Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kushoto: Mukutano unafanywa inje katika muji wa Londres, Uingereza, mwaka wa 1945; kuume: Mukusanyiko wa pekee wa siku moja katika inchi ya Malawi, Afrika, Mwaka wa 2012

SEHEMU YA 5

Masomo ya Ufalme —Watumishi wa Mufalme Wanapewa Mazoezi

Masomo ya Ufalme —Watumishi wa Mufalme Wanapewa Mazoezi

Wazia jambo hili: unamuangalia musemaji aliye kwenye jukwaa na unaonyesha sura yenye kicheko. Musemaji huyo ni ndugu kijana wa kutaniko lenu, na anatoa hotuba yake mara ya kwanza kwenye mukusanyiko. Wakati unaendelea kufurahia hotuba yake, unashangaa sana kuona mazoezi ambayo watu wa Mungu wanapata. Unakumbuka kipindi ambacho alitoa kwa mara ya kwanza katika kutaniko, na unashangaa kuona namna amefanya maendeleo! Alifanya maendeleo mazuri kisha kuhuzuria Masomo ya Mapainia. Na hivi karibuni, yeye na bibi yake walihuzuria Masomo kwa Ajili ya Waeneza Injili wa Ufalme. Wakati ndugu huyo anamaliza hotuba yake nzuri, unapiga mikono kwa furaha, unaangalia watu ambao wako hapo kwenye mukusanyiko, kisha unafikiri juu ya mazoezi ambayo watu wote wa Mungu wanapewa.

Biblia ilitabiri kwamba kutakuwa wakati ambao watu wote wa Mungu watafundishwa na Yehova. (Isa. 54:13) Tunaishi wakati huo. Tunafundishwa kupitia vichapo vyetu, mikutano yetu, na mikusanyiko yetu mbalimbali. Lakini pia tunafundishwa kupitia masomo mbalimbali ambayo yana kusudi la kututayarisha ili tutimize migao fulani katika tengenezo la Yehova. Katika sehemu hii, tutachunguza namna mafundisho hayo yote yanaonyesha waziwazi kwamba Ufalme wa Mungu unatawala leo.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 16

Kukusanyika Pamoja kwa Ajili ya Ibada

Namna gani tunaweza kufaidika zaidi wakati tunakusanyika ili kumuabudu Yehova?

SURA YA 17

Wahubiri wa Ufalme Wanapewa Mazoezi

Namna gani masomo mbalimbali ya kiteokrasi yametayarisha wahubiri wa Ufalme kutimiza migao yao?