Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Barua ya Baraza Lenye Kuongoza

Barua ya Baraza Lenye Kuongoza

Muhubiri Mupendwa wa Ufalme:

JARIBU kufikiria kwamba wewe ni mwanabeteli wa Brooklyn, na Siku ya tano asubuhi tarehe 2 Mwezi wa 10, 1914, munakaa kama kawaida ili kula chakula cha asubuhi. Munangojea Ndugu C. T. Russell, na mara moja mulango wa chumba cha kulia unafunguka, naye anaingia. Kama ilivyo kawaida yake anatua kidogo, kisha kwa furaha anasalimia familia yote ya Beteli kwa maneno haya: “Jambo ndugu na dada.” Lakini, siku hiyo kuliko kuenda mara moja kukaa mahali kwenye anazoea kukaa ili kuongoza ibada ya asubuhi, anapiga mikono na kutoa tangazo hili lenye kufurahisha: “Nyakati za Mataifa zimekwisha; siku za wafalme wao zimekwisha!” Bila shaka, ni vigumu kuzuia furaha yako, kwa sababu umekuwa ukingojea wakati huo kwa muda murefu! Wewe na wengine katika familia ya Beteli munapokea habari hiyo yenye kusisimua na munapiga mikono kwa furaha kubwa sana.

Kumepita miaka mingi tangu wakati Ndugu Russell alitoa tangazo hilo ambalo lilifurahisha sana. Lakini ulizo ni hili: Ufalme umetimiza mambo gani tangu wakati huo? Umetimiza mambo mengi sana! Hatua kwa hatua, Yehova amesafisha na kuzoeza watu wake kupitia Ufalme. Katika mwaka wa 1914, watu hao walikuwa wadogo sana, lakini leo wamekuwa zaidi ya watu milioni saba na nusu. Ni katika njia gani mbalimbali wewe mwenyewe umefaidika na mazoezi hayo?

Leo, ni kawaida kusikia ndugu zetu wanasema, “Gari la Yehova la mbinguni linasonga mbele!” na hilo ni kweli kabisa. Hata hivyo, jambo la hakika ni kwamba tangu mwaka wa 1914, gari hilo la Yehova, ni kusema, sehemu ambayo haionekane ya tengenezo lake la mbinguni, limekuwa lenye kusonga mbele kila siku. Usomaji wa kitabu hiki kwa uangalifu utakusaidia kutambua jambo hilo. Kwa sababu wahubiri wa Ufalme wamekusudia kwamba habari njema inapaswa kuhubiriwa duniani pote, wametumia na kuunda njia nyingi mbalimbali ili kufikia kusudi hilo. Kwa mufano, wametumia magazeti ya ulimwengu, wametembea kama watu wenye kufanya maandamano, wametumia filme, karte za kutoa ushahidi, fono, radio, na hata Internete.

Yehova amebariki kazi hii kwa sababu leo tunachapisha vichapo vyetu vyenye kutegemea Biblia na vyenye kupendeza katika luga zaidi ya 670, na tunamutolea kila mutu vichapo hivyo bila kuomba feza. Ndugu na dada wenye kujitoa kwa kupenda wanasaidia katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme, Majumba ya Mikusanyiko, na ujenzi wa tawi mbalimbali katika inchi ambazo ni tajiri na pia katika inchi masikini. Na wakati magumu inatokea, ndugu na dada wenye upendo wanafanya haraka ili kuenda kuwasaidia ndugu zao ambao wako katika maeneo hayo. Kwa kufanya hivyo, wanaonyesha kwamba wao ni ndugu ambao ‘walizaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.’​—Met. 17:17.

Wakati fulani, viongozi wa dini na wapinzani wengine walitunga ‘matatizo kwa njia ya amri [ao sheria],’ lakini jambo lenye kutia imani nguvu ni kuona kwamba, mara kwa mara nguvu zao zote za kutaka kutuangamiza zimesaidia “kuendeleza mbele habari njema.”​—Zab. 94:20; Flp. 1:12.

Ni pendeleo kubwa sana kutumika pamoja na nyinyi ambao ni “watumishi wa nyumbani” wenzetu. Tafazali, mujue kwamba tunawapenda sana nyinyi wote. Tunaendelea kusali kwamba habari ambazo zinapatikana katika kitabu hiki zikusaidie uone uriti wako wa kiroho kuwa kitu cha bei sana kuliko wakati mwingine wowote.—Mt. 24:45.

Tunawatakia mambo mazuri, sisi

Ndugu zenu,

Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova