SEHEMU YA 3
Kanuni za Ufalme—Kuendelea Kutafuta Haki ya Mungu
WAZIA unapita pamoja na familia yako na unamupepea jirani yako kwa kumusalimu. Mbele ya hapo, umetambua kwamba alikuwa anawaangalia. Yeye pia anakupepea na anakuomba usimame kidogo. Anakuambia hivi: “Ninaweza kukuuliza kidogo? Ni nini inawafanya kuwa tofauti na watu wengine?” Wewe pia unamuuliza, “Unataka kusema nini?” Naye anakuambia, “Wewe ni Shahidi wa Yehova, si vile? Ninyi ni tofauti kabisa na watu wengine. Hamuko sawa na dini zingine. Hamufanye sikukuu, na hamujiingize katika siasa na katika vita. Hamuvute tumbaku. Na inaonekana familia yako ina mwenendo muzuri sana. Ni nini inafanya muwe tofauti kabisa hivyo na watu wengine?”
Bila shaka unaweza kumujibu tu hivi: Sisi tunaongozwa na Ufalme wa Mungu. Mufalme wetu Yesu, anaendelea kutusafisha. Anaendelea kutusaidia tufuate hatua zake, ili tuwe tofauti na ulimwengu huu muovu. Katika sehemu hii, tutaona namna Ufalme wa Masiya umeendelea kusafisha watu wa Mungu kiroho, na kuwasaidia wakuwe na mwenendo safi na pia wafuate utaratibu wa tengenezo: Yote hayo yamefanyika kwa utukufu wa Yehova.
KATIKA SEHEMU HII
SURA YA 11
Mwenendo Safi Unaonyesha Utakatifu wa Mungu
Mahali walinzi walikuwa wanasimama katika hekalu ambalo Ezekieli aliona na njia ya kuingilia imekuwa na maana ya pekee kwa watu wa Mungu tangu mwaka wa 1914.
SURA YA 12
Tengenezo Linalotumikia “Mungu wa Amani”
Biblia haiseme kwamba muchafuko haupatane na utaratibu, lakini inaonyesha kwamba muchafuko haupatane na amani. Sababu gani?Namna gani jambo hilo linatimia kwa Wakristo leo?