Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kushoto: Katika mwaka wa 1931, dada huyu ambaye ni kolpotere anahubiri katika inchi ya Korea; kuume: Katika Korea leo, dada hawa wanahubiri katika luga ya ishara

SEHEMU YA 2

Kazi ya Kuhubiri Ufalme—Kueneza Habari Njema Duniani Pote

Kazi ya Kuhubiri Ufalme—Kueneza Habari Njema Duniani Pote

WAZIA ni siku yako ya kupumuzika; lakini asubui unafikiria kuenda katika mahubiri. Hata hivyo, unasita kidogo, kwa sababu unajisikia kuwa mwenye kuchoka. Kwa hiyo, unaona ni vizuri uendelee kulala! Lakini unasali juu ya jambo hilo na unaamua kuenda katika mahubiri. Siku hiyo, unahubiri na dada fulani mwaminifu na mwenye kuzeeka ambaye uvumilivu na wema wake unagusa moyo wako. Tena wakati munahubiria watu nyumba kwa nyumba ujumbe wa ile kweli, unakumbuka kwamba wakati huohuo ndugu na dada duniani kote wanatangaza pia ujumbe huohuo na wanatumia vichapo ambavyo unatumia, na wote wanafaidika na mazoezi ambayo unapata. Wakati unarudi nyumbani, unajisikia kuwa mwenye nguvu zaidi. Unajisikia mwenye furaha sana kwa sababu haukubaki nyumbani!

Leo, kazi ya kuhubiri ndio kazi ya maana sana ya Ufalme wa Mungu ambayo Wakristo wanapaswa kufanya. Yesu alitabiri kwamba katika siku za mwisho kazi ya kuhubiri inapaswa kufanywa duniani pote. (Mt. 24:14) Unabii huo unatimizwa namna gani? Katika sehemu hii, tutazungumuzia watu, njia mbalimbali, na vyombo ambavyo vimesaidia sana Wakristo kutimiza kazi ya kuhubiri. Tutaona pia namna watu wengi duniani wamesaidiwa kuona kwamba Ufalme wa Mungu ni jambo la kweli.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 6

Watu Wanaofanya Kazi ya Kuhubiri—Wahubiri Wanajitoa Kwa Kupenda

Sababu gani Yesu alitumaini kabisa kwamba katika siku za mwisho atakuwa na jeshi la wahubiri wenye kujitoa kwa kupenda? Namna gani unaweza kuonyesha kwamba unaendelea kutafuta kwanza Ufalme?

SURA YA 7

Njia Mbalimbali Zilizotumiwa Ili Kuhubiri​—Kutumia Kila Njia Ili Kuhubiria Watu

Jifunze juu ya ufundi mupya ambao watu wa Mungu wametumia ili kuhubiria watu wengi habari njema kadiri inavyowezekana mbele ya mwisho kuja.

SURA YA 8

Vyombo kwa Ajili ya Kazi ya Kuhubiri—Vichapo kwa Ajili ya Kazi ya Kuhubiri Duniani Pote

Sababu gani tunaweza kusema kwamba kazi yetu ya kutafsiri inategemezwa na Yesu? Ni mambo gani juu ya vichapo vyetu yanaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu ni jambo la kweli?

SURA YA 9

Matokeo ya Kazi ya Kuhubiri: ‘Mashamba Yamekuwa Meupe, Tayari kwa Mavuno”

Yesu alifundisha mitume wake mambo mbili ya lazima kuhusu mavuno ya kiroho. Namna gani mambo hayo yanatuchochea leo?