Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA 6

Watu Wanaofanya Kazi ya Kuhubiri—Wahubiri Wanajitoa Kwa Kupenda

Watu Wanaofanya Kazi ya Kuhubiri—Wahubiri Wanajitoa Kwa Kupenda

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Mufalme anatokeza jeshi la wahubiri

1, 2. Ni kazi gani kubwa ambayo Yesu alitabiri, na hilo linatokeza ulizo gani la maana?

MARA NYINGI viongozi wa siasa (politike) wanaahidi mambo mengi ambayo hawatimize. Hata wengine kati yao wenye kuwa na nia nzuri wanaweza kushindwa kutimiza mambo ambayo wameahidia watu. Jambo la kufurahisha ni kwamba Yesu ni tofauti na viongozi hao, kwa sababu yeye anatimiza ahadi zake kila wakati.

2 Kisha Yesu kuwekwa kuwa Mufalme katika mwaka wa 1914, alitimiza unabii ambao alikuwa ametoa kumepita miaka 1900 hivi. Wakati kidogo mbele ya kufa kwake, Yesu alisema hivi: ‘Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayoikaliwa.’ (Mt. 24:14) Kutimizwa kwa maneno hayo ingekuwa sehemu ya alama ya kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme. Hata hivyo, ulizo la maana ni hili: Kwa sababu katika siku za mwisho watu wangekuwa na tabia ya kujipenda wenyewe, ya kukosa upendo, na ya kutopenda mambo matakatifu, namna gani Mufalme angetokeza jeshi la wahubiri katika siku hizo? (Mt. 24:12; 2 Tim. 3:1-5) Ni vizuri tupate jibu la ulizo hilo, kwa sababu kila Mukristo wa kweli ni mumoja wa jeshi hilo la wahubiri.

3. Yesu alitumaini kabisa nini, na sababu gani alikuwa na tumaini kama hilo?

3 Fikiria tena maneno ya unabii wa Yesu. Wakati alisema “itahubiriwa,” alitumaini kabisa kwamba habari njema itahubiriwa? Bila shaka! Yesu alitumaini kwamba katika siku za mwisho, atakuwa na wahubiri ambao wangejitoa kwa kupenda. Sababu gani alikuwa na tumaini kama hilo? Alijifunza jambo hilo kwa Baba yake. (Yoh. 12:45; 14:9) Yesu aliishi mbinguni mbele ya kuja hapa duniani, na huko aliona kwamba Yehova alikuwa anatumaini waabudu Wake, kwa sababu walikuwa na roho ya kujitoa kwa kupenda. Acha sasa tujifunze namna Yehova alionyesha kwamba kila siku anawatumainia watumishi wake.

“Watu Wako Watajitoa kwa Kupenda”

4. Yehova aliwaomba Waisraeli wasaidie katika kazi gani, nao walionyesha roho gani?

4 Kumbuka jambo ambalo lilitokea wakati Yehova alimupatia Musa maagizo juu ya kujenga hema ya ibada, ambayo ilikuja kuwa nafasi ambako Waisraeli walikuwa wanakutana ili kumuabudu Yehova. Kupitia Musa, Yehova aliwaomba watu wote wasaidie katika kazi hiyo. Musa aliwaambia kwamba kila mutu ambaye ana moyo wa kutoa kwa kujipendea amuletee Yehova muchango. Matokeo yalikuwa namna gani? Watu waliendelea kuleta matoleo ya kujipendea kila asubui. Watu walileta vitu vingi sana, kwa hiyo, Musa aliwaambia wasilete tena kitu chochote. (Kut. 35:5; 36:3, 6) Waisraeli walionyesha kwamba Yehova alikuwa na sababu nzuri ya kuwatumainia.

5, 6. Kulingana na andiko la Zaburi 110:1-3, Yehova na Yesu walitazamia waabudu wa kweli waonyeshe roho gani katika siku hizi za mwisho?

5 Katika siku hizi za mwisho, Yehova alitazamia pia kuona roho kama hiyo kati ya watumishi wake? Ndiyo! Zaidi ya miaka 1000 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Yehova alimuongoza mufalme Daudi aandike juu ya mambo ambayo yangetokea wakati Masiya angeanza kutawala. (Soma Zaburi 110:1-3.) Yesu, Mufalme mupya, alipaswa kuwa na maadui ambao wangemupinga. Pia, angepaswa kuwa na jeshi la watu wenye kumuunga mukono. Watu hao, wangemutumikia Mufalme bila kulazimishwa. Hata vijana walio kati yao wangejitoa wenyewe kwa kupenda. Wangekuwa wengi sana, kwa hiyo wangestahili kulinganishwa na matone ya umande ambayo wakati wa jua la asubui yanafunika udongo. *

Wahubiri wenye kuunga Ufalme mukono na wenye kujitoa kwa kupenda ni wengi kama matone ya umande (Soma fungu la 5)

6 Yesu alijua kwamba angetimiza unabii ulioandikwa katika andiko la Zaburi 110. (Mt. 22:42-45) Kwa hiyo, alikuwa na sababu nzuri ya kutumaini kwamba atakuwa na watu waaminifu ambao watafanya kazi ya kuhubiri habari njema katika dunia yote kwa kujipendea. Historia ya watumishi wa Mungu imeonyesha nini? Je, Mufalme alitokeza kabisa jeshi la wahubiri wenye kujitoa kwa kupenda katika siku hizi za mwisho?

“Daraka Langu na Pendeleo Langu Ni Kutangaza Ujumbe Huo”

7. Kisha Yesu kuwekwa kuwa Mufalme, alichukua mupango gani ili kutayarisha wafuasi wake kwa ajili ya kazi ambayo walipaswa kufanya?

7 Wakati kidogo kisha Yesu kuwekwa kuwa Mufalme, alichukua mupango wa kuwatayarisha wafuasi wake kwa ajili ya kazi kubwa ambayo walipaswa kufanya. Kama vile tulijifunza katika Sura ya 2, Yesu alifanya kazi ya kuchunguza na ya kusafisha wafuasi wake kuanzia mwaka wa 1914 mupaka miezi ya mwanzo ya mwaka wa 1919. (Mal. 3:1-4) Kisha, katika mwaka wa 1919, alimuweka mutumwa mwaminifu ili aongoze wafuasi wake. (Mt. 24:45) Zaidi sana, kuanzia wakati huo mutumwa huyo alianza kutoa chakula cha kiroho, kupitia hotuba mbalimbali kwenye mikusanyiko na kupitia vichapo. Mara kwa mara, hotuba hizo na vichapo hivyo vimekazia kwamba kila Mukristo ana daraka la kuhubiri.

8-10. Namna gani mikusanyiko ilichochea ndugu kwa ajili ya kazi ya kuhubiri? Toa mufano. (Soma pia kisanduku “ Mikusanyiko ya Mwanzo-Mwanzo Ambayo Ilichochea Kazi ya Kuhubiri.”)

8 Hotuba mbalimbali kwenye mukusanyiko wa maana. Kwa sababu Wanafunzi wa Biblia walikuwa na hamu sana ya kupata muongozo, walikusanyika Cedar Point, Ohio, États-Unis, kuanzia tarehe 1 mupaka tarehe 8 Mwezi wa 9, 1919. Ulikuwa mukusanyiko mukubwa na wa kwanza ambao walifanya kisha Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Siku ya pili ya mukusanyiko huo, Ndugu Rutherford alitoa hotuba, na katika hotuba hiyo, aliwaambia waziwazi wahuzuriaji hivi: “Kazi ya kila Mukristo hapa duniani . . .. ni kuhubiri ujumbe wa Ufalme wa Bwana.”

9 Wazo kubwa la mukusanyiko huo, lilitolewa kisha siku tatu wakati Ndugu Rutherford alitoa hotuba yenye kichwa “Hotuba kwa Wale Wanaofanya Kazi Pamoja.” Hotuba hiyo ilitolewa pia katika gazeti Munara wa Mulinzi na ilikuwa na habari “Kutangaza Ufalme.” Ndugu Rutherford alisema hivi: “Wakati jambo fulani linamufanya Mukristo afikiri kwa uzito, kwa kawaida anajiuliza, sababu gani niko hapa duniani? Na jibu lake linapaswa kuwa hivi, Kwa fazili zake zisizostahiliwa, Bwana amenifanya kuwa ambasadere wake ili kuupelekea ulimwengu ujumbe wa upatanisho. Daraka langu na pendeleo langu ni kutangaza ujumbe huo.”

10 Katika hotuba hiyo ambayo watu hawawezi kusahau, Ndugu Rutherford alitangaza kwamba gazeti mupya, L’Âge d’Or (leo Amuka!), litachapishwa ili litumiwe kuwaongoza watu kwenye Ufalme, ambao ni tumaini la pekee la wanadamu. Kisha aliuliza ni wangapi kati ya watu waliokuwa hapo kwenye mukusanyiko wangependa kufanya kazi ya kugawanya gazeti hilo. Ripoti moja ambayo ilizungumuzia mukusanyiko huo ilisema hivi: “Watu wote 6000 ambao walihuzuria walisimama mara moja ili kuonyesha kwamba walipenda kufanya kazi hiyo. Hilo lilikuwa jambo la ajabu sana!” * Ni wazi kabisa, Mufalme alikuwa na wahubiri wenye kujitoa kwa kupenda na ambao walikuwa na hamu sana ya kutangaza Ufalme wake!

11, 12. Katika mwaka wa 1920, gazeti Munara wa Mulinzi lilisema kwamba ni wakati gani kazi ambayo Yesu alitabiri ingefanywa?

11 Ujumbe ulichapishwa katika vichapo. Kupitia gazeti Munara wa Mulinzi, maana ya kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme ambayo Yesu alitabiri, ilianza kuwa wazi zaidi na zaidi. Tuchukue mifano ya magazeti fulani ambayo yalichapishwa kuanzia mwanzo wa mwaka wa 1920 mupaka mwaka wa 1930.

12 Ni ujumbe gani ungepaswa kutangazwa ili kutimiza andiko la Mathayo 24:14? Kazi hiyo ingefanywa wakati gani? Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 7, 1920, lilikuwa na habari yenye kusema “Habari Njema ya Ufalme.” Habari hiyo ilifasiria ujumbe ambao unapaswa kutangazwa. Ilisema hivi: “Habari njema ambayo tunatangaza inazungumuzia mwisho wa ulimwengu huu muovu, na kuanzishwa kwa ufalme wa Masiya.” Habari hiyo ilionyesha wazi ni wakati gani ujumbe huo unapaswa kuhubiriwa. Ilisema hivi: “Ujumbe huu unapaswa kutangazwa katika kipindi kilicho kati ya vita kubwa ya ulimwengu [Vita ya Kwanza ya Ulimwengu] na ile ‘ziki kubwa.’” Kwa hiyo habari hiyo ilikazia hivi: “Sasa ndio wakati . . . wa kutangaza duniani pote hii habari njema, katika dini zinazojidai kuwa za Kikristo.”

13. Katika mwaka wa 1921, namna gani habari iliyotolewa katika gazeti Munara wa Mulinzi iliamusha roho ya kujitoa kwa kupenda ya Wakristo watiwa-mafuta?

13 Watu wa Mungu walikazwa kufanya kazi ambayo Yesu alitabiri? Hapana. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 3, 1921, lilikuwa na habari hii: “Tuwe Hodari.” Habari hiyo ilivutia sana Wakristo watiwa-mafuta waliokuwa na roho ya kujitoa kwa kupenda. Kila mumoja aliombwa kujiuliza hivi: “Daraka langu na pendeleo langu kubwa, si lile la kufanya kazi hii ya kuhubiri?” Habari hiyo iliendelea kusema: “Wakati unaona kufanya kazi hiyo [kuwa ni pendeleo], unajisikia kama Yeremia, ambaye neno la Bwana katika moyo wake lilikuwa kama ‘moto unaowaka ambao umefungwa katika mifupa [yake],’ na uliokuwa unamuchochea hivi kwamba hakuweza kujizuia kusema.” (Yer. 20:9) Kitia moyo hicho ambacho kilitolewa kwa uchangamufu kilionyesha kwamba Yehova na Yesu wanatumainia watumishi waaminifu ili kutegemeza Ufalme.

14, 15. Katika mwaka wa 1922, gazeti Munara wa Mulinzi liliwachochea Wakristo watiwa-mafuta kuwafikia watu kwa njia gani?

14 Wakristo wa kweli walipaswa kutumia njia gani ili kuwafikishia watu ujumbe wa Ufalme? Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 8, 1922, lilikuwa na habari fupi lakini yenye kuchochea ambayo ilisema hivi: “Kazi Ni ya Lazima.” Katika habari hiyo, Wakristo watiwa-mafuta walitiwa moyo “kupelekea watu kwa bidii ujumbe ambao ulichapishwa katika vichapo na kuzungumuza nao kwenye milango, na kuwatolea ushahidi kwamba ufalme wa mbinguni unakaribia.”

15 Ni wazi kabisa, kuanzia mwaka wa 1919, Kristo ametumia mutumwa mwaminifu na mwenye busara ili kukazia mara kwa mara kwamba daraka na pendeleo la kila Mukristo hapa duniani, ni kutangaza ujumbe wa Ufalme. Kwa hiyo, namna gani Wanafunzi wa Biblia walionyesha kwamba walifurahia vitia-moyo hivyo vya kutangaza Ufalme?

“Waaminifu Watajitoa kwa Kupenda”

16. Wazee fulani waliochaguliwa kidemokrasi walionyesha hali gani juu ya wazo la kwamba watiwa-mafuta wote wanapaswa kuhubiri?

16 Katika miaka ya 1920 na miaka ya 1930, ndugu fulani walipinga wazo la kwamba watiwa-mafuta wote wanapaswa kuhubiri. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 11, 1927, lilifasiria ni nini ilitokeza hali hiyo. Lilisema hivi: “Leo, katika kanisa [kutaniko] kuna ndugu ambao wana madaraka ya uzee . . . lakini ambao wanakataa kutia ndugu zao moyo kufanya kazi ya kuhubiri, pia wao wenyewe wanakataa kufanya kazi hiyo. . . . Wanazarau wazo la kuwapelekea watu nyumba kwa nyumba ujumbe wa Mungu, wa Mufalme wake na ujumbe wa ufalme.” Habari hiyo ilisema waziwazi hivi: “Wakati umefika ili ndugu walio waaminifu watie alama watu kama hao na kuwaepuka, na kuwaambia kwamba hawatawapatia tena madaraka ya uzee.” *

17, 18. Namna gani ndugu wengi katika makutaniko walikubali muongozo wa mutumwa mwaminifu, na katika zaidi ya miaka 100 iliyopita, namna gani mamilioni wameonyesha kwamba wamekubali muongozo huo?

17 Jambo lenye kufurahisha ni kwamba wengi katika makutaniko walikubali kwa uchangamufu muongozo huo wa mutumwa mwaminifu. Waliona kuwa ni pendeleo kabisa kuhubiri ujumbe wa Ufalme. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 3, 1926, lilisema hivi kuhusu jambo hilo: “Waaminifu watajitoa kwa kupenda, . . . ili kujulisha watu ujumbe huu.” Waaminifu hao walitimiza maneno ya unabii ambayo yanapatikana katika andiko la Zaburi 110:3, na walionyesha kwamba wao ni wahubiri wenye kujitoa kwa kupenda kwa kuunga mukono Masiya-Mufalme.

18 Katika miaka zaidi ya 100 iliyopita, mamilioni wamejitoa kwa kupenda ili kutimiza kazi ya kuhubiri Ufalme. Katika sura fulani ambazo zinafuata, tutazungumuzia namna gani walifanya kazi ya kuhubiri, ni kusema, njia mbalimbali na vyombo ambavyo walitumia. Pia tutaona ni nini imekuwa matokeo ya kazi hiyo. Kwa hiyo, tuzungumuzie kwanza sababu gani mamilioni ya wahubiri walijitoa kwa kupenda ili kufanya kazi ya kuhubiri Ufalme, hata kama wamekuwa wenye kuishi katika ulimwengu wa watu wanaotafuta faida zao wenyewe. Wakati tunaendelea kuchunguza sababu, itakuwa vizuri kila mumoja wetu ajiulize, ‘Sababu gani ninahubiria wengine habari njema?’

‘Endelea Kutafuta Kwanza Ufalme’

19. Sababu gani tunafuata shauri la Yesu linalotuomba ‘tuendelee kutafuta kwanza Ufalme’?

19 Yesu aliwashauri wafuasi wake ‘waendelee kutafuta kwanza Ufalme.’ (Mt. 6:33) Sababu gani sisi pia tunafuata shauri hilo? Tunafuata shauri hilo, hasa kwa sababu tunatambua kwamba Ufalme ni jambo la maana sana katika kusudi la Mungu. Katika sura iliyotangulia, tulijifunza kwamba roho takatifu imefunua hatua kwa hatua mafundisho mbalimbali ya kweli yenye kufurahisha juu ya Ufalme. Wakati kweli juu ya Ufalme, kweli ambayo haiwezi kulinganishwa na kitu, inagusa moyo wetu, tunachochewa kabisa kutafuta kwanza Ufalme huo.

Kama vile mutu aliyefurahi sana kwa sababu alipata hazina iliyofichwa, Wakristo wanafurahi sana kwa sababu wamepata kweli ya Ufalme (Soma fungu la 20)

20. Katika mufano wa hazina iliyofichwa, namna gani Yesu alionyesha kwamba wafuasi wake watakubali shauri la kuendelea kutafuta kwanza Ufalme?

20 Yesu alijua kwamba wafuasi wake watafuata shauri la kuendelea kutafuta kwanza Ufalme. Kwa hiyo, acha tuchunguze mufano wake wa hazina ambayo ilifichwa. (Soma Mathayo 13:44.) Katika mufano huo, Yesu alionyesha kwamba mulimaji fulani alikuwa analima shamba lake. Lakini siku fulani alifikia kupata hazina iliyofichwa na mara moja akaona kwamba ilikuwa kitu cha bei sana. Mulimaji huyo alifanya nini? Biblia inasema kwamba kwa sababu ya furaha ambayo alikuwa nayo, alienda na kuuzisha vitu ambavyo alikuwa navyo na akauza shamba hilo. Mufano huo unatufundisha nini? Wakati tunapata kweli ya Ufalme na tunatambua kwamba ni kitu cha bei sana, kwa furaha tutajiima mambo fulani ikiwa ni lazima, ili tuweze kuendelea kuweka faida za Ufalme pa nafasi inayostahili, ni kusema, kuziweka pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu. *

21, 22. Namna gani wahubiri waaminifu wanaonyesha kwamba wanatafuta kwanza Ufalme? Toa mufano.

21 Wahubiri waaminifu na wenye kuunga mukono Ufalme wanaonyesha kwa maneno na kwa matendo kwamba wanatafuta kwanza Ufalme. Wanatumia maisha yao, uwezo wao mbalimbali, na mali zao ili kuhubiri Ufalme. Wengi wamejiima mambo ya lazima sana ili kufanya utumishi wa wakati wote. Wahubiri hao wote wenye kujitoa kwa kupenda wamejionea wenyewe kwamba Yehova anabariki wale wanaotia Ufalme pa nafasi ya kwanza. Tuchunguze mufano wa ndugu Avery Bristow na bibi yake.

22 Ndugu huyo na bibi yake Lovenia, walikuwa wakolportere (leo mapainia) kusini mwa États-Unis, mwishoni mwa miaka ya 1920. Kisha miaka mingi, dada Lovenia alikumbuka: “Bwana yangu na mimi tumekuwa na maisha yenye furaha kwa miaka mingi katika kazi ya upainia kuanzia wakati huo. Mara nyingi hatukujua tutapata feza wapi ili kuuza petroli na chakula. Lakini, kwa kawaida, Yehova alitutolea vitu hivyo kwa njia mbalimbali, na tuliendelea na kazi yetu ya upainia. Kwa kweli hatukukosa mambo ya lazima.” Dada Lovenia alikumbuka jambo lililotokea siku fulani wakati walikuwa katika muji wa Pensacola, Florida, na hawakuwa na feza ao chakula. Kisha mahubiri walirudi kwenye motokari yao yenye kukokotwa na farasi ambayo walitumia kama nyumba. Wakati walifika walikuta vikapo viwili vikubwa vya chakula na barua yenye kusema hivi, “Kutaniko la Pensacola linawapenda.” Wakati dada Lovenia alikumbuka miaka mingi waliyopitisha katika utumishi wa wakati wote, alisema hivi: “Yehova hakutusahau hata siku moja. Hakukosa hata siku moja kutimiza tumaini ambalo tulikuwa nalo kwake.”

23. Unajisikia namna gani juu ya kweli ya Ufalme ambayo umepata, na unaazimia kufanya nini?

23 Ni kweli kwamba sisi wote hatuwezi kuwa katika utumishi wa wakati wote. Hali zetu zinatofautiana. Hata hivyo, sisi wote tunaweza kufurahia pendeleo la kutangaza habari njema kwa nafsi yote. (Kol. 3:23) Kwa sababu sisi tunaona kweli ya Ufalme kuwa jambo la maana sana, tuko tayari, ndiyo, tunapenda kabisa, kujiima hata kitu gani ili tuweze kutumika zaidi kadiri ambayo tunaweza. Wewe pia unaazimia hivyo?

24. Taja jambo moja kati ya mambo makubwa ambayo Ufalme unatimiza katika siku za mwisho?

24 Katika miaka 100 ambayo imepita, bila shaka Mufalme ameendelea kutimiza maneno yake ya unabii ambayo yaliandikwa katika andiko la Mathayo 24:14. Na amefanya hivyo bila kumukaza mutu yeyote. Watu wa ulimwengu wa leo ni wenye kujipenda wenyewe. Hata hivyo, wafuasi wa Yesu wametoka katika ulimwengu huo, wamejitoa kwa kupenda ili kufanya kazi ya kuhubiri. Kazi yao ya kuhubiri habari njema duniani pote ni sehemu ya alama ya kuwapo kwa Yesu katika mamlaka ya Ufalme. Pia ni moja ya mambo makubwa ambayo Ufalme unatimiza katika siku za mwisho.

^ fu. 5 Katika Biblia, umande unatumiwa ili kuonyesha uwingi wa kitu fulani.—Mwa. 27:28; Mika 5:7.

^ fu. 10 Kijitabu Ni Nani Waliopewa Kazi Hii (katika Kiingereza) kilifasiria hivi: Gazeti L’Âge d’Or litatumiwa katika kampanye ya nyumba kwa nyumba ili kutolea watu ujumbe wa Ufalme. . . . Kisha kutolea watu ujumbe, gazeti L’Âge d’Or litaachwa kwenye kila nyumba, iwe mutu amefanya uandikisho ao hapana.” Kisha miaka fulani, ndugu walitiwa moyo kutolea watu uandikisho wa gazeti L’Âge d’Or na gazeti Munara wa Mulinzi. Kuanzia tarehe 1 Mwezi wa 2, 1940, watu wa Yehova walitiwa moyo kutolea watu magazeti na kutoa ripoti yenye kuonyesha ni magazeti ngapi walitolea watu.

^ fu. 16 Wakati huo, katika kutaniko wazee walikuwa wanachaguliwa kwa njia ya kidemokrasi, ni kusema, kwa njia ya kufanya uchaguzi (vote). Kwa hiyo, kutaniko lingeweza kukataa kuchagua wanaume ambao walipinga kazi ya kuhubiri. Katika Sura ya 12, tutazungumuzia namna kutiwa kwa wazee kulianza kufanywa kwa njia ya kiteokrasi.

^ fu. 20 Yesu alizungumuzia jambo kama hilo katika mufano wake mwingine wa mufanya-biashara mwenye kusafiri ambaye alienda kutafuta lulu ya bei sana. Wakati aliipata, aliuzisha vitu vyake vyote na kuuza lulu hiyo. (Mt. 13:45, 46) Mifano hiyo miwili inatufundisha pia kwamba tunaweza kujifunza kweli juu ya Ufalme kwa njia tofauti. Watu fulani ni kama vile waliokota ile kweli; na wengine ni kama vile waliitafuta. Lakini, hata kama tulipata ile kweli namna gani, tuko tayari kujiima hata kitu gani ili kutia Ufalme pa nafasi ya kwanza..