Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kushoto: Msaada ambao ndugu zetu nchini Ujerumani walipokea kutoka Uswisi, 1946; kulia: Rebuilding a Kingdom Hall in Japan after a tsunami, 2011

SEHEMU YA 6

Kutegemeza Ufalme​—Ujenzi wa Majengo ya Ibada na Kazi ya Kutoa Misaada

Kutegemeza Ufalme​—Ujenzi wa Majengo ya Ibada na Kazi ya Kutoa Misaada

UNAINGIA ndani ya Jumba lenu la Ufalme na unaona kila kitu kimebadilika. Siku zote umekuwa ukijivunia jengo hilo. Huenda hata unakumbuka kwamba ulisaidia kulijenga miaka kadhaa iliyopita. Lakini kwa njia fulani unajivunia hata zaidi sasa, kwa kuwa Jumba hilo la Ufalme linatumiwa kama kituo cha muda cha kutoa msaada. Baada ya dhoruba iliyotokea hivi karibuni na kusababisha mafuriko na uharibifu katika eneo lenu, Halmashauri ya Tawi ilifanya mipango haraka ili waathiriwa wapate chakula, mavazi, maji safi, na misaada mingine. Misaada iliyotumwa imepangwa vizuri. Ndugu na dada wanaingia ndani kwa utaratibu na kuchukua vitu wanavyohitaji na, katika visa vingi, wakipangusa machozi ya shangwe.

Yesu alisema kwamba watu wake wangetambuliwa kwa kuwa na upendo miongoni mwao. (Yoh. 13:34, 35) Katika sehemu hii, tutachunguza jinsi ambavyo upendo wa Kikristo unaonyeshwa katika miradi ya ujenzi na kazi ya kutoa misaada inayofanywa na Mashahidi wa Yehova. Upendo huo ni uthibitisho wenye nguvu kwamba tunaishi chini ya utawala wa Ufalme wa Yesu.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 18

Jinsi Kazi za Ufalme Zinavyogharimiwa

Pesa zinatoka wapi? Zinatumiwa jinsi gani?

SURA YA 19

Kazi ya Ujenzi Inayomletea Yehova Sifa

Majengo ya ibada yanamletea sifa Mungu, hata hivyo kuna jambo analothamini zaidi

SURA YA 20

Kazi ya Kutoa Msaada

Tunajuaje kwamba kazi ya kutoa msaada ni sehemu ya utumishi wetu mtakatifu kwa Yehova?