Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 18

Yesu Anaongezeka na Yohana Anapunguka

Yesu Anaongezeka na Yohana Anapunguka

MATAYO 4:12 MARKO 6:17-20 LUKA 3:19, 20 YOHANA 3:22–4:3

  • WANAFUNZI WA YESU WANABATIZA

  • YOHANA MUBATIZAJI ANAFUNGWA KATIKA GEREZA

Kisha kufanya Pasaka ya mwaka wa 30 wakati wetu, Yesu na wanafunzi wake wanatoka Yerusalemu. Lakini, hawarudie mara moja Galilaya, nyumbani kwao. Wanaenda katika inchi ya Yudea, kwenye wanabatiza watu wengi. Yohana Mubatizaji amekuwa akifanya kazi kama hii kumepita mwaka moja hivi, na wanafunzi wake fulani wangali pamoja naye, pengine katika bonde la Muto Yordani.

Yesu mwenyewe habatize mutu yeyote; ni wanafunzi wake ndio wanabatiza chini ya muongozo wake. Wakati huu katika utumishi wa Yesu, wote wawili, ni kusema, Yesu na Yohana wako wanafundisha Wayahudi wenye wanatubu zambi zenye walifanya kwa kuvunja agano la Sheria ya Mungu.—Matendo 19:4.

Lakini wanafunzi wa Yohana wanasikia wivu, na wananungunika juu ya Yesu kwa kuambia Yohana hivi: “Mutu [Yesu] mwenye alikuwa pamoja na wewe . . . anabatiza, na watu wote wanaenda kwake.” (Yohana 3:26) Hata hivyo, Yohana hasikie wivu. Anafurahia matokeo ya muzuri yenye Yesu anapata na anapenda wanafunzi wake pia wafurahi. Yohana anawakumbusha hivi: “Ninyi wenyewe munatoa ushahidi kwamba nilisema, ‘Mimi siko Kristo, lakini nimetumwa nimutangulie.’” Anatoa mufano ili kufasiria jambo hilo katika njia yenye wote wanaweza kuelewa. Anasema hivi: “Kila mutu mwenye kuwa na bibi-arusi ndiye bwana-arusi. Lakini wakati rafiki ya bwana-arusi anasimama na kumusikia, anafurahi sana kwa sababu ya sauti ya bwana-arusi. Basi furaha yangu imefanywa kuwa kamili.”—Yohana 3:28, 29.

Yohana, kama vile rafiki ya bwana-arusi, alifurahi miezi fulani mbele kisha kuonyesha Yesu wanafunzi wake. Wamoja walifuata Yesu na kufikia kutiwa mafuta kwa roho takatifu. Pia, Yohana anapenda wanafunzi wenye amebakia nao wamufuate Yesu. Kwa kweli, kusudi la Yohana ni kutayarisha njia kwa ajili ya utumishi wa Kristo. Yohana anaeleza hivi: “Huyo anapaswa kuendelea kuongezeka, lakini mimi lazima niendelee kupunguka.”—Yohana 3:30.

Yohana mwingine, mwenye tayari ni mwanafunzi wa Yesu, alifikia kuandika kuhusu mahali kwenye Yesu alitoka na daraka kubwa lenye iko nalo la kuokoa wanadamu. Aliandika hivi: “Ule mwenye anatoka juu, iko juu ya wengine wote. . . . Baba anapenda Mwana na ametia vitu vyote katika mukono wake. Ule mwenye anaamini Mwana iko na uzima wa milele; ule mwenye haamini Mwana hataona uzima, lakini kasirani kali ya Mungu inakaa juu yake.” (Yohana 3:31, 35, 36) Hii ni kweli ya maana sana yenye watu wanapaswa kujua!

Muda kidogo tu kisha Yohana Mubatizaji kusema kama daraka lake na kazi yake vinapaswa kupunguka, Yohana anafungwa na Mufalme Herode. Herode amechukua Herodia, bibi ya ndugu-nusu yake mwenye kuitwa Filipo, na kumuoa. Wakati Yohana anaonyesha waziwazi tendo lake la uzinifu, Herode anamufungisha katika gereza. Kisha kusikia kuwa Yohana amefungwa katika gereza, Yesu anaondoka Yudea pamoja na wanafunzi wake na ‘kuenda Galilaya.’—Matayo 4:12; Marko 1:14.