Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

kushoto: Katika mwaka wa 1926, familia ya Beteli ya Brooklyn inafanya kwa mara ya mwisho sikukuu ya Noeli; kuume: Watu wanatambua kwamba Mashahidi wa Yehova wako tofauti na watu wengine

SEHEMU YA 3

Kanuni za Ufalme—Kuendelea Kutafuta Haki ya Mungu

Kanuni za Ufalme—Kuendelea Kutafuta Haki ya Mungu

WAZIA unapita pamoja na familia yako na unamupepea jirani yako kwa kumusalimu. Mbele ya hapo, umetambua kwamba alikuwa anawaangalia. Yeye pia anakupepea na anakuomba usimame kidogo. Anakuambia hivi: “Ninaweza kukuuliza kidogo? Ni nini inawafanya kuwa tofauti na watu wengine?” Wewe pia unamuuliza, “Unataka kusema nini?” Naye anakuambia, “Wewe ni Shahidi wa Yehova, si vile? Ninyi ni tofauti kabisa na watu wengine. Hamuko sawa na dini zingine. Hamufanye sikukuu, na hamujiingize katika siasa na katika vita. Hamuvute tumbaku. Na inaonekana familia yako ina mwenendo muzuri sana. Ni nini inafanya muwe tofauti kabisa hivyo na watu wengine?”

Bila shaka unaweza kumujibu tu hivi: Sisi tunaongozwa na Ufalme wa Mungu. Mufalme wetu Yesu, anaendelea kutusafisha. Anaendelea kutusaidia tufuate hatua zake, ili tuwe tofauti na ulimwengu huu muovu. Katika sehemu hii, tutaona namna Ufalme wa Masiya umeendelea kusafisha watu wa Mungu kiroho, na kuwasaidia wakuwe na mwenendo safi na pia wafuate utaratibu wa tengenezo: Yote hayo yamefanyika kwa utukufu wa Yehova.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 10

Mufalme Anasafisha Wafuasi Wake Kiroho

Ni upatano gani ulio kati ya Noeli na musalaba?

SURA YA 11

Mwenendo Safi Unaonyesha Utakatifu wa Mungu

Mahali walinzi walikuwa wanasimama katika hekalu ambalo Ezekieli aliona na njia ya kuingilia imekuwa na maana ya pekee kwa watu wa Mungu tangu mwaka wa 1914.

SURA YA 12

Tengenezo Linalotumikia “Mungu wa Amani”

Biblia haiseme kwamba muchafuko haupatane na utaratibu, lakini inaonyesha kwamba muchafuko haupatane na amani. Sababu gani?Namna gani jambo hilo linatimia kwa Wakristo leo?