Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 19

Anafundisha Mwanamuke Musamaria

Anafundisha Mwanamuke Musamaria

YOHANA 4:3-43

  • YESU ANAFUNDISHA MWANAMUKE MUSAMARIA NA WATU WENGINE

  • IBADA YENYE MUNGU ANAKUBALI

Yesu na wanafunzi wake wako wanatoka Yudea na kuenda Galilaya. Wanasafiri kuenda upande wa kaskazini kupitia wilaya ya Samaria. Safari hiyo imewachokesha. Katikati ya muchana hivi, wanasimama karibu na muji wa Sikari ili kupumuzikia kwenye kisima chenye pengine Yakobo alichimba ao chenye alilipa feza ili wamuchimbie kumepita miaka mingi. Mupaka leo, kisima hicho kinaweza kupatikana katika muji wenye kuitwa sasa Naplouse.

Wakati Yesu anapumuzika pembeni ya kisima hicho, wanafunzi wake wanaenda katika muji wa karibu ili kuuza chakula. Kisha wao kuenda, mwanamuke Musamaria anakuja kushota maji. Yesu anamuambia hivi: “Nipatie maji nikunywe.”—Yohana 4:7.

Kwa kawaida, Wayahudi na Wasamaria hawana uhusiano wowote kati yao kwa sababu ya ubaguzi mukali. Kwa hiyo mwanamuke huyo anashangaa na kuuliza hivi: “Namna gani wewe mwenye kuwa Muyahudi, unaniomba maji ya kunywa ijapokuwa mimi ni mwanamuke Musamaria?” Yesu anamujibu hivi: “Kama ungejua zawadi ya bure yenye inatoka kwa Mungu na ni nani mwenye anakuambia, ‘Nipatie maji nikunywe,’ ungemuomba, na angekupatia maji ya uzima.” Mwanamuke huyo anamuambia, “Bwana, hauna hata mbeketi ya kushotea maji, na kisima ni kirefu. Basi, umetosha wapi hayo maji ya uzima? Je, wewe ni mukubwa kuliko babu yetu Yakobo, mwenye alitupatia kisima hiki na yeye pamoja na wana wake na wanyama wake wa kufugwa walikunywa maji ya kisima hiki?”—Yohana 4:9-12.

Yesu anamuambia hivi: “Kila mutu mwenye anakunywa maji haya atapata kiu tena. Kila mutu mwenye atakunywa maji yenye nitamupatia hatasikia kiu hata kidogo, lakini maji yenye nitamupatia yatakuwa chemchemi ya maji ndani yake, yenye kububujika ili kutoa uzima wa milele.” (Yohana 4:13, 14) Kwa kweli, hata kama Yesu ni mwenye kuchoka, iko tayari kutolea mwanamuke Musamaria maneno ya kweli yenye kuleta uzima.

Kisha mwanamuke huyo anamuambia: “Bwana, nipatie maji hayo ili nisipate kiu tena na nisiendelee kuja hapa kushota maji.” Sasa Yesu anafanya kama vile anabadilisha habari yenye walikuwa wanazungumuzia na kumuambia hivi: “Uende, uite bwana yako na mukuje hapa.” Mwanamuke huyo anamuambia hivi: “Sina bwana.” Lakini mwanamuke huyo anapaswa kuwa anashangaa kwa sababu ya mambo yenye Yesu anajua wakati anamuambia hivi: “Unasema kweli kwa kusema, ‘Sina bwana.’ Kwa maana umekuwa na wabwana tano, na mwanaume mwenye unaishi naye sasa haiko bwana yako.”—Yohana 4:15-18.

Mwanamuke huyo anaelewa waziwazi maana ya maneno ya Yesu, na kwa kushangaa, anamuambia Yesu hivi: “Bwana, ninaona kuwa wewe ni nabii.” Kisha, mwanamuke huyo anaonyesha kama vile anapendezwa na mambo ya kiroho. Namna gani? Anaongeza hivi: “Mababu zetu [Wasamaria] waliabudu kwenye mulima huu [Mulima Gerizimu, ambao uko karibu na mahali hapo], lakini ninyi [Wayahudi] munasema kama mahali kwenye watu wanapaswa kuabudia ni kule Yerusalemu.”—Yohana 4:19, 20.

Lakini, Yesu anafasiria kama nafasi ya kufanyia ibada haiko ya maana. Anasema hivi: “Saa inakuja wakati hamutaabudu Baba katika mulima huu wala kule Yerusalemu.” Kisha anamuambia hivi: “saa inakuja, na iko sasa, wakati waabudu wa kweli watamuabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anatafuta watu wa namna hiyo ili wamuabudu.”—Yohana 4:21, 23, 24.

Jambo lenye Baba anatafuta kwa waabudu wa kweli haiko nafasi kwenye wanamuabudu lakini namna yao ya kumuabudu. Mwanamuke huyo anashangaa. Anasema hivi: “Ninajua kama Masiya anakuja, mwenye kuitwa Kristo. Wakati atakuja, atatujulisha mambo yote waziwazi.”—Yohana 4:25.

Kisha Yesu anamufunulia kweli ya maana sana: “Ni mimi, ule mwenye anazungumuza na wewe.” (Yohana 4:26) Fikiria jambo hili! Ni mwanamuke fulani mwenye anakuja katikati ya muchana ili kushota maji. Lakini, Yesu anamupatia pendeleo kubwa sana. Anamuambia jambo lenye pengine hajaambia wengine waziwazi, kwamba yeye ni Masiya.

WASAMARIA WENGI WANAAMINI

Wanafunzi wa Yesu wanarudia na chakula kutoka Sikari. Wanamukuta kwenye kisima cha Yakobo nafasi kwenye walimuacha, lakini sasa iko anazungumuza na mwanamuke Musamaria. Wakati wanafunzi wanafika, mwanamuke huyo anaacha mutungi wake wa maji na anaenda katika muji.

Wakati anafika katika muji wa Sikari, mwanamuke huyo anaelezea watu mambo yenye Yesu alimuambia. Kwa uhakika wote, anawaambia hivi: “Mukuje muone mutu mwenye aliniambia mambo yote yenye nilifanya.” Kisha, pengine ili kuamusha upendezi wao, anauliza hivi: “Je, haiwezekane yeye ndiye Kristo?” (Yohana 4:29) Hilo ni ulizo juu ya habari ya maana sana, yenye watu walipenda kujua tangu wakati wa Musa. (Kumbukumbu la Torati 18:18) Hilo linafanya watu wa muji wakuje ili kumuona Yesu wao wenyewe.

Wakati huo, wanafunzi wanamuomba Yesu akule chakula chenye wameleta. Lakini anawajibu hivi: “Niko na chakula chenye hamujue.” Wanafunzi wanashangaa kusikia hivyo, na wanaambiana kati yao: “Je, kuko mutu mwenye alimuletea chakula?” Kwa upole, Yesu anawafasiria kwa kutumia maneno yenye kuwa na maana kwa wafuasi wake wote: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya ule mwenye alinituma na kumaliza kazi yake.”—Yohana 4:32-34.

Kazi yenye Yesu anazungumuzia haiko ile ya kuvuna shayiri, kwa sababu kungali miezi ine hivi ili kazi hiyo ifanywe. Lakini, Yesu anazungumuzia mavuno ya kiroho, wakati anaendelea kusema hivi: “Muinue macho yenu na muone mashamba, ni meupe kwa ajili ya kuvunwa. Tayari muvunaji anapokea malipo na anakusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili mupandaji na muvunaji wafurahi pamoja.”—Yohana 4:35, 36.

Inawezekana Yesu amekwisha kutambua matokeo ya mazungumuzo yake pamoja na mwanamuke Musamaria. Ushuhuda wa mwanamuke huyo unafanya watu wengi wa muji wa Sikari waonyeshe imani katika Yesu, kwa sababu iko anaambia watu hivi: “Aliniambia mambo yote yenye nilifanya.” (Yohana 4:39) Kwa hiyo, wakati wanatoka Sikari mupaka kwenye kisima, wanamuomba Yesu abakie pamoja nao na kuwaelezea mambo mengi zaidi. Yesu anakubali ombi lao na anabakia Samaria siku mbili.

Wakati Wasamaria wanamusikiliza Yesu, wengine wengi zaidi wanakuwa na imani katika yeye. Wanaambia mwanamuke huyo: “Hatuamini tena kwa sababu tu ya mambo yenye ulisema; kwa maana sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba mutu huyu kwa kweli ndiye mwokozi wa ulimwengu.” (Yohana 4:42) Kwa kweli, mwanamuke Musamaria anatutolea mufano muzuri juu ya namna tunaweza kutoa ushahidi kuhusu Kristo; tunapaswa kuamusha upendezi ili wasikilizaji wakuwe na hamu ya kupata habari zaidi.

Kumbuka kama kunabakia miezi ine ili mavuno ianze; inawezekana ni mavuno ya shayiri, yenye yanavunwa katika kipindi cha kuchipuka kwa majani katika eneo hilo. Sasa inawezakana ni Mwezi wa 11 ao Mwezi wa 12. Hilo linaonyesha kuwa kisha Pasaka ya mwaka wa 30 wakati wetu, Yesu na wanafunzi wake wamefanya miezi munane ao zaidi katika Yudea, wakifundisha na kubatiza watu. Sasa wanarudia nyumbani kwao kaskazini katika eneo la Galilaya. Ni nini inawangojea huko?