Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kushoto: Ndugu akikamatwa kwa sababu ya kuhubiri huko Eindhoven, Uholanzi, 1945; kulia: Je, haki ya kuhubiri inalindwa kisheria katika nchi unamoishi?

SEHEMU YA 4

Ushindi wa Ufalme​—Kutetea na Kuithibitisha Kisheria Habari Njema

Ushindi wa Ufalme​—Kutetea na Kuithibitisha Kisheria Habari Njema

MNAPOHUBIRI nyumba kwa nyumba, mnasikia king’ora kwa mbali. Sauti ya king’ora inazidi kuongezeka. Unapoanza kuzungumza na mwenye nyumba anayefuata, shahidi mwenzako anakengeushwa gari la polisi linaposimama karibu nanyi. Polisi anatoka kwenye gari na kuwauliza, “Ninyi ndio mmekuwa mkienda mlango kwa mlango mkizungumzia habari za Biblia? Tumepata malalamiko!” Mnajibu kwa heshima, mkijitambulisha kwamba ninyi ni Mashahidi wa Yehova. Ni nini kitakachotokea?

Kwa kiasi kikubwa, hilo litategemea matukio ya zamani. Kwa miaka mingi, serikali ya nchi unamoishi imewatendeaje Mashahidi wa Yehova? Je, kuna kiasi fulani cha uhuru wa kidini? Ikiwa ndiyo, huenda ni kwa sababu kwa miaka mingi ndugu na dada zako wa kiroho wamejitahidi sana “kutetea na kuithibitisha kisheria habari njema.” (Flp. 1:7) Hata uwe unaishi wapi, kutafakari masimulizi ya ushindi wa kisheria wa Mashahidi wa Yehova kunaweza kuimarisha sana imani yako. Katika sehemu hii, tutachunguza baadhi ya ushindi huo wenye kutokeza. Ushindi ambao tumepata unathibitisha kwamba Ufalme ni halisi, kwani hatungepata ushindi mkubwa hivyo kwa uwezo wetu wenyewe!

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 13

Wahubiri wa Ufalme Wanapeleka Kesi Mahakamani

Mahakimu fulani katika mahakama za juu leo wana maoni kama yale ya mwalimu wa Sheria Gamalieli.

SURA YA 14

Kuunga Mkono kwa Ushikamanifu Serikali ya Mungu Pekee

“Mto” wa mateso yaliyoletwa dhidi ya Mashahidi wa Yehova kwa sababu ya kutounga mkono upande wowote katika siasa umemezwa na chanzo kisichotarajiwa.

SURA YA 15

Kupigania Uhuru wa Kuabudu

Watu wa Mungu wamepigana ili wapate haki ya kutii sheria​​—⁠sheria ya Ufalme wa Mungu.