Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 24

Utumishi Wake Unapanuka Katika Galilaya

Utumishi Wake Unapanuka Katika Galilaya

MATAYO 4:23-25 MARKO 1:35-39 LUKA 4:42, 43

  • YESU ANAHUBIRI KATIKA GALILAYA YOTE PAMOJA NA WANAFUNZI WAKE INE

  • MAHUBIRI NA MIUJIZA YAKE VINAJULIKANA SANA

Yesu amefanya mambo mengi katika siku yenye amekuwa Kapernaumu pamoja na wanafunzi wake ine. Wakati wa mangaribi, watu wa Kapernaumu wanamuletea wagonjwa wao ili awaponyeshe. Yesu hakuwa na wakati mwingi ili kuwa peke yake.

Sasa, Yesu anaamuka asubui sana wakati kungali giza na anaenda inje peke yake. Anapata nafasi ya kuwa peke yake kwenye anaweza kusali Baba yake. Lakini wakati huo wa kuwa pekee yake uko kidogo sana. Wakati “Simoni na wale wenye walikuwa pamoja naye” wanatambua kama Yesu haiko pamoja nao, wanaenda kumutafuta. Inaonekana ni Petro ndiye anawaongoza kwa sababu Yesu alikuwa kwake.—Marko 1:36; Luka 4:38.

Wakati wanamupata Yesu, Petro anamuambia hivi: “Kila mutu anakutafuta.” (Marko 1:37) Ni wazi kuwa, watu wa Kapernaumu wanapenda Yesu abakie. Wanafurahia sana mambo yenye amewafanyia, kwa hiyo wanajaribu “kumuzuia asiende mbali nao.” (Luka 4:42) Lakini, Yesu alikuja katika dunia ili tu kuponyesha watu kimuujiza? Na kazi zake zote anapaswa kuzifanya tu katika eneo hilo? Yesu anasema nini juu ya jambo hilo?

Yesu anajibu wanafunzi wake hivi: “Tuende mahali pengine, katika miji ya karibu, ili nihubiri kule pia, kwa maana hiyo ndiyo sababu nimekuja.” Kwa kweli, Yesu anaambia hata watu wenye wanapenda abakie hivi: “Ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika miji mingine, kwa sababu nilitumwa ili kufanya vile.”—Marko 1:38; Luka 4:43.

Ndiyo, sababu kubwa yenye ilifanya Yesu akuje katika dunia ni kuhubiri juu ya Ufalme wa Mungu. Ufalme huo utatakasa jina la Baba yake na kumaliza kabisa magonjwa yote ya wanadamu. Yesu anatoa uhakikisho kama alitumwa na Mungu kwa kuponyesha watu kimuujiza. Vilevile, miaka mingi mbele ya hapo, Musa alifanya mambo ya ajabu sana ili kuonyesha kuwa alitumwa na Mungu.—Kutoka 4:1-9, 30, 31.

Kwa hiyo, Yesu anatoka Kapernaumu ili kuenda kuhubiri katika miji mingine, na wanafunzi wake ine wanaenda pamoja naye. Wanafunzi hao ine ni Petro na Andrea, na pia Yohana na ndugu yake Yakobo. Juma moja mbele ya hapo, Yesu aliwaalika ili wakuwe wafanyakazi wenzake wenye kusafiri.

Kazi ya Yesu ya kuhubiri katika Galilaya pamoja na wanafunzi wake ine inapata matokeo ya ajabu! Kwa kweli, habari juu ya Yesu inafika mupaka maeneo ya mbali sana. “Habari juu yake ikaenea katika Siria yote,” katika eneo la miji kumi lenye kuitwa Dekapoli, na mupaka upande mwingine wa Muto Yordani. (Matayo 4:24, 25) Watu wengi sana kutoka maeneo hayo, na pia katika Yudea, wanamufuata Yesu na wanafunzi wake. Wengi wanamuletea wagonjwa. Yesu hawavunje moyo; anaponyesha wagonjwa na anafukuza roho waovu kwa wale wenye waliingiwa na pepo wachafu.