Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 12

Yesu Anabatizwa

Yesu Anabatizwa

MATAYO 3:13-17 MARKO 1:9-11 LUKA 3:21, 22 YOHANA 1:32-34

  • YESU ANABATIZWA NA KUTIWA MAFUTA

  • YEHOVA ANAMUTANGAZA YESU KUWA MWANA WAKE

Miezi sita hivi kisha Yohana Mubatizaji kuanza kazi ya kuhubiri, Yesu, mwenye iko sasa na miaka 30 hivi, anakuja kumuona Yohana kwenye Muto Yordani. Juu ya nini? Hakuje tu kumutembelea kwa sababu ni rafiki yake. Ao, Yesu hapendi tu kuona namna kazi ya Yohana iko inaendelea. Hapana, Yesu anakuja kumuomba Yohana amubatize.

Yohana anamuzuia, na iko na sababu ya kufanya hivyo. Anamuambia hivi: “Ni wewe unastahili kunibatiza, sasa wewe unakuja kwangu?” (Matayo 3:14) Yohana anajua kuwa Yesu ni Mwana wa pekee wa Mungu. Kumbuka kama wakati Yohana alikuwa angali katika tumbo la mama yake, aliruka kwa furaha wakati Maria, mwenye alikuwa na mimba ya Yesu, alitembelea Elizabeti, mama ya Yohana. Inawezekana mama ya Yohana alifikia kumuambia juu ya jambo hilo. Na inapaswa kuwa alisikia juu ya tangazo lenye malaika alitoa kuhusu kuzaliwa kwa Yesu na kuhusu malaika wenye waliwatokea wachungaji usiku wenye Yesu alizaliwa.

Yohana anaelewa kuwa ubatizo wenye iko anafanya ni kwa ajili ya wale wenye kutubu zambi zao. Lakini Yesu hana zambi. Hata kama Yohana anataka kumuzuia, Yesu anaendelea kumuomba: “Acha ikuwe vile kwa wakati huu, kwa sababu ni katika njia hiyo tunapaswa kufanya yote yenye Mungu anapenda.”—Matayo 3:15.

Sababu gani inafaa Yesu abatizwe? Ubatizo wa Yesu haiko alama yenye kuonyesha kuwa ametubu zambi. Ubatizo wake unaonyesha kuwa anajitoa mwenyewe ili kufanya mapenzi ya Baba yake. (Waebrania 10:5-7) Yesu amekuwa akifanya kazi ya useremala (kazi ya mbao), lakini sasa wakati umefika ili aanze utumishi wenye Baba yake wa mbinguni alimutuma kufanya katika dunia. Unawaza kuwa Yohana anatazamia kuona jambo fulani la kushangaza wakati atamubatiza Yesu?

Yohana alifikia kusema hivi: “Ule mwenye alinituma nibatize katika maji aliniambia: ‘Mutu yeyote mwenye utaona roho inashuka na kukaa juu yake, huyo ndiye mwenye anabatiza katika roho takatifu.’” (Yohana 1:33) Kwa hiyo, Yohana anatazamia kuona roho ya Mungu inashuka juu ya mutu mwenye anabatiza. Ndiyo sababu, kisha tu Yesu kutoka katika maji, inawezekana Yohana hashangae kuona “roho ya Mungu ikishuka kama njiwa, ikikuja juu ya Yesu.”—Matayo 3:16.

Lakini mambo mengine yanatokea wakati Yesu anabatizwa. ‘Mbingu zinafunguliwa’ juu yake. Hilo linamaanisha nini? Pengine hilo linamaanisha kuwa wakati wa ubatizo wake, Yesu alikumbuka maisha yake ya mbinguni mbele akuje duniani. Kwa hiyo, Yesu anakumbuka sasa maisha yake akiwa mwana wa roho wa Yehova, kutia ndani mambo yenye Mungu alimufundisha mbinguni mbele akuje duniani.

Zaidi ya hilo, wakati wa ubatizo wa Yesu, sauti kutoka mbinguni inatangaza hivi: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali.” (Matayo 3:17) Sauti hiyo ni ya nani? Haiwezi kuwa sauti ya Yesu kwa sababu iko pale pamoja na Yohana. Sauti hiyo ni ya Mungu. Ni wazi kwamba, Yesu ni Mwana wa Mungu. Yeye haiko Mungu mwenyewe.

Ni wazi kwamba Yesu ni mwana wa kibinadamu wa Mungu, kama vile tu ule mwanaume wa kwanza, Adamu alikuwa. Kisha kuzungumuzia ubatizo wa Yesu, mwanafunzi Luka anaandika hivi: “Wakati Yesu alianza kazi yake, alikuwa na miaka karibu makumi tatu (30). Na watu walimuona kuwa mwana wa Yosefu, mwana wa Heli, . . . mwana wa Daudi, . . . mwana wa Abrahamu, . . . mwana wa Noa, . . . mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.”—Luka 3:23-38.

Kama vile tu Adamu alikuwa “mwana [wa kibinadamu] wa Mungu,” ni vile pia Yesu. Wakati anabatizwa, Yesu anaanzisha uhusiano mwingine pamoja na Mungu, anakuwa Mwana wa Mungu wa kiroho. Sasa, Yesu iko tayari kufundisha kweli yenye kutoka kwa Mungu na kuonyesha njia yenye kuongoza kwenye uzima. Yesu anaanza maisha yenye yatafikia kumuongoza atoe uzima wake kama zabihu kwa ajili ya wanadamu watenda-zambi.