Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kushoto: Katika mwaka wa 1946, ndugu wa Uswisi walitumia ndugu wa Ujerumani misaada wakati wa magumu; kuume: Katika Japani mwaka wa 2011, ndugu wanajenga upya Jumba la Ufalme ambalo liliharibiwa na upepo mukali wa tsunami

SEHEMU YA 6

Kuunga Ufalme Mukono​—Kazi ya Kujenga Mahali pa Ibada na Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu

Kuunga Ufalme Mukono​—Kazi ya Kujenga Mahali pa Ibada na Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu

FIKIRIA jambo hili: Unatembea katika Jumba lenu la Ufalme, lakini unashangaa kuona namna limekuwa. Kwa kawaida umekuwa mwenye kufurahia jumba lenu. Pengine unakumbuka hata namna ulisaidia katika ujenzi wa jumba hilo kumekwisha kupita miaka fulani. Lakini, sasa kuna jambo lingine ambalo linakufanya ufurahi hata zaidi. Jumba lenu la Ufalme limegeuzwa kwa muda fulani kuwa mahali pa kugawia ndugu na dada misaada kwa sababu wamepatwa na magumu. Hivi karibuni, upepo wa mvua kali uliharibu eneo la kwenu, na Halmashauri ya Tawi ilichukua mara moja mipango ya kuwasaidia ndugu na dada ili wapate chakula, mavazi, maji safi na misaada mingine. Kazi ya kutoa misaada imepangwa vizuri. Ndugu na dada ni wenye kuwa kwenye mustari na wanapokea misaada ambayo wanahitaji. Wengi wao wanatoa machozi ya furaha.

Yesu alisema kwamba alama ya maana sana yenye kutambulisha wafuasi wake ni upendo kati yao. (Yoh. 13:34, 35) Katika sehemu hii, tutazungumuzia namna Mashahidi wa Yehova wanaonyesha upendo wao wa Kikristo wakati wa ujenzi mbalimbali, na wakati wanajikaza kutolea ndugu na dada misaada wakati wamepatwa na magumu. Upendo huo ni ushahidi wenye nguvu ambao unaonyesha kwamba tunaongozwa na Ufalme wa Yesu ambao unatawala.

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 18

Feza za Kuendesha Kazi za Ufalme Zinatoka Wapi?

Feza zinatoka wapi? Zinatumiwa namna gani?

SURA YA 19

Kazi ya Ujenzi Ambayo Inamuletea Yehova Heshima

Majumba ya ibada inamuletea Mungu heshima, lakini kuna jambo lingine ambalo anaona kuwa la maana zaidi.

SURA YA 20

Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu

Namna gani tunajua kwamba kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu ni sehemu ya utumishi wetu mutakatifu kwa Yehova?