Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

kushoto: Ndugu anakamatwa kwa sababu ya kuhubiri katika Eindhoven, Uholanzi, mwaka wa 1945; kuume: Mahali ambako unaishi, sheria ya serikali inakuruhusu kuhubiri?

SEHEMU YA 4

Ushindi Mbalimbali wa Ufalme​—Mashahidi wa Yehova Wanafanya Habari Njema Ijulikane Kisheria

Ushindi Mbalimbali wa Ufalme​—Mashahidi wa Yehova Wanafanya Habari Njema Ijulikane Kisheria

WAZIA munahubiri nyumba kwa nyumba. Munasikia sauti ya honi (sirène) ya motokari ya polisi kwa mbali. Sauti hiyo inaendelea kuongezeka. Wakati unaanza kuzungumuza na mutu kwenye mulango unaofuata, muhubiri mwenzako anakengeushwa wakati motokari ya polisi inakuja kusimama karibu yenu. Polisi mumoja anatoka katika motokari, anawakaribia na kuwauliza hivi: “Ni nyinyi wawili ndio mumekuwa munahubiri nyumba kwa nyumba? Wametuelezea jambo hilo!” Munamujibu kwa heshima kwamba ninyi ni Mashahidi wa Yehova. Mutafungwa ao hapana?

Jibu la ulizo hilo litategemea hali ya inchi yenu. Kwa miaka mingi, serikali ya inchi yenu imetendea Mashahidi wa Yehova namna gani? Katika inchi yako, Mashahidi wamepewa uhuru wa dini? Ikiwa ndiyo, jua kwamba ni kwa sababu kwa miaka mingi ndugu na dada zako wa kiroho wamefanya nguvu ili ‘kutetea habari njema’ na kuifanya ijulikane “kisheria.” (Flp. 1:7) Hata unaishi wapi, kutafakari juu ya ushindi mbalimbali wa kisheria ambao Mashahidi wa Yehova wamepata, kunaweza kufanya imani yako iwe nguvu sana. Katika sehemu hii, tutachunguza ushindi huo wa maana sana. Ushindi mbalimbali ambao tumepata ni ushuhuda wenye nguvu kwamba Ufalme wa Mungu ni jambo la kweli kabisa, kwa sababu hatungeweza kupata ushindi huo wote kwa nguvu zetu wenyewe!

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 13

Wahubiri Wa Ufalme Wanajitetea Kwenye Tribinali

Waamuzi fulani wa wakati wetu wana maoni kama ya mwalimu wa sheria wa zamani Gamalieli.

SURA YA 14

Waliunga Mukono kwa Ushikamanifu Serikali ya Mungu Tu

Ule “muto” ambao unafananishwa na mateso ambao ulitaka kuangamiza Mashahidi wa Yehova kwa sababu walikataa kujiingiza katika mambo ya siasa ulimezwa kwa njia ambayo haikutazamiwa.

SURA YA 15

Kupigania Uhuru wa Kuabudu

Watu wa Mungu wamepigania haki ya kutii sheria— sheria za Ufalme wa Mungu.