Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 11

Mwenendo Safi Unaonyesha Utakatifu wa Mungu

Mwenendo Safi Unaonyesha Utakatifu wa Mungu

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Namna Mufalme amefundisha raia wake kuheshimu kanuni za Mungu kuhusu mwenendo safi

Wazia unaingia kwenye mulango mukubwa ambao unaongoza kwenye uwanja wa inje wa hekalu kubwa la kiroho la Yehova

1. Nabii Ezekieli aliona mambo gani yenye kuogopesha?

UNGEJISIKIA namna gani ikiwa ungejionea mambo kama yale nabii Ezekieli alijionea kumepita miaka 2500 hivi? Wazia jambo hili: Unakaribia hekalu kubwa lenye kungaa sana, na lenye majengo mbalimbali. Malaika fulani mwenye nguvu iko pale ili kukuonyesha mahali hapo penye kuogopesha! Unapanda kupitia vipandio saba ambavyo vinakuongoza juu kwenye moja ya milango tatu. Milango hiyo inakuogopesha sana. Kila mulango una urefu wa karibu metre 30. Upande huu na upande ule wa njia ya kuingilia kuna mahali walinzi wanasimama. Kwenye nguzo za hekalu hilo kunachorwa mitende (miti iliyo kama mingazi) yenye kupendeza sana.​—Eze. 40:1-4, 10, 14, 16, 22; 41:20.

2. (a) Hekalu ambalo Ezekieli aliona katika maono linafananisha nini? (Soma pia maelezo mengine.) (b) Tunaweza kujifunza nini juu ya mambo ambayo yanaonyeshwa kwenye milango ya hekalu?

2 Hayo ni maono yenye kuonyesha hekalu la kiroho. Nabii Ezekieli alizungumuzia sana hekalu hilo. Kwa hiyo, habari kuhusu hekalu inachukua sura nyingi, ni kusema, kuanzia sura ya 40 mupaka sura ya 48ya kitabu chake cha unabii. Hekalu hilo linafananisha mipango ambayo Yehova alikamata kuhusu ibada safi. Kila jambo lina maana kuhusu ibada yetu katika siku hizi za mwisho. * Milango yake mirefu ao yenye kuinuka sana inamaanisha nini? Inatukumbusha kwamba wale ambao wanakubali mipango ya Yehova kuhusu ibada safi wanapaswa kuishi kulingana na kanuni za Mungu ambazo ni za haki na za hali ya juu. Hata zile nguzo zenye kuwa na umbo ya mitende zina maana ileile, kwa sababu mitende inatumiwa katika Biblia ili kufananisha uadilifu (ao haki), ni kusema jambo lenye kunyooka. (Zab. 92:12) Na tuseme nini juu ya mahali pale ambapo walinzi wanasimama? Ni wazi kwamba wale ambao wanashindwa kutii kanuni za Mungu hawakubaliwe kuingia katika njia ya ibada safi, njia yenye kupendeza sana ambayo inatoa uzima.—Eze. 44:9.

3. Sababu gani wafuasi wa Kristo walipaswa kuendelea kusafishwa?

3 Namna gani maono ya nabii Ezekieli yametimizwa? Kama vile tuliona kwenye Sura ya 2, Yehova alitumia Kristo ili kuwasafisha watu wake kwa namna ya pekee kuanzia mwaka wa 1914 mupaka miezi ya mwanzo ya mwaka wa 1919. Kusafishwa huko kulimalizikia hapo? Bila shaka hapana! Miaka yote 100 ambayo imepita, Kristo ameendelea kutetea kanuni takatifu za Yehova juu ya mwenendo safi. Kwa hiyo, wafuasi wake walihitaji kabisa kuendelea kusafishwa. Sababu gani? Sababu ni kwamba Kristo ameendelea kukusanya wafuasi wake na kuwaondoa katika ulimwengu ambao unajaa matendo machafu, na wakati huohuo Shetani anajaribu kuwarudisha tena katika matope ya matendo machafu ya ulimwengu huu. (Soma 2 Petro 2:20-22.) Acha tuchunguze njia tatu ambazo zimetumiwa ili kusafisha Wakristo wa kweli hatua kwa hatua. Ya kwanza, tutachunguza namna ambayo walisafishwa kuhusiana na mwenendo katika mambo fulani. Ya pili, tutachunguza mipango ya maana ambayo ilichukuliwa ili kutaniko liendelee kuwa safi. Na ya tatu, tutachunguza mupango wa familia.

Kusafishwa Kuhusiana na Mwenendo

4, 5. Ni njia gani Shetani ametumia tangu zamani, na amepata matokeo gani?

4 Kila mara watu wa Yehova wamehangaikia sana kuwa na mwenendo safi na tabia nzuri. Kwa hiyo, kila wakati wanapendezwa na mafundisho ambayo yako wazi juu ya mwenendo. Acha tuchunguze mifano fulani.

5 Matendo ya Uasherati. Yehova alipanga kwamba ngono (kitendo cha ndoa) kati ya mwanamuke na mwanaume ambao walifunga ndoa iwe safi na yenye kufurahisha. Shetani anafurahia kugeuza zawadi nzuri ambayo Mungu ametupatia, kuwa jambo fulani chafu na anaweza kutumia jambo hilo kujaribu watu wa Yehova ili wapoteze urafiki wao pamoja na Mungu. Zamani katika siku za Balaamu, Shetani alitumia njia hiyo ambayo iliuwisha watu wengi, na anatumia sana njia hiyo katika siku hizi za mwisho.—Hes. 25:1-3, 9; Ufu. 2:14.

6. Ni naziri gani ambayo ilitolewa katika gazeti Munara wa Mulinzi, ilitumiwa namna gani, na sababu gani iliachwa kutumiwa? (Soma maelezo mengine.)

6 Ili kumuzuia Shetani katika bidii yake, gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 7, 1908, lilikuwa na naziri ambayo ilikuwa na maneno haya: “Kila wakati na kila mahali, nitajiendesha kwa heshima mbele ya mwanaume ao mwanamuke asiye bibi yangu ao bwana yangu.” * Hata ikiwa naziri hiyo haikulazimishwa, ndugu wengi walifanya naziri hiyo na wakatuma majina yao yachapishwe katika Munara wa Mulinzi. Kisha miaka fulani, ilionekana wazi kwamba naziri hiyo ilianza kuwa jambo la kawaida tu, hata ikiwa ilisaidia ndugu wengi kwa wakati wake; kwa hiyo iliachwa kutumiwa. Lakini, kanuni za mwenendo ambazo ilionyesha zilitetewa ao kuungwa mukono kila siku.

7. Katika mwaka wa 1935, gazeti Munara wa Mulinzi, lilizungumuzia tatizo gani, na ni kanuni gani ilikaziwa tena?

7 Shetani aliendelea kushambulia tena zaidi. Habari fulani katika gazeti la Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 3, 1935, ilizungumuzia wazi tatizo ambalo lilianza kuongezeka kati ya watu wa Mungu. Ndugu wengine walifikiri kwamba kwa sababu wanafanya kazi ya kuhubiri, si lazima washikamane na kanuni za mwenendo katika maisha yao ya pekee. Gazeti Munara wa Mulinzi lilisema waziwazi hivi: “Kila mumoja anapaswa kukumbuka kwamba kufanya tu kazi ya kutoa ushahidi hakutoshe. Mashahidi wa Yehova ni wajumbe wa Yehova, na kwa hiyo, wana daraka la kumutetea inavyofaa na kutetea ufalme wake.” Kisha habari hiyo ilitoa mashauri yaliyo wazi juu ya ndoa na juu ya mambo ya ngono. Mashauri hayo yalisaidia watu wa Mungu ‘kukimbia uasherati [ao matendo ya uasherati].’—1 Kor. 6:18.

8. Namna gani gazeti Munara wa Mulinzi lilikazia kwa kurudilia maana kamili ya neno la Kigiriki ambalo linatafsiriwa na matendo ya uasherati?

8 Katika miaka ya hivi karibuni, gazeti Munara wa Mulinzi lilikazia kwa kurudilia maana kamili ya neno ambalo lilitumiwa katika Maandiko ya Kigiriki kuhusu uasherati [matendo ya uasherati], ni kusema, pornéia. Neno hilo halimaanishe tu tendo la mwanaume kulala na mwanamuke ao mwanamuke kulala na mwanaume. Lakini neno pornéia linamaanisha matendo mbalimbali ya uasherati, kama vile matendo yote machafu ya uasherati ambayo yanafanywa katika nyumba za uasherati. Wafuasi wa Kristo wamelindwa ili wasipatwe na matokeo mabaya ambayo yanawapata watu wengi leo duniani, kwa sababu ya mwenendo mupotovu wa uasherati.—Soma Waefeso 4:17-19.

9, 10. (a) Katika mwaka wa 1935, gazeti Munara wa Mulinzi lilizungumuzia habari gani kuhusu mwenendo? (b) Biblia inasema nini kuhusu kutumia pombe inavyofaa?

9 Matumizi mabaya ya pombe. Habari ambayo ilikuwa katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 3, 1935, ilitokeza jambo lingine ambalo linazungumuzia mwenendo: “Imeonekana kwamba ndugu fulani wanaenda katika mahubiri na wanatimiza madaraka katika kutaniko wakati wamekwisha [kunywa pombe]. Ni wakati gani matumizi ya pombe yanakubaliwa na Maandiko? Ni vizuri mutu kutumia pombe wakati anafanya kazi katika tengenezo la Bwana?”

10 Habari hiyo ilizungumuzia mawazo mazuri ambayo yanapatikana katika Neno la Mungu juu ya pombe. Biblia haikataze kunywa divai ao pombe kwa kiasi, lakini inakataza kabisa ulevi. (Zab. 104:14, 15; 1 Kor. 6:9, 10) Kwa muda murefu watu wa Mungu wamekumbushwa matokeo mabaya ya kuenda katika kazi takatifu wakati mutu amekwisha kunywa pombe. Habari ya wana wa Haruni ambao Mungu aliua kwa sababu walitoa juu ya mazabahu moto ulio kinyume na sheria, inaonyesha jambo hilo. Kisha jambo hilo kutendeka, Mungu alitoa amri ambayo ilikataza makuhani wote kutumia pombe wakati wanatimiza kazi yao takatifu. Amri hiyo ilionyesha jambo ambalo pengine liliongoza wana wa Haruni kufanya jambo hilo ambalo halistahili kabisa. (Law. 10:1, 2, 8-11) Leo, kwa kutumia kanuni ambayo inaonyeshwa na amri hiyo, wafuasi wa Kristo wanakuwa waangalifu na wanaepuka kutumia pombe wakati wanafanya kazi takatifu.

11. Watu wa Mungu wamepata baraka gani kwa kuelewa mambo mengi kuhusu pombe?

11 Katika miaka ya hivi karibuni, wafuasi wa Kristo wamebarikiwa zaidi kwa sababu wameelewa mambo mengi kuhusu pombe. Wameelewa matokeo mabaya ya mambo kama vile, tabia ya kuwa mutumwa wa pombe ao kufanya pombe iwe mazoea ya mutu. Kupitia chakula hicho cha kiroho chenye kutolewa kwa wakati, wengi wamesaidiwa kushinda kabisa tatizo hilo, na wameanza kuendesha maisha yao vizuri. Wengi zaidi wamesaidiwa kuepuka kabisa matatizo hayo. Hawaruhusu tena pombe iwapotezee heshima, iwaharibishie familia yao, na zaidi ya yote, hawaruhusu iwapotezee pendeleo la kumuabudu Yehova kupitia ibada yake safi.

“Hatuwezi kuwazia Bwana wetu akinuka moshi wa tumbaku ao kutia katika kinywa chake jambo lolote ambalo linaweza kumuchafua.”—C. T. Russell

12. Wafuasi wa Kristo walikuwa na mawazo gani kuhusu tumbaku mbele hata ya siku za mwisho kuanza?

12 Matumizi ya tumbaku. Hata mbele ya siku za mwisho kuanza, wafuasi wa Kristo walianza kuonyesha kwamba kutumia tumbaku ni vibaya. Kumekwisha kupita miaka fulani, ndugu mwenye kuzeeka, anayeitwa Charles Capen, alikumbuka wakati alikutana kwa mara ya kwanza na Ndugu Charles Taze Russell, ilikuwa mwisho-mwisho wa miaka ya 1890. Wakati huo ndugu Capen alikuwa na miaka 13. Alikuwa pamoja na mukubwa yake na pia wadogo wake wawili kwenye vipandio vya kuingilia kwenye la Maison de la Bible ya Allegheny, Pennsylvania. Wakati ndugu Russell alipita karibu yao, aliwauliza: “Ninyi vijana munavuta tumbaku? Ninasikia harufu ya tumbaku.” Lakini walimuhakikishia kwamba hawavuti tumbaku. Bila shaka, walijua vizuri kabisa mawazo yake juu ya tumbaku. Katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 8, 1895, Ndugu Russell alitoa maelezo juu ya andiko la 2 Wakorintho 7:1. Alisema: “Siwezi kuelewa namna gani matumizi ya tumbaku katika njia yoyote inaweza kuwa kwa utukufu wa Mungu, ao kwa faida ya Mukristo. . . . Hatuwezi kuwazia Bwana wetu akinuka moshi wa tumbaku ao kutia katika kinywa chake jambo lolote ambalo linaweza kumuchafua.”

13. Ni mafasirio gani yalitolewa kuhusu mwenendo katika mwaka wa 1973?

13 Katika mwaka wa 1935, gazeti Munara wa Mulinzi liliita tumbaku kuwa “majani machafu” na likaonyesha kwamba mutu yeyote anayechagua kutafuna tumbaku ao kuivuta hawezi kuwa tena Mwanabeteli ao kuwa mujumbe wa tengenezo la Mungu katika kazi ya upainia ao kuwa katika utumishi wa kusafiri. Katika mwaka wa 1973 mafasirio zaidi juu ya kuvuta tumbaku yalitolewa. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 6, lilifasiria kwamba hakuna Shahidi wa Yehova anayeweza kuwa na hali nzuri katika kutaniko ikiwa anaendelea na tabia hiyo mbaya yenye kuua, yenye kuchafua, na isiyo ya upendo. Wale ambao walikataa kuachana na tabia ya kutumia tumbaku walitengwa na kutaniko. * Kristo alikuwa amechukua hatua nyingine ya maana ili kusafisha wafuasi wake.

14. Ni kanuni gani kuhusu damu Mungu ametoa, na namna gani zoea la kutia watu damu limeenea mahali pote?

14 Matumizi mabaya ya damu. Wakati wa zamani, Mungu alimuambia Noa kwamba ni zambi kula damu. Alirudilia mawazo hayo katika Sheria ambayo alipatia Waisraeli, na vilevile aliomba kutaniko la Kikristo ‘kujiepusha na damu.’ (Mdo. 15:20, 29; Mwa. 9:4; Law. 7:26) Kwa hiyo, si jambo la kushangaza ikiwa Shetani anatumia njia fulani katika siku zetu ili kufanya wengi wakose kutii sheria hiyo. Katika miaka ya 1800, waganga walikuwa wanajaribu-jaribu ufundi wa kutia watu damu. Na wakati walivumbua aina mbalimbali ya damu, ndipo zoea la kutia watu damu likazidi kuenea mahali pote. Katika mwaka wa 1937, waganga walianza kukamata damu na kuichunga ili kuitumia kisha. Vita ya Pili ya Ulimwengu ndio ilifanya ufundi wa kutia watu damu uendelee sana. Kwa haraka, zoea la kutia watu damu likaenea mara moja katika dunia yote.

15, 16. (a) Mashahidi wa Yehova wanachukua musimamo gani kuhusu kutiwa damu? (b) Wafuasi wa Kristo wamepata musaada gani kuhusu kutotiwa damu, kutunzwa bila kutumia damu, na wamepata matokeo gani?

15 Mwanzoni tu mwa mwaka wa 1944, gazeti Munara wa Mulinzi lilionyesha kwamba kutiwa damu ni njia ingine kabisa ya kula damu. Mwaka ambao ulifuata, Maandiko ambayo yanazungumuzia juu ya damu yalikaziwa na kufasiriwa waziwazi. Kufikia mwaka wa 1951, karatasi yenye kuwa na maulizo na majibu ilitolewa ili kusaidia watu wa Mungu wajue namna ya kuzungumuza na waganga, na pia wafanyakazi katika hospitali. Kuhusu damu, duniani pote wafuasi waaminifu wa Kristo walichukua musimamo bila woga, hata kama mara nyingi walizarauliwa, kuteswa, na kupambana na upinzani mukali. Lakini, Kristo aliendelea kusaidia tengenezo lisonge mbele na kulitolea musaada ambao unahitajiwa. Kwa hiyo, broshua na habari zenye kuwa na maelezo mengi ambayo yalitafutwa vizuri yalichapishwa.

16 Katika mwaka wa 1979, wazee fulani walianza kutembelea hospitali mbalimbali ili kuwasaidia waganga waelewe vizuri musimamo wetu, yale Maandiko yanasema juu ya damu, na kuwaonyesha njia zingine ambazo zinaweza kutumiwa mahali pa damu. Katika mwaka wa 1980, wazee katika miji 39 ya Amerika (États-Unis), walipata mazoezi ya pekee kuhusu kazi hiyo. Kisha, Baraza Lenye Kuongoza lilikubali kuwe na Halmashauri za Uhusiano na Hospitali duniani pote. Je, kufanya hivyo kumesaidia? Leo, maelfu ya waganga, ni kusema, waganga wa kupasua, na wa anesthésistes, wanakubali mawazo ya Mashahidi ambao ni wagonjwa, na wanaheshimu uamuzi wao wa kutunzwa bila kutiwa damu. Hospitali ambazo zinakubali kutunza bila kutia damu zinaongezeka, na hata waganga wengine wanakubali kwamba hayo ndio matunzo mazuri zaidi kuliko matunzo mengine. Hauone kwamba ni jambo lenye kufurahisha sana wakati unafikiria namna Yesu amechunga wafuasi wake ili wasichafuliwe na njia hiyo ya Shetani?​—Soma Waefeso 5:25-27.

Hospitali ambazo zinakubali kutunza bila kutia watu damu zinaendelea kuongezeka, na hata waganga wengine wanakubali kwamba hayo ndio matunzo mazuri zaidi kuliko matunzo mengine

17. Namna gani tunaonyesha kama tunafurahia sana njia ambayo Kristo anatumia ili kusafisha wafuasi wake?

17 Kwa hiyo, ni vizuri tujiulize hivi: ‘Tunafurahia kabisa namna Kristo ameendelea kusafisha wafuasi wake, kuwazoeza ili washikamane na kanuni za hali ya juu za Yehova kuhusu mwenendo?’ Basi ikiwa ni hivyo, acha tukumbuke kila mara kwamba tamaa ya Shetani ni kututenganisha na Yehova na pia Yesu, na anafikia kusudi hilo kwa kutufanya tusiheshimu kanuni za Mungu juu ya mwenendo. Ilitupinge uvutano mubaya wa Shetani, tengenezo la Yehova limeendelea kututolea maonyo yenye upendo na vikumbusho kuhusu njia chafu za ulimwengu huu. Acha tuwe waangalifu, tukubali, na tutii mashauri kama hayo ambayo yanatusaidia.​—Met. 19:20.

Kulinda Kutaniko ili Lisilaumiwe

18. Maono ya Ezekieli inatukumbusha waziwazi jambo gani wakati watu wanaasi kanuni za Mungu kimakusudi?

18 Njia ya pili ambayo Wakristo walisafishwa kuhusiana na mwenendo, ilihusu pia kuchukua mipango fulani ili kutaniko liendelee kuwa safi. Jambo la kuhuzunisha ni hili: si wote ambao wanakubali kanuni za Yehova juu ya mwenendo, na ambao walijitoa kwake ndio wanashikamana kwa uaminifu na uamuzi wao mupaka mwisho. Moyo wa wengine unabadilika na wanaasi kimakusudi kanuni ambazo walikubali. Inaomba kufanya nini na watu kama hao? Maono ya Ezekieli ya hekalu la kiroho ambayo tulizungumuzia mwanzo wa sura hii, yanaweza kutupatia wazo fulani ili kujua ni nini tunaweza kufanya. Pengine ungali unakumbuka ile milango mirefu. Upande huu na upande ule wa njia ya kuingilia kulikuwa mahali ambapo walinzi walikuwa wanasimama. Walinzi hao walikuwa wanalinda hekalu. Inaonekana walizuia yeyote ambaye “hajatahiriwa moyoni” kuingia katika hekalu hilo. (Eze. 44:9) Jambo hilo, linatukumbusha wazi kwamba ibada safi ni pendeleo ambalo linapewa tu wale ambao wanajikaza kufuata kanuni za Yehova juu ya mwenendo katika maisha yao. Ni hivyo pia kuhusu pendeleo la kuabudu pamoja na Wakristo wenzetu leo; pendeleo hilo halipewe kwa kila mutu.

19, 20. (a) Namna gani Kristo amesaidia hatua kwa hatua wafuasi wake kuelewa vizuri zaidi namna ya kushugulikia zambi nzito? (b) Taja sababu tatu ambazo zinafanya mutenda-zambi atengwe na kutaniko.

19 Huko nyuma katika mwaka wa 1892, gazeti Munara wa Mulinzi lilitoa maelezo kwamba ni “daraka letu kuwatenga na kutaniko (Wakristo) wale ambao wanakana waziwazi ao kwa njia nyingine kwamba Kristo alijitoa mwenyewe kuwa zabihu ya ukombozi [bei inayolingana] kwa wote.” (Soma 2 Yohana 10.) Katika mwaka wa 1904, kitabu La Nouvelle Création kilionyesha kwamba wale ambao wanaendelea na mwenendo mubaya wanavunja kutaniko moyo, na jambo hilo ni hatari kabisa. Hapo zamani, kutaniko nzima ndilo lilikuwa linafanya kile walikuwa wanaita “uchunguzi wa kanisa” ili kuhukumu watu ambao wamefanya zambi nzito. Lakini, hukumu kama hizo hazikufanywa kwa ukawaida. Katika mwaka wa 1944, gazeti Munara wa Mulinzi lilionyesha kwamba ni ndugu tu walio na madaraka katika kutaniko ndio wanapaswa kuhukumu mambo kama hayo. Katika mwaka wa 1952, utaratibu ambao unategemea Biblia juu ya kuhukumu mambo ulitolewa katika gazeti Munara wa Mulinzi. Lilitilia mukazo kwamba sababu kubwa ambayo inafanya watu ambao hawatubu watengwe na kutaniko ni kusudi kutaniko liendelee kuwa safi.

20 Miaka mingi tangu wakati huo, Kristo amesaidia wafuasi wake kuelewa vizuri zaidi namna ya kuhukumu watu ambao wanafanya zambi nzito. Wazee wa makutaniko wanazoezwa vizuri sana ili kuhukumu mambo kupatana na njia ya Yehova, ni kusema, kufuata haki na rehema kama inavyofaa. Leo, tunaelewa wazi sababu tatu hivi ambazo zinaweza kufanya mutenda-zambi ambaye hatubu, atengwe na kutaniko: (1) ili jina la Yehova lisilaumiwe ao kusemwa vibaya, (2) ili kulinda kutaniko lisiambukizwe na matokeo mabaya ya zambi nzito, na (3) ili kumuchochea mutenda-zambi atubu ikiwa inawezekana.

21. Ni katika njia gani mupango wa kutenga mutu na kutaniko umekuwa baraka kwa wafuasi wa Kristo?

21 Unaona namna mupango wa kutenga mutu na kutaniko umekuwa baraka kwa wafuasi wa Kristo leo? Zamani katika Israeli, mara nyingi mwenendo mubaya wa wakosaji ulikuwa unaharibu taifa nzima. Wakati fulani, watu hao walikuwa hata wengi kuliko wale ambao walimupenda Yehova na wale ambao walipenda kufanya mambo mazuri. Kwa hiyo, mara nyingi jina la Yehova lilikuwa linalaumiwa ao kusemwa vibaya na taifa lilikuwa linapoteza baraka za Mungu. (Yer. 7:23-28) Lakini leo, Yehova anafanya kazi pamoja na wanaume na wanawake ambao wanamupenda. Kwa sababu watenda-zambi wenye mioyo migumu wanaondolewa katikati yetu, hawaruhusiwe kuwa silaha ambazo Shetani anatumia ili kuhatarisha tena kutaniko na kulifanya lipoteze usafi wake. Kwa hiyo, uvutano wao unapunguzwa kabisa. Kwa ujumla, tunahakikishiwa kwamba Yehova anaendelea kutubariki. Kumbuka kwamba Yehova aliahidi hivi: “Silaha yoyote itakayofanywa juu yako haitafanikiwa.” (Isa. 54:17) Wazee wana daraka nzito la kuhukumu watenda-zambi. Je, tunawaunga mukono kwa uaminifu?

Kumutukuza Yule Ambaye Familia Zote Zinapata Jina Kwake

22, 23. Sababu gani ni vizuri kushukuru Wakristo wenzetu ambao waliishi mwanzo wa miaka ya 1900, hata hivyo, sababu gani ndugu walihitaji kuwa na usawaziko katika familia?

22 Njia ya tatu ambayo wafuasi wa Kristo wamepata faida ya kuendelea kusafishwa ni kuhusu ndoa na maisha ya familia. Tunaweza kusema kwamba namna yetu ya kufikiria familia imesafishwa kwa muda wa miaka mingi? Ndiyo. Kwa mufano, wakati tunasoma juu ya watumishi wa Mungu mwanzoni mwa miaka ya 1900, tunavutiwa na hata kushangazwa na roho yao ya kujiima. Sisi ni wenye shukrani sana wakati tunaona namna walitanguliza utumishi wao mutakatifu mbele ya kila kitu kingine katika maisha. Hata hivyo, tunaweza kuona kwamba ndugu hao walihitaji kuwa na usawaziko katika jambo hilo. Sababu gani?

23 Ilikuwa jambo la kawaida ndugu kukubali migawo ya utumishi ao kazi ya kusafiri ambayo ilikuwa inawapeleka mbali na kuwatenganisha na familia zao kwa miezi mingi. Wakati fulani, kubaki bila kuoa kulikaziwa sana kupita hata namna Maandiko yanasema. Pia, wakati huo hakukuwa na mashauri mengi kuhusu namna ya kujenga ndoa za Kikristo. Hali kama hizo zimeendelea kwa wafuasi wa Kristo leo? Hapana!

Migao ya kiteokrasi haipaswe kutiwa mbele ya madaraka ya familia

24. Namna gani Kristo alisaidia wafuasi wake waaminifu wawe na maoni yanayofaa kuhusu ndoa na familia?

24 Leo, migawo ya kiteokrasi haipaswe kutiwa mbele ya madaraka ya familia. (Soma 1 Timotheo 5:8.) Zaidi ya hilo, Kristo amefanya iwezekane kwamba wafuasi wake waaminifu hapa duniani wapate musaada wa mashauri mengi juu ya ndoa na familia, mashauri yenye kusawazika kutoka katika Maandiko. (Efe. 3:14, 15) Katika mwaka wa 1978, kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha kilitokea. Kisha miaka 18 hivi, kukatokea kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Pia, gazeti Munara wa Mulinzi limekuwa na habari nyingi ambazo ziliandikwa ili kusaidia watu ambao walifunga ndoa wajue namna ya kutumia kanuni za Maandiko katika ndoa yao.

25-27. Kwa miaka mingi, namna gani mahitaji ya vijana wa miaka mbalimbali yamefikiriwa tena na tena?

25 Tuseme nini kuhusu vijana? Kwa miaka mingi, mahitaji yao yameendelea kufikiriwa pia. Tengenezo la Yehova limeendelea kuwatolea watoto vitu vizuri kulingana na miaka yao. Hapo mwanzoni, mashauri juu ya vijana hayakuwa mengi, lakini kisha yaliongezeka na kumiminika sana. Kwa mufano, tangu mwaka wa 1919 mupaka 1921, gazeti L’Âge d’Or lilikuwa linatolea vijana habari ambayo ilikuwa inasema, “Funzo la Biblia kwa Vijana.” Kisha, katika mwaka wa 1920 kulitokea broshua yenye kichwa ABC de l’Âge d’Or, na katika mwaka wa 1941 kulitokea kitabu Enfants. Katika miaka ya 1970, kulitokea vitabu Kumsikiliza Mwalimu Mkuu, Kupata Faida Zote za Ujana Wako, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Katika mwaka wa 1982, habari mufululizo zenye kichwa “Vijana Huuliza” zilianza kutokea katika gazeti Amuka! Habari hizo zilitokeza kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, kilichotolewa katika mwaka wa 1989.

Kwenye mukusanyiko ambao ulifanywa Ujerumani, ndugu walipokea kwa furaha broshua Ninajifunza Biblia

26 Leo, tuna mabuku mawili ya kitabu Vijana Huuliza yenye kuzungumuzia hali ambazo vijana wanakutana nazo leo, pamoja na mufululizo wa habari ambazo zinaendelea kupatikana kwenye adresi yetu ya Internete jw.org. Pia tuna kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Adresi yetu ya Internete ina mambo mengi kwa ajili ya vijana. Mambo kama vile picha za watu fulani ambao wanatajwa katika Biblia, michezo mbalimbali ya Biblia kwa ajili ya vijana na watoto, video, na hadisi mbalimbali za Biblia, habari za kujifunza Biblia kwa ajili ya watoto wa miaka tatu na ambao wako chini ya miaka tatu. Ni wazi kwamba, tangu Kristo alikumbatia watoto wadogo, wakati alikuwa hapa duniani, mawazo yake juu ya watoto hayajabadilika. (Mk. 10:13-16) Anapenda watoto wetu ao vijana wetu wajisikie kuwa wanapendwa na walishwe vizuri kiroho.

27 Pia Yesu anapenda watoto walindwe ili wasitendewe vibaya. Kadiri ulimwengu huu wenye mwenendo muchafu umezidi kuzama sana katika mambo ya upotovu, tabia kama vile, kuwalala watoto wadogo ao kuwabaka inazidi kuongezeka. Kwa hiyo, habari zenye kufasiria mambo wazi zilichapishwa ili kusaidia wazazi kulinda watoto wao na tabia hiyo mbaya sana. *

28. (a) Inaomba kufanya nini ili kubaki katika ibada safi kulingana na maono ya hekalu ambalo Ezekieli aliona? (b) Umeazimia kufanya nini?

28 Wewe hauone kwamba ni jambo lenye kufurahisha sana kuona namna Kristo ameendelea kusafisha wafuasi wake, kuwazoeza ili waheshimu kanuni za Yehova za hali ya juu kuhusu mwenendo, waishi kulingana na kanuni hizo na wafaidike na kanuni hizo? Kumbuka tena hekalu ambalo nabii Ezekieli aliona katika maono. Usisahau milango yake mirefu. Kwa kweli, hekalu hilo ni hekalu la kiroho. Hata hivyo, je, tunaona hekalu hilo kuwa jambo la kweli kabisa? Kuenda tu kwenye Jumba la Ufalme, kusoma Biblia ao kuhubiri hakutoshe ili kuingia katika hekalu hilo. Hayo ni mambo ambayo hata mutu munafiki anaweza kufanya, lakini hiyo haionyeshe kwamba ameingia katika hekalu la Yehova. Tukifanya mambo hayo, na wakati huohuo tunaishi kulingana na kanuni za hali ya juu za Yehova kuhusu mwenendo, na ikiwa tunafuata ibada safi kwa moyo muzuri, tunaweza kusema kwamba tumeingia katika hekalu hilo. Na kwamba tunatumikia katika nafasi hiyo iliyo takatifu sana kuliko nafasi zingine, ni kusema, mupango wa Yehova Mungu juu ya ibada safi! Acha kila siku tufurahie pendeleo hilo la ajabu. Acha pia tuendelee kufanya yote ambayo tunaweza ili kuonyesha utakatifu wa Yehova kwa kushikamana na kanuni zake za haki!

^ fu. 2 Katika mwaka wa 1932, kitabu Justification katika buku lake la 2 kilionyesha kwanza kwamba unabii mbalimbali wa Biblia kuhusu kurudishwa kwa watu wa Mungu katika inchi yao, umetimizwa katika siku zetu juu ya Israeli la kiroho wala si juu ya Israeli la kimwili. Unabii huo mbalimbali unaonyesha kurudishwa kwa ibada safi. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 3, 1999, lilifasiria kwamba hekalu ambalo Ezekieli aliona katika maono, ni unabii ambao unaonyesha kurudishwa kwa ibada safi na kwa hiyo, utimizo wa unabii huo ni wa kiroho na ni wa lazima sana katika siku za mwisho.

^ fu. 6 Naziri hiyo ilikataza ndugu na dada wasiooana kuwa wao wenyewe katika chumba. Wanaweza kuwa pamoja ikiwa tu mulango umefunguliwa kabisa wazi, ao ikiwa wao ni bibi na bwana ao ni mutu wa familia kabisa. Kwa miaka mingi, naziri hiyo ilikuwa sehemu ya programu ya Ibada ya Asubuhi ya Beteli na ilirudiliwa kila siku.

^ fu. 13 Matumizi mabaya ya tumbaku, inamaanisha, kuivuta, kuitafuna ao kuiliima kwa kusudi hilo.

^ fu. 27 Ona kwa mufano, sura ya 32 ya kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu; na pia habari ya gazeti Amuka! la Mwezi wa 10, 2007, “ ; na pia habari ya gazeti Amuka! la Mwezi wa 10, 2007, “ ; na pia habari ya gazeti Amuka! la Mwezi wa 10, 2007, “Walinde Watoto Wako!