SEHEMU YA 6
Kutegemeza Ufalme—Ujenzi wa Majengo ya Ibada na Kazi ya Kutoa Misaada
UNAINGIA ndani ya Jumba lenu la Ufalme na unaona kila kitu kimebadilika. Siku zote umekuwa ukijivunia jengo hilo. Huenda hata unakumbuka kwamba ulisaidia kulijenga miaka kadhaa iliyopita. Lakini kwa njia fulani unajivunia hata zaidi sasa, kwa kuwa Jumba hilo la Ufalme linatumiwa kama kituo cha muda cha kutoa msaada. Baada ya dhoruba iliyotokea hivi karibuni na kusababisha mafuriko na uharibifu katika eneo lenu, Halmashauri ya Tawi ilifanya mipango haraka ili waathiriwa wapate chakula, mavazi, maji safi, na misaada mingine. Misaada iliyotumwa imepangwa vizuri. Ndugu na dada wanaingia ndani kwa utaratibu na kuchukua vitu wanavyohitaji na, katika visa vingi, wakipangusa machozi ya shangwe.
Yesu alisema kwamba watu wake wangetambuliwa kwa kuwa na upendo miongoni mwao. (Yoh. 13:34, 35) Katika sehemu hii, tutachunguza jinsi ambavyo upendo wa Kikristo unaonyeshwa katika miradi ya ujenzi na kazi ya kutoa misaada inayofanywa na Mashahidi wa Yehova. Upendo huo ni uthibitisho wenye nguvu kwamba tunaishi chini ya utawala wa Ufalme wa Yesu.
KATIKA SEHEMU HII
SURA YA 19
Kazi ya Ujenzi Inayomletea Yehova Sifa
Majengo ya ibada yanamletea sifa Mungu, hata hivyo kuna jambo analothamini zaidi
SURA YA 20
Kazi ya Kutoa Msaada
Tunajuaje kwamba kazi ya kutoa msaada ni sehemu ya utumishi wetu mtakatifu kwa Yehova?