Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 2

Yesu Anapewa Heshima Mbele ya Kuzaliwa Kwake

Yesu Anapewa Heshima Mbele ya Kuzaliwa Kwake

LUKA 1:34-56

  • MARIA ANAMUTEMBELEA MUTU WA JAMAA YAKE MWENYE KUITWA ELIZABETI

Kisha malaika Gabrieli kumuambia Maria kama atapata mimba na kuzaa mutoto mwenye ataitwa Yesu na mwenye atakuwa Mufalme milele, Maria anauliza hivi: “Hilo litawezekana namna gani kwa kuwa sijalala na mwanaume?”—Luka 1:34.

Gabrieli anamujibu hivi: “Roho takatifu itakuja juu yako, na nguvu za Mwenye Kuwa Juu Zaidi zitakufunika kwa kivuli. Na kwa hiyo ule mwenye atazaliwa ataitwa mutakatifu, Mwana wa Mungu.”—Luka 1:35.

Pengine ili kusaidia Maria akubali ujumbe wake, Gabrieli anaongeza hivi: “Angalia! Elizabeti mutu wa jamaa yako amepata mimba, katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, ule mwenye kuitwa mwanamuke tasa; kwa sababu kwa Mungu hakuna neno lenye haliwezekane.”—Luka 1:36, 37.

Jibu la Maria linaonyesha kama anakubali mambo yenye Gabrieli anamuambia. Anasema hivi: “Angalia! Mimi ni mutumwa wa Yehova! Na itendeke kwangu kulingana na tangazo lako.”—Luka 1:38.

Kisha tu Gabrieli kuenda, Maria anajitayarisha kuenda kumutembelea Elizabeti, mwenye anaishi pamoja na Zekaria, bwana yake, karibu na Yerusalemu katika vilima vya Yudea. Kutoka Nazareti kwenye Maria alikuwa anaishi mupaka kwa Elizabeti, ni safari yenye ingeweza kuchukua siku tatu ao ine.

Mwishowe, Maria anafika kwa Zekaria. Wakati anaingia, anamusalimia Elizabeti, mutu wa jamaa yake. Mara moja Elizabeti anajazwa roho takatifu, na anamuambia Maria hivi: “Umebarikiwa kati ya wanamuke, na uzao wa tumbo lako la uzazi umebarikiwa! Basi, namna gani nimepata pendeleo hili, kumupokea kwangu mama ya Bwana wangu? Kwa maana, angalia! wakati tu nilisikia salamu yako, mutoto mwenye kuwa katika tumbo langu la uzazi aliruka kwa furaha.”—Luka 1:42-44.

Kisha Maria anajibia kwa kusema maneno ya shukrani yenye kutoka moyoni. Anasema hivi: “Nafsi yangu inamutukuza Yehova, na roho yangu haiwezi kuacha kufurahia sana Mungu Mwokozi wangu, kwa sababu ameangalia hali ya chini ya mutumwa wake. Kwa maana angalia! tangu sasa na kuendelea vizazi vyote vitanitangaza kuwa mwenye furaha, kwa sababu Mwenye nguvu amenitendea mambo ya ajabu.” Tunaona kwamba hata kama alipata pendeleo hilo, Maria anamupatia Mungu heshima yote. Anasema hivi: “Jina lake ni takatifu, na kizazi kisha kizazi, rehema yake iko juu ya wale wenye kumuogopa.”—Luka 1:46-50.

Katika maneno ya kiunabii yenye kuongozwa na roho ya Mungu, Maria anaendelea kumusifu Mungu, na kusema: “Ametenda kwa nguvu kwa mukono wake; amesambaza wale wenye majivuno katika kusudi la mioyo yao. Ameshusha watu wenye nguvu kutoka kwenye viti vya ufalme na ameinua watu wa hali ya chini; ameshibisha kabisa wenye njaa kwa vitu vya muzuri, na ameacha wenye walikuwa na mali waende mikono wazi. Amesaidia Israeli mutumishi wake, amekumbuka rehema yake, kama vile tu aliahidi mababu zetu, Abrahamu na uzao wake, milele.”—Luka 1:51-55.

Maria anafanya miezi karibu tatu kwa Elizabeti, pengine juu ya kumusaidia katika majuma hayo ya mwisho-mwisho mbele Elizabeti azae. Ni jambo lenye kupendeza kabisa kuona namna wanamuke hao wawili waaminifu wako pamoja wakati huo wa maisha yao, kila mumoja wao akiwa na mutoto katika tumbo lake la uzazi kwa musaada wa Mungu!

Ona tena namna Yesu anapewa heshima mbele hata azaliwe. Elizabeti anamuita “Bwana wangu,” na mutoto katika tumbo lake la uzazi “aliruka kwa furaha” wakati tu alimuona Maria. Ni tofauti kabisa na namna watu wengine watamutendea Maria na mutoto wake mwenye atazaliwa, kama vile tutaona.