Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA 18

Feza za Kuendesha Kazi za Ufalme Zinatoka Wapi?

Feza za Kuendesha Kazi za Ufalme Zinatoka Wapi?

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Sababu gani na namna gani watu wa Yehova wanatoa feza ili kuunga mukono kazi ya Ufalme?

1, 2. (a) Namna gani Ndugu Russell alimujibu pastere fulani ambaye alipenda kujua ni wapi Wanafunzi wa Biblia wanatoa feza ili kuendesha kazi yao? (b) Tutazungumuzia nini katika sura hii?

SIKU moja kiongozi fulani wa kanisa ambalo linaitwa Église réformée, alienda kumuona Ndugu Charles T. Russell ili kujua namna gani Wanafunzi wa Biblia wanapata feza za kuendesha kazi yao.

Ndugu Russell alimuambia hivi: “Sisi hatuombe-ombe feza.”

Pastere huyo akamuuliza ndugu Russell: “Ninyi munapata feza namna gani?”

Ndugu Rusell akamujibu hivi: “Hata nikikuambia ukweli hautaniamini. Wakati watu wanapendezwa, na wanakuja kwenye mikutano yetu, hawaone kikapo cha kuomba feza kinapitishwa mbele yao. Lakini wao wenyewe wanaona kwamba garama zimefanywa. Katika mioyo yao wanaona kwamba tulilipia jumba ambalo tunatumia kwa ajili ya ibada . . . Na wanajiuliza wanaweza kufanya nini ili kutoa feza kidogo kwa kutegemeza kazi hii.”

Pastere huyo alimuangalia Ndugu Russell bila kuamini yale alimuambia.

Ndugu Russell aliendelea kumuambia hivi: “Ninakuambia ukweli kabisa. Watu wananiuliza ulizo hili, ‘Ninaweza kufanya nini ili kutoa feza kidogo za kutegemeza kazi hii?’ Wakati mutu anabarikiwa na anapata feza ao mali, atapenda kuitumia kwa ajili ya Bwana. Ikiwa mutu hana kitu, sababu gani tumulazimishe kutoa?” *

2 Maneno hayo ya Ndugu Russell yalikuwa ya “kweli kabisa.” Tangu zamani watu wa Mungu wanatoa michango kwa kujipendea ili kutegemeza ibada ya kweli. Katika sura hii, tutazungumuzia mifano fulani ya zamani ambayo inapatikana katika Maandiko na mifano ya wakati wetu. Wakati tunaendelea kuchunguza ni wapi tunatoa feza leo ili kuendesha kazi za Ufalme, itakuwa vizuri kila mumoja wetu ajiulize: ‘Ninaweza kufanya nini ili kuonyesha kwamba ninaunga Ufalme mukono katika jambo hili?’

‘Kila Mutu Mwenye Moyo Wenye Kupenda na Alete Muchango’

3, 4. (a) Sababu gani Yehova anatumainia sana waabudu wake? (b) Waisraeli walifanya nini ili kuonyesha kwamba waliunga mukono kazi ya kujenga hema ya kutaniko?

3 Yehova anatumainia sana waabudu wake wa kweli. Anajua kwamba ikiwa wanapewa nafasi, wataonyesha kwa furaha kwamba wanashikamana naye kwa kutoa bila kulazimishwa. Acha tuchunguze sasa matukio mbili ambayo yalitendeka katika taifa la Israeli.

4 Kisha Yehova kuwatoa Waisraeli katika Misri, aliwaomba wajenge hema, ao tabenakulo kwa ajili ya ibada. Hema hiyo na vyombo mbalimbali ambavyo vilipaswa kutumiwa viliomba feza mingi. Yehova alimuambia Musa awaambie watu juu ya kazi hiyo ili wawe na nafasi ya kutoa musaada wao. Alimuambia awaambie hivi: ‘Kila mutu mwenye moyo wenye nia [moyo wa kupenda] na alete muchango kwa ajili ya Yehova.’ (Kut. 35:5) Watu hao ambao walikuwa wametoka tu katika mateso ya “kila namna ya utumwa,” walikubali kuunga kazi hiyo mukono? (Kut. 1:14) Ndiyo, waliunga kazi hiyo mukono kwa namna ya ajabu. Walitoa zahabu, feza na vitu vingine vya bei, vitu ambavyo inaonekana walipata kutoka kwa mabwana wao wa zamani, Wamisri. (Kut. 12:35, 36) Waisraeli walitoa vitu zaidi kupita vitu ambayo vilihitajiwa na iliomba watu “wazuiliwe wasilete [tena].”​—Kut. 36:4-7.

5. Waisraeli walifanya nini wakati Daudi aliwapatia nafasi ya kutoa michango ili hekalu lijengwe?

5 Miaka 475 hivi kisha tukio hilo, Daudi alichukua “mali yake ya pekee” ili kutoa muchango kwa ajili ya ujenzi wa hekalu, mahali pa kwanza penye kudumu pa ibada ya kweli duniani. Kisha, alipatia ndugu zake Waisraeli nafasi ya kutoa pia. Aliwauliza hivi: ‘Ni nani anayejitolea kuujaza mukono wake leo kwa zawadi kwa ajili ya Yehova?’ Ili kuonyesha kwamba walikubali, Biblia inasema kwamba watu ‘walimutolea Yehova matoleo kwa hiari [kwa kupenda] kwa moyo kamili.’ (1 Nya. 29:3-9) Daudi alitambua ni wapi michango hiyo ilitoka, ndiyo sababu alimuambia Yehova hivi katika sala: ‘Kila kitu kinatoka kwako, na sisi tumekupa kutoka katika mukono wako mwenyewe.’​—1 Nya. 29:14.

6. Sababu gani feza zinahitajiwa ili kuendesha kazi ya Ufalme leo, na kwa hiyo ni maulizo gani ya maana yanaulizwa?

6 Musa hakuwalazimisha watu wa Mungu kutoa, na Daudi pia hakufanya hivyo. Lakini, watu walitoa kwa moyo wa kupenda. Namna gani leo? Tunajua vizuri kwamba kazi ambayo inafanywa na Ufalme wa Mungu inaomba feza. Inaomba feza mingi kuchapa na kugawanya Biblia na vichapo vingine ambavyo vinategemea Biblia, kujenga na kulinda Majumba ya Ufalme na ya mikusanyiko, beteli mbalimbali, na kutolea ndugu zetu misaada wakati wanapatwa na misiba ao magumu mbalimbali. Kwa hiyo, maulizo fulani ya maana yanaulizwa: Feza za kuendesha kazi hizo zinatoka wapi? Wafuasi wa Mufalme wanapaswa kulazimishwa kutoa?

“Halitaomba-omba Wala Kuwalilia-lilia Watu Watoe Feza Ili Kulitegemeza”

7, 8. Sababu gani watu wa Yehova hawaombe-ombe wala kuwalilia-lilia watu watoe feza ili kuendesha kazi yao?

7 Ndugu Russell na wenzake walikataa kuiga njia za kuomba-omba feza ambazo zinatumiwa kwa kawaida na dini ambazo zinajidai kuwa za Kikristo. Gazeti la pili la Munara wa Mulinzi, kwenye kichwa “Unapenda gazeti Munara wa Mulinzi?” Ndugu Russell alisema hivi: “Tunaamini kwamba gazeti Munara wa Mulinzi linategemezwa na YEHOVA, na ikiwa ni hivyo, halitaomba-omba wala kuwalilia-lilia watu watoe feza ili kulitegemeza. Wakati Yeye anayesema: ‘Feza zote ni zangu, na zahabu yote ni yangu,’ atashindwa kutoa feza ambazo zinahitajiwa, tutaelewa kwamba wakati umefika wa kuacha kuchapisha gazeti hilo.” (Hag. 2:7-9) Miaka zaidi ya 130 imepita, gazeti Munara wa Mulinzi linaendelea kuchapishwa zaidi, na tengenezo ambalo linachapisha gazeti hilo linaendelea kusonga mbele na kuwa nguvu zaidi!

8 Watu wa Yehova hawaombe-ombe feza. Hawapitishe vikapo ili kuomba-omba sadaka, ao hawaandikie watu barua za kuomba feza. Hawaombe sadaka wala hawafanye biashara yoyote ili kupata feza. Wanaendelea kufuata yale ambayo gazeti Munara wa Mulinzi lilisema tangu zamani: “Hatuone kuwa ni jambo lenye kufaa kuomba-omba feza kwa ajili ya kazi ya Bwana, kama vile dini zingine zinafanya . . . tumeona kwamba feza ambazo zinaombwa kwa njia nyingi kwa jina la Bwana ni chukizo, na ni jambo ambalo hakubali. Jambo hilo haliwaletee watoaji baraka zake wala kazi ambayo inatimizwa na feza hizo haibarikiwe naye.” *

‘Kila Mutu Afanye Kama Alivyokusudia Katika Moyo Wake’

9, 10. Taja sababu moja ambayo inatusukuma tutoe michango ya kujipendea?

9 Kwa sababu sisi ni raia wa Ufalme, hatulazimishwe kutoa michango. Tofauti na hilo, kwa furaha tunatumia feza zetu na mali zetu zingine ili kutegemeza kazi za Ufalme. Sababu gani tunatoa hivyo kwa kujipendea? Acha tuzungumuzie sababu tatu.

10 Ya kwanza, tunatoa michango kwa kujipendea kwa sababu tunamupenda Yehova na tunapenda kufanya ‘mambo ambayo yanapendeza machoni pake.’ (1 Yoh. 3:22) Bila shaka, Yehova anapendezwa na muabudu wake ambaye anatoa bila kulazimishwa kwa sababu anasukumwa na moyo. Acha tuchunguze maneno ya mutume Paulo kuhusu namna Wakristo wanapaswa kutoa. (Soma 2 Wakorintho 9:7.) Mukristo wa kweli si mutoaji anayesukumwa ao anayesitasita. Lakini, yeye anatoa kwa sababu ‘amekusudia katika moyo wake’ kufanya hivyo. * Inamaanisha kwamba mbele ya kutoa atakuwa amekwisha kufikiria uhitaji na namna anaweza kutimiza uhitaji huo. Mutoaji kama huyo anapendwa sana na Yehova, kwa sababu ‘Mungu anapenda mutoaji muchangamufu.’ Tafsiri ingine ya Biblia inasema hivi: ‘Mungu anapenda mutu ambaye anapenda kutoa.’

Katika inchi ya Mozambique watoto pia wanaonyesha kwamba wanapenda kutoa

11. Ni nini inatuchochea tumutolee Yehova toleo letu nzuri zaidi?

11 Ya pili, tunatoa michango ya vitu vya kimwili, kwa sababu hiyo ndio njia ya kumushukuru Yehova kwa ajili ya baraka nyingi ambazo ametutolea. Acha tuchunguze kanuni ambayo inapatikana katika sheria ya Musa na ambayo inaweza kumusaidia kila mutumishi wa Yehova kujichunguza. (Soma Kumbukumbu la Torati 16:16, 17.) Wakati Waisraeli walikuwa wanahuzuria sikukuu tatu kubwa za mwaka, kila mwanaume Muisraeli alitoa zawadi ‘kulingana na baraka ambazo Yehova’ alikuwa amemupatia. Kwa hiyo, mbele ya kuhuzuria sikukuu fulani, kila mwanaume Muisraeli alikuwa anaangalia na kufikiria katika moyo wake baraka ambazo Yehova alikuwa amemupatia, na kisha alikuwa anaamua ni toleo gani nzuri zaidi angeweza kuleta. Sisi pia, wakati tunafikiria namna Yehova ametubariki katika njia mbalimbali, moyo wetu unasukumwa kumutolea toleo letu nzuri zaidi. Toleo letu la michango ya vitu vyetu vya kimwili, ambalo tunatoa kwa kujipendea linaonyesha kwamba tunafurahia sana baraka ambazo Yehova ametumwangia.​—2 Kor. 8:12-15.

12, 13. Namna gani michango yetu ya kujipendea inaonyesha kwamba tunamupenda Mufalme wetu, na kila mumoja wetu anaombwa kuto angapi?

12 Ya tatu, michango yetu ya kujipendea inaonyesha kwamba tunamupenda Mufalme wetu Yesu Kristo. Namna gani? Kumbuka maneno ambayo Yesu aliwaambia wanafunzi wake ule usiku wa mwisho wa maisha yake duniani. (Soma Yohana 14:23.) Yesu aliwaambia hivi: ‘Mutu akinipenda atashika neno langu.’ Kushika “neno” la Yesu kunamaanisha pia kushika amri yake ya kuhubiri habari njema ya Ufalme katika dunia yote. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Tunashika “neno” hilo kwa kufanya yote ambayo tunaweza, ni kusema, kutumia wakati wetu, nguvu zetu, na vitu vyetu vya kimwili ili kutegemeza kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba tunamupenda Masiya Mufalme wetu.

13 Kwa kweli, kwa sababu sisi ni raia waaminifu wa Ufalme, tunapenda kuonyesha kwa moyo wetu wote kwamba tunaunga Ufalme mukono kwa kutoa michango ya feza. Tunaombwa kutoa feza ngapi? Huo ni uamuzi wa kila mutu. Kila mutu anatoa kulingana na uwezo wake. Ndugu zetu wengi, hawana vitu vingi vya kimwili. (Mt. 19:23, 24; Yak. 2:5) Hata hivyo, ndugu hao wanaweza kutiwa moyo kwa kujua kwamba Yehova na Mwana wake wanapendezwa hata na michango midogo ambayo wao pia wanafanya kwa kujipendea.​—Mk. 12:41-44.

Tunapata Feza Namna Gani?

14. Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova walikuwa wanawaomba watu nini mbele ya kuwatolea vichapo?

14 Kwa miaka mingi, wakati Mashahidi wa Yehova walikuwa wanatolea watu vichapo, walikuwa wanawaomba muchango wa kiasi fulani cha feza. Muchango huo ulikuwa mudogo sana. Kwa hiyo, hata watu ambao walikuwa na feza kidogo sana wangeweza kupata vichapo. Bila shaka, ikiwa mwenye-nyumba hakuwa na feza ili kutoa muchango huo, lakini alionekana kuwa mwenye kupendezwa, wahubiri wa Ufalme walikuwa tayari kumuachia kichapo. Jambo ambalo walifurahia zaidi ilikuwa ni kuachia watu wenye moyo muzuri vichapo ili waweze kuvisoma na kufaidika navyo.

15, 16. (a) Katika mwaka wa 1990, Baraza Lenye Kuongoza lilifanya mabadiliko gani kuhusu namna yetu ya kutolea watu vichapo? (b) Tunatoa namna gani michango yetu ya kujipendea? (Soma pia kisanduku “ Michango Yetu ya Kujipendea Inatumiwa Namna Gani?”)

15 Katika mwaka wa 1990, Baraza Lenye Kuongoza lilianza kubadilisha namna yetu ya kutolea watu vichapo. Kuanzia mwaka huo, katika Amerika (États-Unis), vichapo vilianza kutolewa bila kuomba kiasi fulani cha feza kama muchango. Barua ambayo ilitumwa kwa makutaniko yote katika Amerika ilisema hivi: “Wahubiri na watu wenye kupendezwa watapewa magazeti na vitabu bila kuwaomba ao hata kusemea kiasi fulani cha muchango ambao unapaswa kutolewa. Si lazima mutu atoe kwanza muchango ili apewe kichapo. . . . Mutu yeyote ambaye anapenda kutoa muchango wa kujipendea ili kutegemeza kazi yetu ya kufundisha anaweza kufanya hivyo. Lakini anaweza kupewa vichapo, iwe anatoa muchango ao hapana.” Mupango huo ulisaidia ili kuonyesha kwamba kazi yetu ni ya kujipendea na inahusu mambo ya dini na pia ulisaidia kuonyesha wazi kwamba “sisi si wachuuzi wa neno la Mungu.” (2 Kor. 2:17) Kisha, tawi mbalimbali duniani pote zilianza kutumikisha mupango huo wa kutoa michango kwa kujipendea.

16 Tunatoa namna gani michango hiyo ya kujipendea? Katika kila Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova munapatikana visanduku vya michango ya kujipendea. Mutu anaweza kutia michango ndani ya visanduku hivyo, ao anaweza kutuma muchango wake moja kwa moja kwenye biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova. Kila mwaka habari fulani katika gazeti Munara wa Mulinzi inakumbusha namna mbalimbali ya kutoa muchango kama huo wa kujipendea.

Feza Ambazo Zinatolewa Zinatumiwa Namna Gani?

17-19. Fasiria namna gani feza ambazo tunatoa zinatumiwa kwa ajili ya (a) kazi ya kuhubiri ya duniani pote, (b) ujenzi wa Majumba ya Ufalme duniani pote, na (c) garama za kutaniko.

17 Kwa ajili ya kazi ya duniani pote. Feza hizo zinatumiwa ili kulipia garama ambazo zinafanywa ili kuendesha kazi ya kuhubiri habari njema. Kama vile kuchapisha vichapo na kuvisafirisha katika duniani yote, kujenga na kulinda biro mbalimbali za tawi, na kuendesha masomo mbalimbali ya kiteokrasi. Pia, feza hizo zinatumiwa ili kusaidia wamisionere, waangalizi wenye kusafiri na mapainia wa pekee. Tena michango yetu ya kujipendea inatumiwa ili kusaidia ndugu zetu wakati wanapatwa na misiba ao magumu. *

18 Kwa Ajili ya kazi ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme duniani pote. Feza hizo zinatumiwa ili kusaidia makutaniko kujenga ao kutengeneza upya jumba lao la Ufalme. Wakati michango ingine inatolewa, feza zingine zinapatikana ili kusaidia kazi hiyo. *

19 Kwa Ajili ya garama za Kutaniko. Feza hizo zinatumiwa ili kulipia garama fulani za kutaniko, kutengeneza Jumba la Ufalme. Wazee wanaweza kupendekeza kwamba kiasi fulani cha feza kitumwe kwenye biro ya tawi ili kutegemeza kazi ya kuhubiri ya duniani pote. Ikiwa wazee wanaamua hivyo, wataomba kutaniko lifanye azimio. Ikiwa kutaniko linakubaliana na azimio hilo, feza zinaweza kutumwa. Kila mwezi, ndugu ambaye anaangalia mambo ya feza za kutaniko atatayarisha ripoti ya matumizi ya feza, na ripoti hiyo itasomewa kutaniko.

20. Namna gani unaweza kumuheshimu Yehova na ‘vitu vyako vyenye samani’?

20 Wakati tunafikiria ukubwa wa kazi ambayo inafanyika duniani pote ili kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi, tunachochewa ‘kumuheshimu Yehova kwa vitu [vyetu] vyenye samani.’ (Met. 3:9, 10) Vitu vyetu vyenye samani vinamaanisha, nguvu zetu za kimwili, uwezo ao akili yetu, na uwezo wetu wa kiroho. Bila shaka, tunapenda kutumikisha mambo hayo kwa ukamili ili kutegemeza kazi ya Ufalme. Hata hivyo, kumbuka kwamba vitu vyetu vya samani vinamaanisha pia vitu vyetu vya kimwili. Acha basi tuazimie kutoa kile ambacho tunaweza na wakati tunaweza kufanya hivyo. Michango yetu ya kujipendea inamuletea Yehova utukufu, na inaonyesha kwamba tunaunga mukono Ufalme wa Masiya.

^ fu. 1 Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 7, 1915, ukurasa wa 218-219.

^ fu. 8 Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 8, 1899 (katika Kiigereza), ukurasa wa 201.

^ fu. 10 Mutu fulani mwenye elimu ya Biblia anasema kwamba neno la Kigiriki ambalo linatafsiriwa “kukusudia” “lina maana ya kupanga mbele ya wakati.” Anasema tena: “Kutoa kunamuletea mutu furaha, hata hivyo, mutu anapaswa kupanga mbele ya wakati kitu ambacho atatoa na namna atakitoa.”​—1 Kor. 16:2.

^ fu. 17 Ikiwa unapenda kupata habari zaidi kuhusu kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu ao misiba, soma Sura ya 20.

^ fu. 18 Ikiwa unapenda kupata habari zaidi kuhusu kazi ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme, soma Sura ya 19.