Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 20

Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu

Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Wakristo wanaonyesha upendo wao wakati wa magumu

1, 2. (a) Wakristo wa Yudea walipambana na magumu gani? (b) Ni tendo gani la upendo Wakristo Wayahudi walijionea?

NI MWAKA wa 46 hivi wakati wa mitume. Muji wa Yudea unashambuliwa na njaa kali sana. Kwa sababu hakuna chakula kingi katika muji, chakula kinapanda bei sana. Kwa hiyo, Wakristo Wayahudi hawana uwezo wa kujiuzia chakula. Wana njaa, wanakosewa kabisa chakula. Lakini, hivi karibuni watajionea ulinzi wa mukono wa Yehova. Kwa wakati wao, hakuna wanafunzi wengine wa Kristo ambao walikuwa wamekwisha kujionea ulinzi kama huo. Ni jambo gani litafanyika?

2 Wakristo Wayahudi na wa Mataifa ambao walikuwa wanaishi katika muji wa Antiokia na Siria, walifanya nini wakati walisikia kwamba ndugu zao Wayahudi wa Yerusalemu na Yudea wanateseka? Walikusanya feza na kuwatumia. Pia walichagua kati yao ndugu wawili wenye kutumainiwa, Barnaba na Sauli ili wapeleke musaada huo kwa wazee wa kutaniko la Yerusalemu. (Soma Matendo 11:27-30; 12:25.) Fikiria namna ndugu wa Yudea waliguswa moyo kwa sababu ya tendo hilo la upendo ambalo ndugu zao wa Antiokia waliwaonyesha!

3. (a) Namna gani watu wa Mungu leo, wanaendelea kufuata mufano wa Wakristo wa Antiokia? Toa mufano. (Soma pia kisanduku “ Programu Yetu Kubwa Zaidi ya Kwanza ya Kutolea Ndugu Misaada Katika Siku Zetu.”) (b) Ni maulizo gani tutazungumuzia katika sura hii?

3 Jambo hilo ambalo lilifanyika siku za mitume, ndilo tukio la kwanza kuandikwa ambalo linaonyesha namna Wakristo ambao wanaishi katika sehemu fulani ya dunia wanatumia Wakristo wengine misaada wakati wa magumu. Leo, tunafuata mufano huo wa ndugu zetu wa Antiokia. Wakati tunajulishwa kwamba ndugu zetu katika inchi fulani wamepatwa na magumu ao musiba, tunawatolea musaada. * Ili kuelewa namna misaada ambayo tunajikaza kutoa wakati wa magumu ni sehemu ya utumishi wetu mwengine ambao tunamutolea Mungu, acha tuchunguze maulizo matatu kuhusu kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu. Sababu gani tunaona kazi hiyo kuwa ni utumishi ambao tunamutolea Mungu? Kazi yetu ya kutoa misaada iko na makusudi gani? Inaleta faida gani?

Sababu Gani Kazi Hiyo Ni Utumishi Mutakatifu

4. Mutume Paulo aliwaambia Wakorintho nini juu ya huduma ya Kikristo?

4 Katika barua yake ya pili kwa Wakorintho, mutume Paulo alifasiria kwamba utumishi wa Wakristo uko na sehemu mbili za maana. Hata ikiwa ni Wakristo watiwa-mafuta ndio waliandikiwa barua hiyo, maneno ya mutume Paulo yanawahusu pia “kondoo wengine.” Yoh. 10:16) Sehemu moja ya kazi yetu ni “huduma [utumishi] ya upatanisho,” ( ni kusema, kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha. (2 Kor. 5:18-20; 1 Tim. 2:3-6) Sehemu ingine ni kazi ambayo tunatimiza kwa faida ya ndugu zetu. Mutume Paulo anazungumuzia sehemu hiyo kuwa “huduma [kazi]” ya kutoa misaada. (2 Kor. 8:4) Katika Kigiriki neno “huduma” ambalo linapatikana katika maneno “huduma ya upatanisho” na ‘huduma ya kutoa misaada’, ni di·a·ko·niʹ. Sababu gani matumizi ya neno hilo ni ya maana?

5. Sababu gani ni jambo la maana kwamba mutume Paulo aliita kazi ya kutolea ndugu misaada kuwa ni huduma?

5 Kwa kutumia neno lilelile la Kigiriki kuhusu kazi hizo mbili, mutume Paulo anaonyesha kwamba kazi ya kutolea ndugu misaada inapatana na sehemu zingine za huduma ao kazi ambazo zilikuwa zinatimizwa na kutaniko la Kikristo. Mbele ya kuzungumuzia jambo hilo alikuwa amekwisha kusema hivi: “Kuna huduma za namna mbalimbali, na bado kuna Bwana yuleyule; na kuna utendaji wa namna mbalimbali; . . . Lakini ni roho ileile moja inayofanya utendaji huu wote.” (1 Kor. 12:4-6, 11) Kwa kweli, mutume Paulo alionyesha kwamba kuna upatano kati ya huduma mbalimbali ambao ulitimizwa katika kutaniko na ‘utumishi mutakatifu.’ * (Rom. 12:1, 6-8) Kwa hiyo, haitushangaze ikiwa Paulo aliona kwamba ni jambo la maana kutumia sehemu ya wakati wake “ili kuwahudumia watakatifu”!—Rom. 15:25, 26.

6. (a) Kama vile mutume Paulo alifasiria, sababu gani kazi ya kutolea ndugu misaada ni sehemu ya ibada yetu? (b) Fasiria namna gani kazi yetu ya kutolea ndugu misaada inafanyika leo. (Soma kisanduku “ Wakati Musiba Unatokea!” ukurasa wa 214.)

6 Mutume Paulo aliwasaidia Wakorintho waelewe kwamba kazi ya kutolea ndugu misaada ni sehemu ya ibada yao kwa Yehova na vilevile ni sehemu ya huduma yao kwa Yehova. Fikiria sababu ya mutume Paulo: Ikiwa Wakristo walitoa misaada ni kwa sababu walikuwa wenye ‘kujitiisha kwenye habari njema juu ya Kristo.’ (2 Kor. 9:13) Kwa hiyo, Wakristo wanasaidia ndugu zao kwa sababu wanataka kutumikisha mafundisho ya Kristo katika maisha yao. Mutume Paulo anasema kwamba matendo ya upendo ambayo Wakristo wanaonyesha ndugu zao, ni ‘fazili nyingi zaidi zisizostahiliwa za Mungu.’ (2 Cor. 9:14; 1 Pet. 4:10) Ndiyo sababu, gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 2, 1975, lilizungumuzia kazi ya kusaidia ndugu zetu wakati wa magumu; lilisema waziwazi hivi: “Tunapaswa kuwa na uhakika kwamba Yehova na Mwana wake Yesu Kristo wanaona kazi hiyo kuwa ya maana sana.” Bila shaka, kazi ya kusaidia ndugu wakati wa magumu ao misiba ni sehemu ya maana sana ya utumishi wetu mutakatifu.​—Rom. 12:1, 7; 2 Kor. 8:7; Ebr. 13:16.

Makusudi ya Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu

7, 8. Kusudi letu la kwanza la kutolea ndugu misaada ni nini? Fasiria.

7 Kazi yetu ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu ina makusudi gani? Mutume Paulo alijibia ulizo hilo katika barua yake ya pili kwa Wakorintho. (Soma 2 Wakorintho 9:11-15.) Katika andiko hilo, mutume Paulo anakazia makusudi matatu ambayo yanatuchochea kuunga mukono ‘huduma ya utumishi wa [ao kwa ajili ya] watu wote,’ ni kusema, kazi ya kutoa misaada. Acha tuzungumuzie makusudi hayo.

8 Kusudi la Kwanza: Kazi yetu ya kutoa misaada inamuletea Yehova utukufu. Katika mistari tano ya andiko ambayo tulizungumuzia hapo juu, mutume Paulo anavutia mara nyingi uangalifu wa ndugu zake kwa Yehova Mungu. Paulo anawakumbusha kuhusu “wonyesho wa shukrani kwa Mungu” na kuhusu “maonyesho mengi ya shukrani kwa Mungu.” (Mustari wa 11, na 12) Anaonyesha kwamba kazi hiyo ya kutoa misaada inachochea Wakristo ‘kumutukuza Mungu’ na kusifu ‘fazili nyingi zaidi zisizostahiliwa za Mungu.’ (Mustari wa 13, na 14) Mutume Paulo anamalizia mazungumuzo yake juu ya kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu ao misiba kwa kusema hivi: “Mungu apewe shukrani.”—Mustari wa 15; 1 Pet. 4:11.

9. Kazi ya kutolea ndugu misaada inaweza namna gani kubadilisha mawazo mabaya ya watu? Toa mufano.

9 Kama mutume Paulo, leo watumishi wa Mungu wanaona kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu kuwa nafasi nzuri ya kumuletea Yehova utukufu, na ya kupamba mafundisho yake. (1 Kor. 10:31; Tito 2:10) Kwa kweli, kazi hiyo ya kutolea ndugu misaada, mara nyingi inasaidia sana kuondoa mawazo mabaya ambayo watu fulani walikuwa nayo juu ya Yehova na juu ya Mashahidi wake. Tuchukue mufano huu: Mwanamuke fulani ambaye alikuwa anaishi katika eneo ambalo liliharibiwa na upepo mukali, alikuwa ameandika hivi kwenye mulango wake: “Mashahidi wa Yehova hawakaribishwe hapa.” Kisha siku fulani aliona ndugu upande mwingine wa barabara wanatengeneza nyumba fulani ambayo ilikuwa imeharibiwa. Kwa muda wa siku fulani, aliona namna wafanyakazi hao walikuwa wanatumika kwa urafiki sana, kisha akaamua kuenda kuwauliza wao ni nani. Wakati alijulishwa kwamba wao ni Mashahidi wa Yehova, alishangaa sana na kusema hivi: “Nilikuwa na maoni mabaya juu yenu.” Matokeo yalikuwa nini? Alifuta maandishi ambayo aliandika kwenye mulango wake.

10, 11. (a) Ni mifano gani inaonyesha kwamba tunafikia kusudi letu la pili la kazi yetu ya kutolea ndugu misaada? (b) Ni kichapo gani kinasaidia wafanyakazi ambao wanatolea ndugu misaada? (Soma kisanduku “ Chombo Kingine kwa Ajili ya Wafanyakazi Ambao Wanatolea Ndugu Misaada.”)

10 Kusudi la Pili: Tunagawia ndugu zetu mahitaji yao kwa uwingi. (2 Kor. 9:12a) Tuko tayari kutimiza mahitaji ya ndugu na dada zetu ambao wanapatwa na magumu ili kuwatolea kitulizo. Sababu gani? Kwa sababu ndugu na dada katika kutaniko la Kikristo wanafanyiza ‘mwili mumoja,’ na “kiungo kimoja kikiumia [ao kuteswa], vile viungo vingine vyote vinaumia.” (1 Kor. 12:20, 26) Kwa hiyo, upendo wa kindugu na huruma vinawachochea ndugu na dada wengi leo kubadilisha programu zao bila kusita, kukusanya vyombo vyao vya kazi, na kuenda mahali ambapo kumefanyika musiba ili kutolea ndugu zao musaada. (Yak. 2:15, 16) Kwa mufano, katika mwaka wa 2011 kisha inchi ya Japani kupigwa na upepo mukali unaoitwa tsunami, Beteli ya Amerika ilituma barua kwa Halmashauri za Ujenzi wa Eneo za Amerika, ili kuomba ikiwa ndugu ambao wana ufundi wa kujenga wanaweza kuenda huko Japani kusaidia kujenga upya Majumba ya Ufalme. Matokeo yalikuwa namna gani? Kwa majuma kidogo tu, ndugu na dada karibu 600 wenye kujitolea walijaza fomu ili kuenda kusaidia. Walikubali pia kujilipia ndege wao wenyewe ili kuenda Japani! Beteli ya Amerika ilisema hivi: “Kujitoa kwao kulitutia moyo sana.” Wakati ndugu fulani wa Japani alimuuliza mumoja wa wafanyakazi hao wenye kujipendea sababu gani alikuja Japani kusaidia, alimujibu hivi: “Ndugu zetu katika Japani ni sehemu ya ‘mwili wetu.’ Taabu yao ni taabu yetu, mateso yao ni mateso yetu.” Wakati mwingine, upendo wa kujitoa kwa ajili ya wengine umefanya ndugu hao wenye kujitolea watie maisha yao katika hatari kwa ajili ya kusaidia ndugu zao. *​—1 Yoh. 3:16.

11 Watu ambao si Mashahidi wanaonyesha pia kwamba wanasamini kazi yetu ya kusaidia ndugu zetu wakati wa magumu. Kwa mufano, katika mwaka wa 2013, muji wa Arkansas, Amerika, ulipatwa na musiba. Kisha gazeti fulani liliandika namna Mashahidi wa Yehova wenye kujitolea walikuja haraka ili kusaidia. Liliandika hivi: “Mashahidi wa Yehova wanapanga mambo vizuri kuhusu wafanyakazi wenye kujitolea ili waweze kusaidia ndugu zao ambao walipatwa na musiba. Na jambo hilo linawasaidia wafanye kazi kwa ufundi sana na kwa matokeo mazuri.” Kwa kweli, kama vile mutume Paulo aliandika, tunagawia ndugu mahitaji yao kwa uwingi.

12-14. (a) Sababu gani kufikia kusudi letu la tatu la kutolea ndugu misaada ni jambo la maana sana? (b) Ndugu na dada walisema nini ili kuonyesha kwamba kuendelea na programu ya kiroho ni jambo la maana sana?

12 Kusudi la Tatu: Tunasaidia ndugu ambao walipatwa na magumu kurudilia programu yao ya kiroho. Sababu gani jambo hilo ni la maana? Mutume Paulo anasema kwamba wale ambao wanatolewa musaada watachochewa kumutolea Mungu “maonyesho mengi ya shukrani.” (2 Kor. 9:12b) Unafikiri kuna njia nzuri zaidi ambayo watu wenye kuteseka wanaweza kutumia ili kuonyesha shukrani zao kwa Yehova, isipokuwa kwa kurudilia haraka iwezekanavyo programu yao ya kawaida ya kiroho? (Flp. 1:10) Katika mwaka wa 1945, gazeti Munara wa Mulinzi lilisema hivi: “Mutume Paulo alikubali . . . kukusanywa kwa michango kwa sababu ilikuwa inasaidia . . . ndugu Wakristo kupata misaada fulani ya kimwili na hilo liliwasaidia kufanya kazi ya kutoa ushahidi juu ya Yehova bila magumu na kwa bidii kabisa.” Kusudi letu ni hilohilo pia leo. Wakati ndugu wanarudilia kazi ya kuhubiri, wanatia moyo jirani zao wenye kuteseka, lakini wao pia wanatiwa nguvu.​—Soma 2 Wakorintho 1:3, 4.

13 Acha tuchunguze maelezo fulani ya ndugu na dada ambao walipokea musaada wakati walikuwa katika uhitaji mukubwa. Walianza tena kuhubiri, na wakatiwa nguvu kwa kufanya hivyo. Ndugu mumoja alisema hivi: “Ilikuwa baraka kabisa kwa familia yetu kuanza tena kuhubiri. Mahubiri ilitusaidia sana, kwa kuwa wakati tuliwatia wengine moyo tulisahau magumu yetu kwa muda fulani.” Dada mwengine alisema hivi: “Kukazia sana kazi ya kiroho kulinisaidia nisifikirie sana vitu mbalimbali ambavyo viliharibika. Mahubiri ilinifanya nijisikie kuwa salama.” Dada mwengine alisema hivi: “Kulikuwa na mambo mengi ambayo hatukujua tufanye nini, lakini kazi ya kuhubiri ilitolea familia yangu muongozo. Kuzungumuza na wengine juu ya tumaini letu la ulimwengu mupya kulitia nguvu tumaini letu la kwamba vitu vyote vitakuwa vipya.”

14 Kuhuzuria mikutano ni utendaji ao kazi ingine ya kiroho ambayo ndugu ambao wanapatwa na musiba wanapaswa kurudilia haraka iwezekanavyo. Tuchukue mufano wa dada Kiyoko, ambaye anakaribia miaka 60. Upepo wa tsunami ulimufanya apoteze karibu kila kitu, alibaki tu na mavazi na pia viato ambavyo alikuwa anavaa wakati huo. Hakujua namna angeendelea kuishi. Kisha muzee wa kutaniko akamuambia kwamba wataanza kufanyia mikutano yao ya kawaida katika motokari yake. Dada Kiyoko alisema hivi: “Muzee huyo na bibi yake, dada mwengine na mimi tulikaa katika motokari ao motokaa. Mukutano ulikuwa mwepesi, lakini kama tu muujiza, mawazo ya tsunami yaliondoka katika akili yangu. Nilisikia ninakuwa na amani ya akili. Mukutano huo ulinisaidia kuona nguvu ya kuwa pamoja na Wakristo wengine.” Dada mwengine alizungumuzia mikutano ambayo alihuzuria kisha musiba kutokea. Alisema hivi: “Mikutano hiyo ilinisaidia kuvumilia!”​—Rom. 1:11, 12; 12:12.

Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Inaleta Faida Zenye Kudumu

15, 16. (a) Wakristo wa Korintho na wa mahali pengine wangepata faida gani kwa kuunga mukono kazi ya kutolea ndugu misaada? (b) Namna gani sisi pia leo tunapata faida ya kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu?

15 Wakati mutume Paulo alikuwa anazungumuzia huduma ao kazi ya kutoa misaada, alifasiria pia Wakorintho faida ambazo wao na Wakristo wengine wangepata kwa kufanya kazi hiyo. Aliandika hivi: ‘Kupitia dua kwa ajili yenu wanatamani [Wakristo Wayahudi katika Yerusalemu ambao walipokea misaada] kuwaona ninyi kwa sababu ya fazili nyingi zaidi zisizostahiliwa za Mungu juu yenu.’ (2 Kor. 9:14) Ndio, ukarimu wa Wakorintho uliwasukuma Wakristo Wayahudi kusali kwa ajili ya ndugu zao katika Korintho, na Wakristo wa Mataifa pia, na hilo lingefanya wawe na upendo mwingi kuwaelekea.

16 Ili kuonyesha faida ambazo zinatokana na kazi ya kutolea ndugu misaada leo, gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 12, 1945, lilizungumuzia maneno ya mutume Paulo. Lilisema hivi: “Wakati kikundi fulani cha watu wa Mungu ambao wamejitoa kwake kinatoa michango ili kusaidia kikundi kingine ambacho kina magumu, bila shaka, hilo linatia nguvu umoja wao!” Ndugu ambao wanafanya kazi ya kutoa misaada wamejionea jambo hilo. Muzee fulani wa kutaniko ambaye alisaidia katika kazi ya kutolea ndugu misaada wakati maji yalijaa na kuharibu vitu vyao, alisema hivi: “Kufanya kazi ya kutolea ndugu misaada kulinifanya niwakaribie zaidi kuliko mbele.” Dada mumoja ambaye alishukuru sana wakati alipokea musaada alisema hivi: “Undugu wetu ndio jambo pekee ambalo tuko nalo wakati tunaendelea kungojea Paradiso hapa duniani.”​—Soma Methali 17:17.

17. (a) Namna gani maneno ya andiko la Isaya 41:13 yanapatana na kazi ya kutolea ndugu misaada? (b) Taja mifano tatu yenye kuonyesha namna kazi ya kutolea ndugu misaada inamuheshimisha Yehova na inafanya umoja wetu uwe na nguvu. (Soma pia kisanduku “ Wafanyakazi Kutoka Katika Dunia Yote Wanajitolea ili Kutoa Misaada.”)

17 Wakati ndugu ambao wanafanya kazi ya kutoa misaada wanafika mahali ambapo kulitokea musiba, ndugu ambao wamepatwa na musiba wanajionea katika njia ya kipekee ukweli wa ahadi hii ya Mungu: ‘Mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika mukono wako wa kuume, Mwenye kukuambia, Usiogope. Mimi mwenyewe nitakusaidia.’ (Isa. 41:13) Dada mumoja ambaye aliokoka musiba, alisema hivi: “Wakati niliona uharibifu ambao uliletwa na musiba, sikuwa tena na tumaini, lakini Yehova alinyoosha mukono wake. Musaada ambao ndugu walinitolea ulikuwa mukubwa sana.” Kisha musiba kuharibu eneo fulani, wazee wawili wa mahali hapo waliandika hivi kwa jina la makutaniko yao: “Tetemeko la udongo lilileta mateso makubwa, lakini tulijionea musaada wa Yehova kupitia ndugu zetu. Tulikuwa tumesoma juu ya kazi ya kutolea ndugu misaada, lakini sasa tumejionea na macho yetu namna kazi hiyo inafanywa.”

Unaweza pia Kusaidia?

18. Unapaswa kufanya nini ikiwa unapenda kuonja furaha ya kazi ya kutolea ndugu misaada? (Soma pia kisanduku “ Ilimusaidia Kutumia Maisha Yake Vizuri.”)

18 Ungependa pia kuonja furaha ya kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu? Ikiwa ndiyo, kumbuka kwamba wafanyakazi hao wanachaguliwa katikati ya ndugu na dada ambao wanajenga Majumba ya Ufalme. Kwa hiyo, uwaambie wazee wa kutaniko lako kwamba unapenda kujaza fomu. Muzee fulani mwenye uzoefu katika kazi ya kutolea ndugu misaada alitoa shauri hili: “Mbele ya kuenda katika eneo ili kusaidia, ngojea mupaka wakati utaitwa na Halmashauri ya Misaada ya Wakati wa Misiba.” Kwa kufanya hivyo, kazi yetu itafanywa kwa utaratibu.

 19. Namna gani wafanyakazi wa kutolea ndugu misaada wanasaidia sana kuonyesha kwamba sisi ni wanafunzi wa kweli wa Kristo?

19 Kwa kweli, kufanya kazi ya kutolea ndugu misaada ni njia ya maana sana ambayo kupitia hiyo tunaonyesha kwamba tunatii amri ya Kristo ambayo inatuomba kuwa na “upendo kati [yetu] wenyewe.” Kwa kuwa na upendo kama huo, tunaonyesha kwamba sisi ni wanafunzi wa kweli wa Kristo. (Yoh. 13:34, 35) Sisi ni wenye kubarikiwa kabisa kwa sababu tuko na wafanyakazi wengi sana wenye kujipendea ambao wanamuletea Yehova utukufu wakati wanatoa musaada kwa wale ambao wanaunga Ufalme wa Mungu mukono kwa uaminifu!

^ fu. 3 Sura hii inazungumuzia namna tunajikaza ili kutolea ndugu na dada misaada wakati wa magumu. Lakini, mara nyingi, tunatolea pia misaada watu wasio Mashahidi.​—Gal. 6:10.

^ fu. 5 Mutume Paulo alitumia pia neno diaʹkonos (muhuduma) ili kuzungumuzia “watumishi wa huduma.”​—1 Tim.3:12.

^ fu. 10 Soma habari “Kusaidia Familia Yetu ya Waamini Katika Bosnia,” katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 11, 1994, ukurasa 23-27.