Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 39

Ole kwa Kizazi Chenye Kukataa Kusikiliza

Ole kwa Kizazi Chenye Kukataa Kusikiliza

MATAYO 11:16-30 LUKA 7:31-35

  • YESU ANAKEMEA WATU WA MIJI FULANI

  • ANATOA KITULIZO NA PUMUZIKO

Yesu anamuona Yohana Mubatizaji kuwa mutu wa maana sana, lakini watu wengi wanamuona Yohana namna gani? Yesu anasema hivi: “Kizazi hiki . . . ni kama watoto wadogo wenye kukaa katika masoko na kuita wachezaji wenzao wakisema: ‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamukucheza; tuliomboleza, lakini hamukujipiga-piga kwa huzuni.’”—Matayo 11:16, 17.

Yesu anapenda kusema nini? Anafasiria waziwazi maneno yake. Anasema hivi: “Wakati Yohana alikuja hakukuwa anakula na hakukuwa anakunywa, lakini watu wanasema, ‘Iko na pepo muchafu.’ Wakati Mwana wa binadamu alikuja alikuwa anakula na kunywa, lakini watu wanasema, ‘Angalia, mutu mulafi na mwenye anazoea kunywa divai, rafiki ya wakusanya-kodi na watenda-zambi.’” (Matayo 11:18, 19) Kwa upande moja, Yohana aliishi maisha mepesi kama Munaziri, hata kama hakukuwa anakunywa divai, lakini kizazi hiki kinasema kuwa iko na pepo muchafu. (Hesabu 6:2, 3; Luka 1:15) Kwa upande mwingine, Yesu anaishi kama watu wengine. Anakula na kunywa kwa usawaziko, lakini anashitakiwa kuwa ni mulafi na mwenye anazoea kunywa divai. Inaonekana kuwa haiwezekane kufurahisha watu hao.

Yesu analinganisha kizazi hiki na watoto wadogo wenye kukaa katika masoko wenye wanakataa kucheza wakati watoto wenzao wanawapigia filimbi ao wanakataa kujipiga-piga kwa huzuni wakati wengine wanaomboleza. Yesu anasema hivi: “Vilevile, hekima inaonekana kuwa yenye kufanya mambo yenye kuwa sawa kupitia kazi zake.” (Matayo 11:16, 19) Ndiyo, “kazi” hizo, ni kusema, ushuhuda wenye Yohana na Yesu walitoa, unaonyesha wazi kuwa mashitaka yenye yalifanywa juu yao ni ya uongo.

Kisha kuzungumuzia kizazi hicho kuwa ni kizazi chenye kukataa kusikiliza, Yesu anakemea muji wa Korazini, wa Betsaida, na wa Kapernaumu, kwenye amefanya miujiza. Yesu anasema kama ikiwa angefanya miujiza hiyo katika miji ya Wafoinike ya Tiro na Sidoni, watu wa miji hiyo wangepaswa kutubu. Anataja pia Kapernaumu, muji wenye ulikuwa makao yake makubwa kwa wakati fulani. Hata katika muji huo, watu wengi hawakusikiliza. Yesu anasema hivi juu ya muji huo: “Itakuwa mwepesi zaidi kwa inchi ya Sodoma katika Siku ya Hukumu kuliko kwako.”—Matayo 11:24.

Kisha Yesu anamusifu Baba yake, mwenye anaficha “watu wenye hekima na wenye elimu” kweli za maana za kiroho lakini anafunua kweli hizo kwa watu wa hali ya chini, wenye wako kama watoto wadogo. (Matayo 11:25) Yesu anatolea watu kama hao mwaliko huu muzuri: “Mukuje kwangu, ninyi wote wenye kuteseka na wenye kubeba mizigo mizito, na mimi nitawapumuzisha. Mubebe nira yangu na mujifunze kupitia mimi, kwa maana mimi ni mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo, na mutapata pumuziko kwa ajili yenu. Kwa maana nira yangu haiko yenye kuumiza, na muzigo wangu ni mwepesi.”—Matayo 11:28-30.

Yesu anatoa pumuziko namna gani? Watu wamelemewa na mafundisho yenye Viongozi wa dini wanawatwika kama mizigo, kama vile sheria juu ya Sabato zenye kuvuka mipaka. Lakini Yesu anawaletea pumuziko kwa kuwafundisha kweli juu ya Mungu, kweli yenye haichafuliwe na mafundisho ya viongozi hao wa dini. Pia anapatia pumuziko wale wenye wanajisikia kuwa wamepondwa na wakubwa wa politike na wale wenye wamelemewa na zambi. Ndiyo, Yesu anawaonyesha namna zambi zao zinaweza kusamehewa na namna wanaweza kuishi katika amani pamoja na Mungu.

Wale wote wenye wanabeba nira laini ya Yesu wanaweza kujitoa wenyewe kwa Mungu na kutumikia Baba yetu wa mbinguni, mwenye huruma na rehema. Kufanya hivyo haiko muzigo muzito, kwa sababu mambo yenye Mungu anatuomba haiko mizigo mizito hata kidogo.—1 Yohana 5:3.