Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 26

“Zambi Zako Zimesamehewa”

“Zambi Zako Zimesamehewa”

MATAYO 9:1-8 MARKO 2:1-12 LUKA 5:17-26

  • YESU ANASAMEHE ZAMBI ZA MUTU MWENYE KUPOOZA NA ANAMUPONYESHA

Sasa, watu wa maeneo mbalimbali wamepata habari juu ya Yesu. Watu wengi wanasafiri na kuenda maeneo ya mbali ili kusikia mafundisho yake na kuona kazi zake za ajabu. Lakini, kisha siku fulani anarudia katika Kapernaumu, nafasi kwenye atafanya utumishi mukubwa zaidi. Habari juu ya kurudia kwake inajulikana haraka katika muji huo wote wenye kuwa pembeni ya Bahari ya Galilaya. Kwa hiyo, watu wengi wanakuja nyumbani kwenye Yesu iko. Wamoja kati yao ni Wafarisayo na walimu wa Sheria wenye wametoka Galilaya na Yudea, na pia Yerusalemu.

‘Na watu wengi sana wanakusanyika mupaka hapako nafasi tena, hata kwenye mulango, na anaanza kuwaambia lile neno.’ (Marko 2:2) Sasa hali iko muzuri kwa ajili ya tukio la maana sana. Hili ni tukio lenye linaweza kutusaidia kujua kama Yesu iko na uwezo wa kuondoa kile kinaletea wanadamu mateso na kurudishia wote wenye anachagua afya ya muzuri.

Wakati Yesu iko anafundisha katika chumba chenye kujaa watu wengi, wanaume ine wanakuja na mwanaume mwenye kupooza juu ya kitanda. Wanapenda Yesu aponyeshe rafiki yao. Lakini, kwa sababu ya watu wengi, wanashindwa “kumupeleka moja kwa moja kwenye Yesu alikuwa.” (Marko 2:4) Wanavunjika moyo sana. Wanapanda juu ya sehemu ya juu ya nyumba na kutoboa tundu. Kisha wanateremusha kitanda chenye kuwa na mwanaume huyo mwenye kupooza ndani ya nyumba.

Je, Yesu anakasirika kwa sababu wanamukatiza mazungumuzo? Hapana, kabisa! Anashangazwa sana na imani yao na anaambia mwanaume huyo mwenye kupooza hivi: “Zambi zako zimesamehewa.” (Matayo 9:2) Lakini, Yesu anaweza kabisa kusamehe zambi? Waandishi na Wafarisayo wanapinga maneno yake, na wanaambiana hivi: “Sababu gani mutu huyu anasema namna hii? Anamutukana Mungu. Ni nani anaweza kusamehe zambi isipokuwa mumoja tu, Mungu?”—Marko 2:7.

Yesu anatambua mawazo yao, na kuwaambia hivi: “Sababu gani munawaza mambo haya katika mioyo yenu? Ni jambo gani lenye kuwa mwepesi zaidi, kumuambia mutu mwenye kupooza, ‘Zambi zako zimesamehewa,’ ao kusema, ‘Simama, kamata kitanda chako na utembee’?” (Marko 2:8, 9) Ndiyo, kwa musingi wa zabihu ya ukombozi yenye Yesu atafikia kutoa, anaweza kusamehe zambi za mwanaume huyo.

Kisha, Yesu anaambia watu, kutia ndani maadui wake, kama iko na mamlaka ya kusamehe zambi katika dunia. Anaangalia mutu mwenye kupooza na kumuambia hivi: “Ninakuambia, simama, kamata kitanda chako, na uende nyumbani kwako.” Na mara moja mwanaume huyo anafanya hivyo, anasimama na kukamata kitanda chake mbele ya watu wote wenye kuwa katika chumba. Watu wanashangaa! Wanamusifu Mungu na kusema: “Hatujaona hata siku moja jambo kama hili”!—Marko 2:11, 12.

Ni wazi kuwa Yesu anaonyesha kwamba kuko uhusiano kati ya zambi na ugonjwa na kwamba kuko uhusiano kati ya kusamehewa zambi na kuwa na afya ya muzuri. Biblia inafundisha kama muzazi wetu wa kwanza, Adamu, alifanya zambi na kama sisi wote tumeriti matokeo ya mubaya ya zambi, ni kusema, magonjwa na kifo. Lakini chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu, Yesu atasamehe zambi za wote wenye kumupenda Mungu na kumutumikia. Magonjwa yataondolewa milele.—Waroma 5:12, 18, 19.