, 20. (a) Ni azimio gani lenye kufurahisha sana ambalo lilitolewa kwenye mukusanyiko wa mwaka wa 1931? (b) Namna gani ndugu walionyesha furaha yao juu ya jina lao mupya?

19 Katika Mwezi wa 7, 1931, Wanafunzi wa Biblia 15000 hivi walikuja kuhuzuria mukusanyiko ambao ulifanyika katika muji wa Columbus, Ohio, États-Unis. Wakati waliona programu ya mukusanyiko, walivutiwa na herufi mbili kubwa​—J na W (katika Kiingereza)​—ambazo ziliandikwa kwenye programu hiyo. Walijiuliza ‘herufi hizo zinamaanisha nini?’ Wahuzuriaji walikuwa wanawazia-wazia tu. Kisha, Siku ya Yenga tarehe 26 Mwezi wa 7, Ndugu Joseph Rutherford alitangaza azimio lenye kuchochea kwa maneno haya: “Tunatamani kujulikana na kuitwa kwa jina hili, ni kusema, Mashahidi wa Yehova.” Wakati huo, wote katika huzurio walielewa sasa maana ya zile herufi mbili. Katika Kiingereza herufi hizo zilimaanisha, Jehovah’s Witnesses (ao Mashahidi wa Yehova). Jina hilo la Biblia, lilitegemea andiko la Isaya 43:10.

20 Wahuzuriaji walikubali azimio hilo kwa furaha kubwa, na walipiga mikono kwa muda murefu. Furaha hiyo katika muji wa Columbus ilisikilika katika sehemu za mbali za dunia kupitia radio! Ndugu Ernest Barber wa Australia na dada Naomi bibi yake, walikumbuka jambo hilo na walisema hivi: “Wakati ndugu walipiga mikono katika Amerika, ndugu wa Melbourne walisimama na kurukaruka na kuendelea kupiga mikono. Hatutasahau jambo hilo hata kidogo!” *

Jina la Mungu Linatukuzwa Duniani Pote

21. Namna gani jina hilo mupya lilisaidia watumishi wa Mungu kuwa na nguvu zaidi katika mahubiri?

21 Jina Mashahidi wa Yehova lenye kutegemea Biblia, lilifanya watumishi wa Mungu wawe na nguvu zaidi katika kazi ya kuhubiri. Ndugu Edward Grimes na bibi yake Jessie, mapainia katika États-Unis, walihuzuria mukusanyiko huo katika mwaka wa 1931 katika muji wa Columbus. Walisema hivi: “Tuliitwa Wanafunzi wa Biblia wakati tulitoka nyumbani, lakini wakati tulirudia nyumbani tulikuwa na jina la Mashahidi wa Yehova. Tulifurahi kwa sababu sasa tulikuwa na jina ambalo lilitusaidia kutukuza jina la Mungu wetu.” Kisha mukusanyiko huo, Mashahidi fulani walitumia njia mupya ili kutukuza jina la Mungu. Walijitambulisha kwa mwenye nyumba kwa kumupatia karte ambayo iliandikwa hivi: “Mimi ni shahidi wa YEHOVA anayehubiri Ufalme wa YEHOVA Mungu wetu.” Kwa kweli, watu wa Mungu walijivunia kuitwa kwa jina la Yehova, na walikuwa tayari kutangaza maana ya jina hilo mahali pote.​—Isa. 12:4.

“Tuliitwa Wanafunzi wa Biblia wakati tulitoka nyumbani, lakini wakati tulirudia nyumbani tulikuwa na jina la Mashahidi wa Yehova”

22. Ni nini inayoonyesha kwamba watu wa Yehova wana jina linalowatofautisha?

22 Kumepita miaka mingi tangu Yehova aliwachochea ndugu zetu watiwa-mafuta kuchukua jina linalowatofautisha. Kuanzia mwaka wa 1931, Shetani aliweza kufunika jina hilo la watu wa Mungu? Amefanya watu wasitutofautishe na dini zingine? Jibu ni hapana! Kuliko kuwa hivyo, jina letu la mashahidi wa Mungu ambalo linatutofautisha na dini zingine, linajulikana sana kuliko wakati mwingine wowote. (Soma Mika 4:5; Malaki 3:18.) Kwa sababu tumeshikamana sana na jina la Mungu, kila mutu anayetumia jina hilo leo, watu wanamuona mara moja kuwa Shahidi wa Yehova. Kuliko kufunikwa na dini za uongo zinazofananishwa na milima, ibada ya kweli ya Yehova ‘inawekwa imara juu ya kilele cha milima.’ (Isa. 2:2) Bila shaka leo, ibada ya Yehova na jina lake takatifu, vinatukuzwa ao kuinuliwa juu sana.

23. Kulingana na andiko la Zaburi 121:5, ni jambo gani la kweli na la maana sana juu ya Yehova linatutia nguvu sana?

23 Ni jambo lenye kutia nguvu kabisa kujua kwamba Yehova atatulinda na mashambulizi ya sasa na ya wakati unaokuja. (Zab. 121:5) Tuko na sababu nzuri ya kujisikia kama mutunga zaburi aliyeandika hivi: ‘Lenye furaha ni taifa ambalo Mungu wake ni Yehova, watu ambao amewachagua wawe uriti wake.’​—Zab. 33:12.

^ fu. 20 Soma Sura ya 7, ukurasa 72-74, ili kujua mambo mengi juu ya matumizi ya radio hiyo.