Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 17

Anafundisha Nikodemo Wakati wa Usiku

Anafundisha Nikodemo Wakati wa Usiku

YOHANA 2:23–3:21

  • YESU ANAZUNGUMUZA NA NIKODEMO

  • “KUZALIWA TENA,” MAANA YAKE NINI?

Wakati iko katika Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka ya mwaka wa 30 wakati wetu, Yesu anafanya alama za ajabu, ao miujiza. Kwa hiyo, watu wengi wanaonyesha imani katika yeye. Nikodemo, Mufarisayo na mwenye kuwa katika tribinali kubwa ya Wayahudi yenye kuitwa Sanhedrini, anashangaa. Kwa sababu anapenda kujua mengi, anamutembelea Yesu usiku, pengine ni kwa sababu anaogopa kuwa ataharibu sifa yake ikiwa viongozi wengine Wayahudi wanamuona.

Nikodemo anamuambia hivi: “Rabi, tunajua kama umetoka kwa Mungu ukiwa mwalimu, kwa maana hakuna mwenye anaweza kufanya alama hizi zenye unafanya kama Mungu haiko pamoja naye.” Yesu anamujibu Nikodemo kwa kumuambia kama, ili mutu aingie katika Ufalme wa Mungu, anapaswa ‘kuzaliwa tena.’—Yohana 3:2, 3.

Lakini, namna gani mutu anaweza kuzaliwa tena? Nikodemo anauliza hivi: “Je, anaweza kuingia katika tumbo la uzazi la mama yake mara ya pili na kuzaliwa tena?”—Yohana 3:4.

Hapana, kuzaliwa tena hakumaanishe hivyo. Yesu anafasiria hivi: “Kama mutu hazaliwe kwa maji na roho, hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu.” (Yohana 3:5) Wakati Yesu alibatizwa na wakati roho takatifu ilishuka juu yake, alizaliwa “kwa maji na roho.” Wakati huo, kulikuwa tangazo kutoka mbinguni lenye kusema: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali.” (Matayo 3:16, 17) Kwa njia hiyo, Mungu alitangaza kuwa sasa Yesu amekuwa mwana wake wa kiroho mwenye kuwa na nafasi ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Kisha, kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33 wakati wetu, roho takatifu itamwangwa juu ya wengine wenye wamebatizwa, na kwa hiyo, watakuwa wamezaliwa tena na kuwa wana wa kiroho wa Mungu.—Matendo 2:1-4.

Ni nguvu Nikodemo aelewe mambo yenye Yesu iko anamufundisha juu ya Ufalme. Kwa hiyo, Yesu anamutolea habari zaidi kuhusu daraka lake la pekee akiwa Mwana wa kibinadamu wa Mungu. Yesu anamuambia hivi: “Kama vile Musa aliinua nyoka katika jangwa, ni vile Mwana wa binadamu anapaswa kuinuliwa, ili kila mutu mwenye anamuamini apate uzima wa milele.”—Yohana 3:14, 15.

Miaka mingi mbele ya hapo, Waisraeli wenye waliumwa na nyoka wenye sumu walipaswa kuangalia nyoka wa shaba ili waendelee kuishi. (Hesabu 21:9) Vilevile, wanadamu wote wanapaswa kuonyesha imani katika Mwana wa Mungu ili waokolewe kutoka katika kifo na kupata uzima wa milele. Ili kukazia daraka lenye upendo la Yehova katika jambo hilo, Yesu anafikia kuambia Nikodemo hivi: “Kwa maana, Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Yesu ameanza utumishi wake kumepita miezi sita hivi. Sasa iko katika Yerusalemu, na anaonyesha waziwazi kuwa yeye ndiye njia ya wokovu kwa ajili ya wanadamu.

Yesu anaambia Nikodemo hivi: “Mungu hakutuma Mwana wake katika ulimwengu ili ahukumu ulimwengu.” Hilo linamaanisha kuwa Yesu hakutumwa ili kuhukumu ulimwengu katika njia ya mubaya, kwa kuhukumia wanadamu wote uharibifu. Lakini, kama vile Yesu mwenyewe anasema, alitumwa “ili ulimwengu uokolewe kupitia yeye.”—Yohana 3:17.

Nikodemo alikuja kumuona Yesu usiku kwa sababu ya woga. Kwa hiyo, inapendeza kuona namna Yesu anamaliza mazungumuzo pamoja naye kwa kumuambia hivi: “Sasa huu ndio musingi wa hukumu: kwamba mwangaza [ni kusema, Yesu kupitia maisha na mafundisho yake] umekuja katika ulimwengu, lakini watu wamependa giza kuliko mwangaza, kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. Kwa maana kila mutu mwenye anazoea kutenda mambo maovu anachukia mwangaza na hakuje kwenye mwangaza, ili matendo yake yasikaripiwe. Lakini kila mutu mwenye anafanya mambo ya kweli anakuja kwenye mwangaza, ili matendo yake yafunuliwe kuwa yamefanywa kupatana na Mungu.”—Yohana 3:19-21.

Sasa ni daraka la Mufarisayo huyo na mwalimu wa Israeli, Nikodemo, kufikiri juu ya mambo yenye ametoka kusikiliza kuhusu daraka la Yesu katika kusudi la Mungu.