Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kushoto: Mkutano uliofanywa nje huko London, Uingereza, 1945; kulia: Kusanyiko la pekee huko Malawi, Afrika, 2012,

SEHEMU YA 5

Elimu ya Ufalme​—Kuwazoeza Watumishi wa Mfalme

Elimu ya Ufalme​—Kuwazoeza Watumishi wa Mfalme

UNATABASAMU unapomtazama msemaji jukwaani. Yeye ni ndugu kijana katika kutaniko lenu, na anatoa hotuba yake ya kwanza katika programu ya kusanyiko. Unapomsikiliza, unastaajabishwa na jinsi ambavyo watu wa Mungu wamezoezwa. Unakumbuka hotuba ya kwanza ya kijana huyo na unaona jinsi ambavyo amefanya maendeleo. Alizoezwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, kisha katika Shule ya Utumishi wa Painia. Hivi karibuni, yeye na mke wake walifurahia kuhudhuria Shule ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Unapopiga makofi kwa sababu ya hotuba nzuri ya ndugu huyo, unatazama huku na huku na kutafakari jinsi ambavyo watu wa Mungu wamefundishwa.

Biblia ilitabiri wakati ambapo watu wa Mungu ‘wangefundishwa na Yehova.’ (Isa. 54:13) Tunaishi wakati huo. Tunaelimishwa kupitia machapisho yetu, mikutano, makusanyiko, na shule mbalimbali ambazo zimekusudiwa kututayarisha kwa ajili ya migawo hususa katika tengenezo la Yehova. Katika sehemu hii, tutazungumzia jinsi ambavyo elimu hiyo inatoa uthibitisho hakika kwamba Ufalme wa Mungu unatawala leo.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 16

Kukusanyika Pamoja kwa Ajili ya Ibada

Tunaweza kufaidikaje zaidi tunapohudhuria mikutano ili kumwabudu Yehova?

SURA YA 17

Kuwazoeza Wahudumu wa Ufalme

Shule za kitheokrasi zimewatayarishaje wahudumu wa Ufalme kutimiza migawo yao?