Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 27

Matayo Anaalikwa

Matayo Anaalikwa

MATAYO 9:9-13 MARKO 2:13-17 LUKA 5:27-32

  • YESU ANAALIKA MATAYO, MUKUSANYA-KODI

  • KRISTO ANAPITISHA WAKATI PAMOJA NA WATENDA-ZAMBI ILI KUWASAIDIA

Muda kidogo kisha kuponyesha mutu mwenye kupooza, Yesu anabakia katika eneo la Kapernaumu pembeni ya bahari ya Galilaya. Tena, watu wengi sana wanamufuata, na anaanza kuwafundisha. Wakati iko anapita pembeni ya biro ya kodi, anaona Matayo, mwenye kuitwa pia Lawi, anakaa kwenye biro ya kodi. Yesu anamutolea mwaliko muzuri sana: “Kuwa mufuasi wangu.”—Matayo 9:9.

Kama vile ilikuwa kwa Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana, inawezekana Matayo pia anajua kwa kiasi fulani mafundisho ya Yesu na miujiza yenye amefanya katika eneo hilo. Kama wao, Matayo anakubali mwaliko bila kukawia. Matayo anazungumuzia jambo hilo katika kitabu chake cha Injili, kwa kusema: “Akasimama [Matayo mwenyewe] mara moja na kumufuata” Yesu. (Matayo 9:9) Kwa hiyo, Matayo anaacha daraka lake la mukusanya-kodi na anakuwa mwanafunzi wa Yesu.

Wakati fulani kisha, pengine ili kuonyesha shukrani yake kwa mwaliko wa pekee wenye Yesu amemutolea, Matayo anafanya karamu kubwa katika nyumba yake. Zaidi ya kualika Yesu na wanafunzi wake, anaalika watu gani wengine? Watu fulani kati ya wale wenye Matayo alitumika nao zamani, ni kusema, wakusanya-kodi wengine. Wanakusanya kodi mbalimbali kwa ajili ya wakubwa wa serikali ya Roma wenye watu wanachukia. Kwa ujumla, namna gani Wayahudi wanaona wakusanya-kodi? Watu wanawazarau kwa sababu mara nyingi wanaomba feza nyingi zaidi kuliko vile kodi inapaswa kulipwa. Kwenye karamu hiyo, kuko pia ‘watenda-zambi,’ watu wenye kujulikana kuwa wanafanya mambo ya mubaya.—Luka 7:37-39.

Wakati wanamuona Yesu kwenye karamu pamoja na watu hao, Wafarisayo wenye wanajiona kuwa wanafanya mambo yenye kuwa sawa wanauliza wanafunzi wake hivi: “Sababu gani mwalimu wenu anakula pamoja na wakusanya-kodi na watenda-zambi?” (Matayo 9:11) Yesu anawasikia, na kuwajibu: “Watu wenye afya ya muzuri hawana lazima ya munganga, lakini wagonjwa ndio wako na lazima yake. Muende basi, mujifunze maana ya maneno haya: ‘Ninataka rehema, hapana zabihu.’ Kwa maana sikukuja kuita watu wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa, lakini nilikuja kuita watenda-zambi.” (Matayo 9:12, 13; Hosea 6:6) Wafarisayo hawatumie neno “mwalimu” kutoka moyoni wakati wanamuzungumuzia Yesu, lakini Yesu anaweza kuwafundisha jambo fulani juu ya mambo yenye kuwa sawa.

Inaonekana, Matayo amealika wakusanya-kodi na watenda-zambi ili wamusikilize Yesu na kuponyeshwa kiroho, “kwa maana wengi wao walikuwa wanamufuata.” (Marko 2:15) Yesu anapenda kuwasaidia wakuwe na uhusiano wa muzuri pamoja na Mungu. Tofauti na Wafarisayo wenye kujiona kuwa wanafanya mambo yenye kuwa sawa, Yesu yeye hazarau watu kama hao. Anachochewa na huruma na rehema; anaweza kuwa munganga wa kiroho kwa wale wote wenye kugonjwa kiroho.

Yesu anaonyesha rehema wakusanya-kodi na watenda-zambi, haiko ili kufunga macho juu ya zambi zao, lakini ili kuwaonyesha huruma kama vile anaonyesha huruma wale wenye kugonjwa kimwili. Kwa mufano, kumbuka wakati aligusa kwa huruma mutu mwenye ukoma, na kusema hivi: “Ninataka! Kuwa safi.” (Matayo 8:3) Sisi pia, tunapaswa kukomalisha sifa kama hiyo ya rehema na kusaidia wale wenye kuwa na lazima ya musaada, zaidi sana kwa kuwatolea musaada wa kiroho.