Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kushoto: Familia ya Betheli ya Brooklyn ikisherehekea Krismasi kwa mara ya mwisho mwaka wa 1926; Kulia: Watu huona kwamba Mashahidi wa Yehova wako tofauti

SEHEMU YA 3

Viwango vya Ufalme​—Kuutafuta Uadilifu wa Mungu

Viwango vya Ufalme​—Kuutafuta Uadilifu wa Mungu

UNAMSALIMU jirani yako unapopita njiani. Hivi karibuni, umeona kwamba amekuwa akikuchunguza wewe na familia yako. Anakusalimu kisha anasema: “Naomba nikuulize swali? Ni nini kinachowafanya ninyi muwe tofauti?” “Unamaanisha nini?” unauliza. Anasema, “Ninyi ni Mashahidi wa Yehova, sivyo? Ninyi si kama watu wengine. Hamchangamani na dini nyingine—hamsherehekei sikukuu, na hamjihusishi katika siasa na vita. Hamvuti sigara. Na familia yako inaonekana kuwa inafuata viwango vya juu vya maadili. Ni nini kinachowafanya muwe tofauti sana na wengine?”

Unajua jibu: Tunaishi chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu. Akiwa Mfalme, Yesu anaendelea kutusafisha. Anatusaidia tufuate hatua zake na hivyo tuwe tofauti kabisa na ulimwengu huu mwovu. Katika sehemu hii, tutaona jinsi ambavyo Mfalme wa Kimasihi amekuwa akiwasafisha watu wa Mungu kiroho, kiadili, na kitengenezo—yote hayo yakifanywa kwa utukufu wa Yehova.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 10

Mfalme Anawasafisha Watu Wake Kiroho

Krismasi na msalaba vina vyanzo gani?

SURA YA 11

Usafi wa Maadili​—Unaonyesha Utakatifu wa Mungu

Vyumba vya walinzi na malango katika maono ya Ezekieli ya hekalu yamekuwa na maana ya pekee kwa watu wa Mungu tangu mwaka wa 1914.

SURA YA 12

Tengenezo Linalomtumikia “Mungu wa Amani”

Biblia haitofautishi vurugu na utaratibu bali na amani. Kwa nini? Na jibu linawahusuje Wakristo leo?