Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 9

Matokeo ya Kazi ya Kuhubiri: ‘Mashamba Yamekuwa Meupe, Tayari kwa Mavuno”

Matokeo ya Kazi ya Kuhubiri: ‘Mashamba Yamekuwa Meupe, Tayari kwa Mavuno”

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Yehova amefanya mbegu za ile kweli ya Ufalme zikomae

1, 2. (a) Sababu gani wanafunzi wanashangaa sana? (b) Yesu anazungumuzia aina gani ya mavuno?

WANAFUNZI wa Yesu wanashangaa sana. Yesu ametoka kuwaambia hivi: ‘Muinue macho yenu, mutazame mashamba yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.’ Wanaangalia-angalia upande ambao Yesu anaonyesha mukono, lakini wanaona tu mashamba ya rangi ya kijani kibichi: rangi ya shairi (orge) yenye kuchipuka hivi karibuni. Lakini hawaone mashamba meupe kama vile Yesu anasema. Pengine wanajiuliza, ‘ni mavuno gani hayo ambayo anazungumuzia?’ Wanajua kwamba itachukua miezi fulani mbele ya mashamba kuwa tayari kwa mavuno!’—Yoh. 4:35 La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo.

2 Hata hivyo, Yesu hakuwa anazungumuzia mavuno ya kawaida. Anatumia nafasi hiyo ili kufundisha wanafunzi wake mambo mawili ya maana sana kuhusu mavuno ya kiroho, ni kusema, kuvuna watu. Ni mambo gani anapenda kuwafundisha? Ili kujua mambo hayo, acha tuchunguze habari hiyo kwa urefu zaidi.

Wanachochewa Kutenda na Wanapewa Ahadi ya Kufurahi

3. (a) Pengine ni nini ilimuchochea Yesu kusema: ‘Mashamba yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno’? (Ona maelezo mengine.) (b) Yesu alisema nini ili kufasiria maneno yake?

3 Yesu aliwaambia wanafunzi wake maneno hayo kuhusu mavuno mwishoni mwa mwaka wa 30. Ilikuwa pembeni ya muji wa Samaria ambao unaitwa Sikari. Wakati wanafunzi wake walienda katika muji, Yesu alibaki kwenye kisima kimoja cha maji na hapo alihubiria mwanamuke fulani mafundisho ya kweli ya Neno la Mungu. Mwanamuke huyo alielewa mara moja kwamba mafundisho hayo ni ya lazima sana. Wakati wanafunzi wa Yesu walirudi, mwanamuke huyo alienda haraka mupaka Sikari na akawaelezea majirani mambo yenye kupendeza ambayo alikuwa amejifunza. Mambo ambayo aliwaelezea majirani yaliwapendeza sana, na wengi wao walienda haraka kwenye kisima ili kumuona Yesu. Inaonekana kwamba ni wakati huo ndio Yesu kuliko kuangalia mashamba, anaangalia kwa mbali na anaona Wasamaria wengi ambao walikuwa wanakuja. Na kwa hiyo, alisema hivi: ‘Mutazame mashamba, yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.’ * Kisha, ili kufasiria kwamba alikuwa anazungumuzia mavuno ya kiroho, wala si ya kawaida, Yesu alisema tena hivi: ‘Muvunaji anakusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele.’​—Yoh. 4:5-30, 36.

4. (a) Ni mambo gani mawili Yesu alipenda kufundisha kuhusu mavuno? (b) Tutapata majibu ya maulizo gani?

4 Ni mambo gani mawili ya maana ambayo Yesu alipenda kuwafundisha wanafunzi wake kuhusu mavuno ya kiroho? Jambo la kwanza ni hili: kazi inapaswa kufanywa kwa haraka. Wakati aliwaambia wanafunzi wake kwamba ‘mashamba yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno,’ alikuwa anapenda kuwachochea watende. Ili kuwasaidia wanafunzi wake wajue kwamba inafaa kutenda kwa haraka, Yesu aliongeza maneno haya: ‘Tayari muvunaji anapokea mushahara.’ Ndiyo, tayari mavuno yalikuwa yameanza, hakukuwa tena wakati wa kupoteza! Jambo la pili: wafanyakazi ni wenye kufurahi. Yesu alisema kwamba wapandaji na wavunaji watafurahi pamoja. (Yoh. 4:35b, 36) Bila shaka, Yesu alifurahi sana wakati aliona kwamba ‘Wasamaria wengi walimuamini.’ Vilevile, wanafunzi wake wangesikia furaha sana wakati wangetumika kwa moyo wao wote katika mavuno. (Yoh. 4:39-42) Habari ya wafuasi wa kwanza-kwanza wa Yesu ina maana ya pekee kwetu, kwa sababu inaonyesha mambo ambayo yanatendeka leo katika kipindi hiki cha mavuno makubwa zaidi ya kiroho ambayo hayatafanyika tena. Mavuno ambayo yanafanyika katika siku zetu yalianza wakati gani? Wavunaji ni nani? Na kumekuwa matokeo gani?

Mufalme Wetu Anaongoza Kazi ya Mavuno Makubwa Zaidi Ambayo Hayatafanyika Tena

5. Ni nani anayeongoza kazi ya mavuno ambayo yanafanyika duniani pote, na namna gani maono ya mutume Yohana yanaonyesha kwamba kazi hiyo inapaswa kufanywa kwa haraka?

5 Mutume Yohana aliona maono, na katika maono hayo Yehova anafunua kwamba alimupatia Yesu daraka la kuongoza kazi ya kuvuna watu duniani pote. (Soma Ufunuo 14:14-16.) Yesu anaonekana mwenye kuvaa taji kwenye kichwa na anashika mundu (ao mupanga wa kuvuna). Ile ‘taji ya zahabu’ ambayo Yesu anavaa inaonyesha kwamba yeye ni Mufalme mwenye kutawala. Na ‘mundu mukali’ ambao anakamata katika mukono, unaonyesha daraka lake la Muvunaji. Kwa sababu Yehova anasema kupitia malaika kwamba ‘mavuno ya dunia yameivya kabisa,’ hilo linaonyesha kwamba Yehova anakazia sana kwamba kazi inapaswa kufanywa kwa haraka. Kwa kweli, ‘saa ya mavuno imekuja,’ hakuna tena wakati wa kupoteza! Yesu anatii amri ya Mungu ya kutia mundu wake ili kuvuna. Anafanya hivyo na dunia inavunwa, ni kusema, watu wa dunia wanavunwa. Maono hayo yenye kufurahisha yanatukumbusha tena kwamba ‘mashamba yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.’ Je, maono hayo yanatusaidia kujua ni wakati gani mavuno hayo ambayo yanafanyika duniani pote yalianza? Ndiyo!

6. (a) Ni wakati gani “majira ya mavuno” yalianza? (b) Ni wakati gani “mavuno ya dunia” yalianza? Fasiria jibu lako.

6 Kwa sababu katika Ufunuo sura ya 14, Yohana anamuona Yesu ambaye ni Muvunaji, amevaa taji (mustari wa 14), hilo linaonyesha kwamba Yesu alikuwa amekwisha kuwekwa kuwa Mufalme katika mwaka wa 1914. (Dan. 7:13, 14) Wakati fulani, kisha hapo, Yesu anapewa amri ya kuanza mavuno (mustari wa 15). Kufuatana kwa matukio hayo, kunaonekana pia katika mufano wa Yesu wa mavuno ya ngano. Katika mufano huo Yesu alisema hivi: ‘Mavuno ni umalizio wa mufumo wa mambo.’ Kwa hiyo, kipindi cha mavuno na cha umalizio wa mufumo wa mambo vinaanza wakati mumoja, ni kusema, katika mwaka wa 1914. Kisha, “katika majira ya mavuno,” ndipo mavuno ya kweli ya ngano yalianza. (Mt. 13:30, 39) Tukiangalia nyuma katika miaka iliyopita, tunaweza kuona kwamba mavuno yalianza miaka fulani kisha Yesu kuwekwa kuwa Mufalme na kuanza kutawala. Tangu mwaka wa 1914 mupaka miezi ya mwanzo ya mwaka wa 1919, Yesu alianza kufanya kazi ya kusafisha wafuasi wake watiwa-mafuta. (Mal. 3:1-3; 1 Pet. 4:17) Kisha hapo, “mavuno ya dunia” yalianza katika mwaka 1919. Bila kupoteza wakati, Yesu alitumia mutumwa mwaminifu ambaye alitoka tu kuchagua ili kusaidia ndugu zetu waone kwamba kazi ya kuhubiri inapaswa kufanywa kwa haraka. Acha tuchunguze mambo ambayo yalitokea.

7. (a) Ni uchunguzi wa unabii gani uliwasaidia ndugu zetu waone kwamba kazi ya kuhubiri inapashwa kufanywa kwa haraka? (b) Ndugu zetu walitiwa moyo kufanya nini?

7 Katika Mwezi wa 7, 1920, gazeti Munara wa Mulinzi lilisema hivi: “Wakati unachunguza Maandiko, inaonekana wazi kwamba kanisa (kutaniko) limepewa pendeleo kubwa la kutangaza ujumbe wa ufalme.” Kwa mufano, maneno ya unabii wa Isaya yalisaidia ndugu kuelewa kwamba habari ya Ufalme inapaswa kutangazwa ulimwenguni pote. (Isa. 49:6; 52:7; 61:1-3) Hawakujua ni namna gani kazi hiyo itatimizwa, lakini walitumaini kwamba Yehova atawafungulia njia. (Soma Isaya 59:1.) Kwa sababu ndugu walielewa vizuri kwamba kazi ya kuhubiri inapaswa kufanywa kwa haraka, walitiwa moyo kuongeza utendaji wao katika kazi ya kuhubiri. Ndugu walikubali kitia moyo hicho?

8. Katika mwaka wa 1921, ndugu zetu walielewa mambo gani mawili kuhusu kazi ya kuhubiri?

8 Katika Mwezi wa 12, 1921, gazeti Munara wa Mulinzi lilitangaza hivi: “Mwaka wa 1921 ulikuwa mwaka muzuri sana kuliko miaka mingine; hesabu kubwa ya watu wamesikia ujumbe wa ile kweli katika mwaka huo kuliko miaka ambayo ilitangulia.” Gazeti hilo lilisema tena hivi: “Kungali na kazi mingi ya kufanya. . . . Acha tuifanye kwa moyo wa furaha.” Ona namna ndugu walielewa mambo hayo mawili ya maana juu ya kazi ya kuhubiri ambayo Yesu alikazia katika akili ya mitume wake. Alikazia kwamba kazi inapaswa kufanywa kwa haraka na kwamba wafanyakazi ni wenye kufurahi.

9. (a) Katika mwaka wa 1954, gazeti Munara wa Mulinzi lilisema nini kuhusu kazi ya mavuno, na sababu gani? (b) Katika miaka 50 iliyopita, hesabu ya wahubiri duniani pote iliongezeka namna gani? (Soma pia kisanduku “ Ongezeko la Wahubiri Duniani Pote.”)

9 Tangu mwaka wa 1930 mupaka Mwaka wa 1940, kisha ndugu kuelewa kwamba umati mukubwa wa kondoo wengine watakubali ujumbe wa Ufalme, ndugu waliongeza bidii yao katika kazi ya kuhubiri. (Isa. 55:5; Yoh. 10:16; Ufu. 7:9) Walipata Matokeo gani? Hesabu ya wahubiri wa Ufalme iliongezeka kutoka wahubiri 41000 katika mwaka wa 1934 mupaka kufikia wahubiri 500000 katika mwaka wa 1953! Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 12, 1954, lilisema hivi mara moja: “Ni roho ya Yehova na nguvu ya Neno lake ndio imetimiza kazi hii kubwa zaidi ya mavuno duniani pote.” *​—Zek. 4:6.

 

ONGEZEKO LA WAHUBIRI DUNIANI POTE

Inchi

1962

1987

2013

Australia

15927

46170

66023

Brazili

26390

216216

756455

Ufaransa

18452

96954

124029

Italia

6929

149870

247251

Japani

2491

120722

217154

Meksiko

27054

222168

772628

Nijeria

33956

133899

344342

Ufilipino

36829

101735

181236

Amerika

289135

780676

1203642

Zambia

30129

67144

162370

 

KUONGEZEKA KWA MAFUNZO YA BIBLIA

1950

234952

1960

646108

1970

1146378

1980

1371584

1990

3624091

2000

4766631

2010

8058359

Matokeo ya Kazi ya Mavuno Ilitabiriwa Kupitia Mifano Yenye Kugusa Moyo

10, 11. Katika mufano wa mbegu ya haradali, ni mambo gani yanakaziwa kuhusiana na kuota kwa mbegu hiyo?

10 Katika mifano yake kuhusu Ufalme, Yesu alitabiri katika maneno yenye kugusa moyo matokeo ya kazi ya mavuno. Acha tuchunguze mufano wa mbegu ya haradali na mufano wa chachu. Tutazungumuzia sana namna mifano hiyo imetimizwa katika wakati huu wa mwisho.

11 Mufano wa mbegu ya haradali. Mutu fulani alipanda mbegu ya haradali. Ikaota na kuwa muti mukubwa, na ndege walikuja kupata makao katika muti huo. (Soma Mathayo 13:31, 32.) Ni mambo gani yanakaziwa katika mufano huo kuhusiana na kuota kwa mbegu hiyo? (1) Namna muti unakuwa mukubwa ni jambo lenye kushangaza. ‘Mbegu iliyo ndogo zaidi kuliko mbegu zote’ inakuwa muti wenye “matawi makubwa.” (Mk. 4:31, 32) (2) Muti kuwa mukubwa ni jambo hakika. ‘Baada ya [mbegu] kupandwa, inamea [inaota].’ Ona kwamba Yesu hasemi, inaweza kuota. Lakini, anasema wazi kwamba inaota. Hakuna jambo litazuia mbegu hiyo kuota na kuwa muti mukubwa. (3) Muti huo ambao unakomaa na kuwa mukubwa unavutia viumbe fulani na vinakuja kutafuta makao katika muti. “Ndege wa mbinguni wamekuja” na ‘wanapata makao chini ya kivuli chake.’ Namna gani mambo hayo matatu yanatimizwa katika siku zetu kuhusiana na mavuno ya kiroho?

12. Namna gani mufano wa mbegu ya haradali unatimia katika mavuno ya wakati wetu? (Ona pia muchoro “ Kuongezeka kwa Mafunzo ya Biblia.”)

12 (1) Muti unakuwa mukubwa: Mufano huo wa mbegu ya haradali unaonyesha namna ujumbe wa Ufalme ungeenea na namna Kutaniko la Kikristo lingeongezeka. Kuanzia mwaka wa 1919, wafanyakazi wenye bidii wamekusanywa katika kutaniko la Kikristo ambalo lilianza tena kufanya kazi. Wakati huo, hesabu ya wafanyakazi ilikuwa ndogo, lakini iliongezeka kwa haraka. Kwa kweli, kuota kwa mbegu hiyo mwanzo-mwanzo wa miaka ya 1900 mupaka leo, limekuwa jambo la ajabu sana. (Isa. 60:22) (2) Uhakika: Hakuna kitu kinaweza kuzuia kutaniko la Kikristo kuendelea kuongezeka. Hata ikiwa maadui wa Mungu wametilia mbegu hiyo ndogo vipingamizi ao magumu yaliyo kama majiwe, inaendelea kuota na kukomaa. (Isa. 54:17) (3) Makao: “Ndege wa mbinguni” ambao wanapata makao katika muti huo, wanafananisha mamilioni ya watu wengi wenye mioyo mizuri ambao wamekubali ujumbe wa Ufalme katika inchi 240 hivi. Watu hao wamekubali pia kujiunga na kutaniko la Kikristo. (Eze. 17:23) Katika muti huo wanapata chakula cha kiroho, kitulizo na ulinzi.​—Isa. 32:1, 2; 54:13.

Mufano wa mbegu ya haradali unaonyesha kwamba wale walio katika kutaniko la Kikristo wanapata makao na ulinzi(Soma fungu la 11 na 12)

13. Ni mambo gani yanatiliwa mukazo katika mufano wa chachu?

13 Mufano wa chachu. Kisha mwanamuke fulani kutia chachu katika sehemu fulani ya unga, chachu ilichachisha fungu hilo lote. (Soma Mathayo 13:33.) Ni mambo gani yanatiliwa mukazo katika mufano huo? Acha tuzungumuzie mambo mawili. (1) Uwezo wa kubadilisha kabisa maisha ya watu. Chachu inasambaa kabisa mupaka inachachisha fungu lote. (2) Uwezo wa kuenea kwa namna ambayo haionekane. Chachu inachachisha “vipimo vikubwa vitatu vya unga,” ni kusema, fungu lote. Namna gani mambo hayo mawili yanafanyika katika siku zetu kulingana na mavuno ya kiroho?

14. Kulingana na mufano wa chachu, ni mambo gani yanafanyika katika mavuno ya wakati wetu?

14 (1) Uwezo wa kubadilisha kabisa maisha ya watu: Chachu inafananisha ujumbe wa Ufalme, na fungu la unga linafananisha wanadamu. Kama vile tu chachu ikisha kuchangwa pamoja na unga inaubadilisha, ni hivyo ujumbe wa Ufalme unabadilisha mioyo ya watu wakisha kukubali ujumbe huo. (Rom. 12:2) (2) Uwezo wa kuenea kwa namna ambayo haionekane: Kuenea kwa chachu kunafananisha kuenea kwa ujumbe wa Ufalme. Chachu inapenya katika unga mupaka inaenea katika fungu lote. Vilevile, ujumbe wa Ufalme umeenea ‘mupaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.’ (Mdo. 1:8) Katika mufano huo, hali hiyohiyo ya kuenea inaonyesha pia kwamba hata katika inchi ambamo kazi yetu inakatazwa, ujumbe wa Ufalme utaenea; hata kama katika inchi hizo kazi yetu ya kuhubiri inafanywa bila watu kuona hilo waziwazi.

15. Namna gani maneno ambayo yanapatikana katika andiko la Isaya 60:5, 22 yametimia? (Soma pia visanduku “ Yehova Amefanya Iwezekane,” ukurasa wa 93, na “ Namna ‘Mudogo’ Amekuwa ‘Taifa Lenye Nguvu’” ukurasa 96-97.)

15 Miaka 800 hivi mbele ya Yesu kutoa mifano hiyo, kupitia nabii Isaya, Yehova alikuwa ametabiri kwa kutumia maneno ambayo hayawezi kusahaulika kuhusu kuenea kwa kazi ya mavuno ya kiroho katika siku zetu, na pia kuhusu furaha ambayo wafanyakazi wa mavuno wangepata. * Yehova anaonyesha kwamba watu wataendelea “kuja kutoka mbali,” na watakuja kwenye tengenezo lake. Yehova mwenyewe anazungumuza na “mwanamuke” fulani, ambaye leo anafananishwa na mabaki ya watiwa-mafuta walio hapa duniani. Anamuambia hivi: ‘Utaona na hakika utangaa, na moyo wako kwa kweli utatetemeka [utapigapiga] na kupanuka [ao kujaa sana na furaha], kwa sababu mali za bahari zitajielekeza kwako; mali za mataifa zitakuja kwako.’ (Isa. 60:1, 4, 5, 9) Maneno hayo ni ya kweli kabisa! Leo, watumishi wa Yehova ambao wamemutumikia siku nyingi, wanangaa kwa furaha wakati wanaona namna hesabu ya wahubiri wa Ufalme katika inchi zao imeongezeka kutoka hesabu ya watu wadogo sana na kuwa maelfu ya watu.

Watumishi Wote wa Yehova Wana Sababu ya Kufurahi

16, 17. Toa sababu moja inayofanya ‘mupandaji na muvunaji wapate kushangilia pamoja.’ (Soma pia kisanduku “ Trakte Mbili Ziligusa Mioyo ya Watu Wawili Katika Amazoni.”)

16 Usisahau kwamba Yesu aliwaambia mitume wake hivi: ‘Muvunaji anakusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili mupandaji na muvunaji wapate kushangilia [ao kufurahi] pamoja.’ (Yoh. 4:36) Ni mambo gani yanatufanya ‘tufurahi pamoja’ katika kazi ya mavuno ambayo yanafanyika duniani? Kuna mambo mengi ambayo yanatufanya tunafurahi pamoja. Acha tuzungumuzie mambo tatu.

17 Jambo la kwanza: tunafurahia kuona namna Yehova anatimiza daraka lake katika kazi hii. Wakati tunahubiri ujumbe wa Ufalme, tunapanda mbegu. (Mt. 13:18, 19) Wakati tunasaidia mutu fulani kuwa mwanafunzi wa Kristo, tunavuna. Na sisi wote tunasikia furaha sana wakati tunaona kwa mushangao namna Yehova anafanya mbegu ya Ufalme ‘iote na kuwa ndefu.’ (Mk. 4:27, 28) Mbegu fulani ambazo tunapanda zinaota kisha wakati fulani na zinavunwa na wengine. Pengine wewe pia umekwisha kujionea jambo hilo kama dada Joane. Dada Joane anaishi Uingereza, na alibatizwa kumekwisha kupita miaka 60. Alisema hivi: “Nimekutana na watu ambao waliniambia kwamba nilipanda mbegu katika mioyo yao wakati niliwahubiria kumekwisha kupita miaka mingi. Sikuwajua Mashahidi wengine ambao walijifunza nao kisha miaka na kuwasaidia kuwa watumishi wa Yehova. Ninafurahi kwamba mbegu ambazo nilipanda ziliota na kukua na kisha zilivunwa.”​—Soma 1 Wakorintho 3:6, 7.

18. Kulingana na andiko la 1 Wakorintho 3:8, tuna sababu gani ya kufurahi?

18 Jambo la pili: Tunabaki wafanyakazi wenye furaha wakati tunafikiria maneno haya ya mutume Paulo: ‘Kila mutu atapokea sawabu [ao malipo] yake mwenyewe kulingana na kazi yake mwenyewe.’ (1 Kor. 3:8) Mutu anapewa malipo kulingana na kazi yake, si kulingana na matokeo ya kazi hiyo. Maneno hayo ni yenye kutia moyo kabisa hasa kwa wale ambao wanahubiri katika maeneo ambayo watu hawakubali kabisa ujumbe! Mungu yeye anaona kwamba kila Shahidi ambaye anafanya kazi ya kupanda mbegu kwa moyo wote ni mwenye “kuzaa matunda mengi,” na kwa hiyo, ana sababu nzuri ya kufurahi.​—Yoh. 15:8; Mt. 13:23.

19. (a) Namna gani unabii wa Yesu ambao unapatikana katika andiko la Mathayo 24:14 unatupatia sababu nzuri ya kuwa na furaha? (b) Tunapaswa kuendelea kukumbuka nini hata kama hatupate matokeo mazuri katika kazi ya kufanya wanafunzi?

19 Jambo la tatu: Tunafurahi kuwa kazi yetu inatimiza unabii. Fikiria jibu la Yesu wakati mitume wake walimuuliza: ‘Ni nini itakuwa ishara [ao alama] ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mufumo wa mambo?’ Aliwajibia kwamba kazi ya kuhubiri duniani pote ingekuwa sehemu moja ya ishara hiyo. Je, Yesu alikuwa anazungumuzia kazi ya kufanya wanafunzi? Hapana. Yeye alisema hivi: ‘Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayoikaliwa ili kuwa ushahidi.’ (Mt. 24:3, 14) Kwa hiyo, wakati tunahubiri ujumbe wa Ufalme, tunapanda mbegu, na hiyo ni sehemu ya alama ya siku za mwisho. Basi, wakati tunahubiri habari njema ya Ufalme, tukumbuke kwamba hata ikiwa hatupate nafasi ya kufanya wanafunzi, tumepata nafasi ya kutoa “ushahidi.” * Ndiyo, hata ikiwa watu wanakubali ao wanakataa, tunatimiza unabii wa Yesu na ni pendeleo kabisa kuwa “wafanyakazi pamoja na Mungu.” (1 Kor. 3:9, La Sainte Bible en swahili de la RD. Congo) Hiyo ni sababu nzuri kabisa ya kufurahi!

‘Tangu Kuchomoza kwa Jua Mupaka Kutua kwake’

20, 21. (a) Maneno yaliyo katika unabii wa Malaki 1:11 yanatimia namna gani? (b) Umeazimia kufanya nini kuhusiana na kazi ya mavuno, na sababu gani?

20 Yesu alionyesha mitume wake kwamba kazi ya mavuno ilipaswa kufanywa kwa haraka. Tangu mwaka wa 1919, Yesu amesaidia wanafunzi wake wa siku zetu kuelewa jambo hilo pia. Ili kuonyesha kwamba wameelewa jambo hilo, watu wa Mungu wameongeza bidii yao katika kazi ya kuhubiri. Kwa kweli, imeonekana wazi kwamba hakuna kitu kinaweza kuzuia kazi ya mavuno. Kama vile nabii Malaki alitabiri, kazi ya kuhubiri inaendelea kufanywa leo ‘tangu kuchomoza kwa jua mupaka kutua kwake.’ (Mal. 1:11) Ndiyo, tangu kuamuka kwa jua mupaka kulala kwa jua, ni kusema, tangu mashariki mupaka mangaribi, kila mahali ambako wapandaji na wavunaji wanapatikana duniani, wanatumika pamoja na wanafurahi pamoja. Na tangu kuamuka kwa jua mupaka kulala kwa jua, ni kusema, tangu asubuhi mupaka mangaribi, kila siku, tunachunga katika akili kwamba kazi inapaswa kufanywa kwa haraka.

21 Wakati tunaangalia nyuma zaidi ya miaka 100 hivi iliyopita, na tunaona namna kikundi kidogo cha watumishi wa Mungu kimefikia kuwa “taifa lenye nguvu.” Kwa kweli, mioyo yetu ‘inatetemeka [ao inapigapiga] na kupanuka [ao kujaa]” na furaha. (Isa. 60:5, 22)Acha furaha hiyo na upendo wetu kwa Yehova, “Bwana wa mavuno,” imuchochee kila mumoja wetu aendelee kutimiza daraka lake la kufanya kazi kubwa ya mavuno ambayo haitafanyika tena!​—Lu. 10:2.

^ fu. 3 Maneno ya Yesu kuhusu ‘mashamba kuwa meupe’ yangeweza kumaanisha kanzu nyeupe ambazo Wasamaria wengi walikuwa wamevaa; Wasamaria ambao Yesu alikuwa ameona wanakaribia.

^ fu. 9 Ili kujua mengi kuhusu miaka hiyo na miaka ambayo ilifuata, tunakutia moyo kusoma ukurasa wa 425-520 wa kitabu Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu. Kurasa hizo zinazungumuzia kazi ya mavuno ambayo ilitimizwa tangu mwaka wa 1919 mupaka mwaka wa 1992.

^ fu. 15 Ili kupata maelezo zaidi kuhusu unabii huo wenye kupendeza, soma kitabu Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote II, ukurasa wa 303-320.

^ fu. 19 Wanafunzi wa Biblia wa kwanza-kwanza walikuwa wamekwisha kuelewa ukweli huo wa maana sana. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 11, 1895, lilisema hivi: “Hata ikiwa ni ngano kidogo tu ndio inaweza kukusanywa, ushahidi mukubwa juu ya kweli utakuwa umetolewa. . . . Kila mutu anaweza kuhubiri ile injili.”