Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kushoto: Dada huko Alabama, Marekani, akicheza hotuba iliyorekodiwa ya Ndugu Rutherford, mwishoni mwa miaka ya 1930

SEHEMU YA 1

Kweli ya Ufalme​—Kuandaa Chakula cha Kiroho

Kweli ya Ufalme​—Kuandaa Chakula cha Kiroho

UNAMTAZAMA mwanafunzi wako wa Biblia na kumwona akiwa mwenye shangwe kwa sababu ameelewa vizuri andiko ambalo mmetoka tu kusoma. Anasema hivi kwa sauti ya upole, “Yaani unamaanisha Biblia inafundisha kwamba tunaweza kuishi milele katika Paradiso—hapa hapa duniani?” Mhubiri uliyeandamana naye katika huduma anatabasamu kisha anauliza, “Wewe umeona nini katika andiko hilo?” Akiwa mwenye shauku, mwanafunzi huyo anatikisa kichwa kwa kustaajabu, na kusema, “Siamini kwamba eti sijawahi kufundishwa jambo hili!” Unakumbuka kwamba alisema maneno kama hayo majuma machache tu yaliyopita, alipojifunza kwa mara ya kwanza kwamba jina la Mungu ni Yehova.

Je, umewahi kujionea jambo kama hilo? Watu wengi wa Mungu wamejionea hali hiyo. Mambo kama hayo hutukumbusha kwamba tumepewa zawadi yenye thamani sana—ujuzi wa ile kweli! Hata hivyo, tua kidogo na ujiulize: Uliipataje zawadi hiyo? Katika sehemu hii tutachunguza swali hilo. Namna ambavyo watu wa Mungu wamepata uelewaji wa kiroho hatua kwa hatua ni uthibitisho wa kutosha kwamba Ufalme wa Mungu ni halisi. Kwa karne moja, Mfalme wa Ufalme huo, Yesu Kristo, amekuwa akihakikisha kwamba watu wa Mungu wanafundishwa ile kweli.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 3

Yehova Anafunua Kusudi Lake

Je, Ufalme ulikuwa sehemu ya kusudi la Mungu la awali? Yesu aliufunuaje Ufalme?

SURA YA 4

Yehova Analikweza Jina Lake

Ufalme umetimiza nini kuhusiana na jina la Mungu? Wewe binafsi unawezaje kushiriki katika kulitakasa jina la Yehova?

SURA YA 5

Mfalme Anaufunua Ufalme

Pata uelewaji sahihi kuhusu Ufalme wa Mungu, watawala na raia wake, na uhitaji wa kuwa washikamanifu.