Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 43

Mifano Mbalimbali Kuhusu Ufalme

Mifano Mbalimbali Kuhusu Ufalme

MATAYO 13:1-53 MARKO 4:1-34 LUKA 8:4-18

  • YESU ANATOA MIFANO KUHUSU UFALME

Inawezekana Yesu iko katika Kapernaumu wakati anakemea Wafarisayo. Mangaribi ya siku hiyo, anatoka nyumbani na kuenda kwenye bahari ya karibu, ni kusema, Bahari ya Galilaya; mahali kwenye watu wengi sana wanakusanyika. Yesu anapanda katika mashua, anaenda mbali kidogo na inchi kavu, na anaanza kufundisha watu hao kuhusu Ufalme wa mbinguni. Anafanya hivyo kupitia mifano mbalimbali. Wasikilizaji wake wanajua hali nyingi ao mambo yenye Yesu anataja, na hilo linawasaidia kuelewa bila tatizo mambo mbalimbali kuhusu Ufalme.

Kwanza, Yesu anazungumuzia mupandaji mwenye iko anapanda mbegu. Mbegu fulani zinaanguka pembeni ya barabara na ndege wanazikula. Mbegu zingine zinaanguka mahali penye miamba kwenye hakuna udongo mwingi. Mizizi haiwezi kuenda mbali sana, na kisha mimea yenye iliota inaungua kwa sababu ya jua na inakauka. Lakini mbegu zingine zinaanguka katikati ya miiba, na miiba hiyo inafinya mimea wakati inaota. Mwishowe, mbegu fulani zinaanguka kwenye udongo muzuri. Mbegu hizo zinazaa matunda, “hii mara mia moja (100) zaidi, ile mara makumi sita (60), na ile nyingine mara makumi tatu (30).”—Matayo 13:8.

Katika mufano mwingine, Yesu analinganisha Ufalme na wakati mwanaume mumoja anapanda mbegu. Katika hali hii, ikuwe mwanaume ni mwenye kulala ao iko macho, mbegu zinaota. Lakini “yeye hajue” zilifanya hivyo namna gani. (Marko 4:27) Mbegu hizo zinaota na kukomaa peke yazo na kuzaa matunda, yenye anaweza kuvuna.

Kisha anatoa mufano wa tatu wenye unahusu kazi ya kupanda. Mwanaume anapanda mbegu ya muzuri, lakini “wakati watu walikuwa wamelala usingizi,” adui akakuja na kupanda magugu katikati ya ngano. Watumwa wa mwanaume huyo wanamuuliza ikiwa wanapaswa kuenda kuongoa magugu hayo. Anawajibu hivi: “Hapana, ili, wakati munakusanya magugu, musingoe ngano pia. Muache zote zikomae pamoja mupaka wakati wa mavuno, na katika kipindi cha mavuno nitaambia wavunaji: Mukusanye magugu kwanza na kuyafunga mafungu-mafungu ili kuyachoma; kisha mukusanye ngano na kuitia katika depo yangu.”—Matayo 13:24-30.

Watu wengi wenye wako wanamusikiliza Yesu wanajua muzuri kazi ya mashamba. Anataja pia kitu kingine chenye kinajulikana sana, mbegu ya haradali. Mbegu hiyo inakuwa muti mukubwa zaidi hivi kwamba ndege wanaweza kuishi katika matawi yake. Kuhusu mbegu hiyo, Yesu anasema hivi: “Ufalme wa mbinguni ni kama mbegu ya haradali, yenye mutu alikamata na kupanda katika shamba lake.” (Matayo 13:31) Lakini, Yesu haiko anafundisha watu juu ya mimea. Iko anaonyesha namna kitu fulani kinaweza kukomaa katika njia yenye kushangaza, namna kitu kidogo sana kinaweza kukomaa ao kufikia kuwa kitu fulani kikubwa sana.

Kisha, Yesu anazungumuzia jambo fulani lenye watu wengi kati ya wasikilizaji wake wanajua. Analinganisha Ufalme wa mbinguni na “chachu yenye mwanamuke alikamata na kuichanga na vipimo vikubwa vitatu (3) vya unga.” (Matayo 13:33) Hata kama chachu hiyo haiwezi kuonekana, lakini, inaenea katika tonge lote na kufanya tonge hilo livimbe. Inavimbisha sana tonge na kuleta mabadiliko yenye mwanzoni hayaonekane.

Kisha kutoa mifano hiyo, Yesu anaacha watu waende na anarudia nyumbani kwenye alikuwa anaishi. Bila kukawia, wanafunzi wake wanakuja kumuona, wanapenda kuelewa maana ya mifano yenye alikuwa anatoa.

WANAFAIDIKA NA MIFANO YA YESU

Wanafunzi wamekwisha kumusikia Yesu anatumia mifano, lakini haiko mifano mingi sana hivi. Wanamuuliza: “Sababu gani unasema nao kwa kutumia mifano?”—Matayo 13:10.

Sababu moja yenye inamuchochea afanye hivyo ni juu ya kutimiza unabii wa Biblia. Injili ya Matayo inasema hivi: “Hakuwa anasema nao bila mufano, ili kutimiza neno lenye lilisemwa kupitia nabii, mwenye alisema: ‘Nitafungua kinywa changu kwa mifano; nitatangaza mambo yenye yalifichwa tangu kuwekwa musingi.’”—Matayo 13:34, 35; Zaburi 78:2.

Lakini kuko sababu ingine yenye inafanya Yesu atumie mifano. Mifano inasaidia kufunua mawazo ya watu. Wengi kati ya watu hao wanapendezwa na Yesu kwa sababu wanamuona tu kuwa musimuliaji fulani wa hadisi mwenye uzoefu na mutu mwenye kufanya miujiza. Hawamuone kama vile Bwana mwenye watu wanapaswa kutii na kufuata kwa moyo wao wote. (Luka 6:46, 47) Hawapendi kubadilisha mawazo ao tabia yao. Hawapendi ujumbe uguse kabisa mioyo yao.

Yesu anajibia ulizo la wanafunzi wake kwa kusema hivi: “Ndiyo sababu ninasema nao kwa kutumia mifano; kwa sababu wanaangalia, lakini hawaone, na wanasikiliza lakini hawasikie, na hawaelewe maana. Na unabii wa Isaya unatimia kwao wenye unasema: ‘. . . Moyo wa watu hawa umekuwa mugumu.’”—Matayo 13:13-15; Isaya 6:9, 10.

Lakini, hilo halihusu wote wenye wako wanamusikiliza Yesu. Anaeleza hivi: “Yenye furaha ni macho yenu kwa sababu yanaona na masikio yenu kwa sababu yanasikia. Kwa maana, kwa kweli ninawaambia ninyi, manabii wengi na watu wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa walitamani kuona mambo yenye munaona lakini hawakuyaona, na kusikia mambo yenye munasikia lakini hawakuyasikia.”—Matayo 13:16, 17.

Ndiyo, mitume 12 na wanafunzi wengine washikamanifu hawako na mioyo migumu. Kwa hiyo, Yesu anasema hivi: “Ninyi mumepewa uwezo wa kuelewa siri takatifu za Ufalme wa mbinguni, lakini wao hawakupewa uwezo huo.” (Matayo 13:11) Kwa sababu wanapenda kwa moyo wao wote kuelewa, Yesu anafasiria wanafunzi wake mufano wa mupandaji.

Yesu anawaambia hivi: “Mbegu ni neno la Mungu.” (Luka 8:11) Na udongo ni moyo wa mutu. Hiyo ndio siri ya kuelewa mufano wake.

Juu ya mbegu yenye ilipandwa pembeni ya barabara, Yesu anafasiria hivi: “Ibilisi anakuja na kuondoa lile neno katika mioyo yao ili wasiamini na wasiokolewe.” (Luka 8:12) Wakati anazungumuzia mbegu yenye ilipandwa kwenye miamba, Yesu anamaanisha mioyo ya watu wenye wanapokea neno kwa furaha lakini neno hilo halina mizizi ndani ya mioyo yao. “Kisha taabu ao mateso kutokea kwa sababu ya lile neno,” wanakwazika. Ndiyo, ikiwa “wakati wa jaribu” unatokea, pengine ni upinzani kutoka kwa watu wa familia ao watu wengine, wanaanguka.—Matayo 13:21; Luka 8:13.

Halafu mbegu yenye inaanguka katikati ya miiba? Yesu anaambia wanafunzi wake kuwa watu hao, ni wale wenye wamesikia neno. Lakini, wanashindwa na “mahangaiko ya mupangilio huu wa mambo na nguvu za udanganyifu wa utajiri.” (Matayo 13:22) Walikuwa na neno katika moyo wao, lakini sasa neno hilo linasongwa na linakosa kuzaa matunda.

Aina ya mwisho ya udongo yenye Yesu anaeleza ni udongo muzuri. Hao, ni wale wenye wanasikia neno na kulikubali katika moyo wao, kwa kuelewa kabisa maana ya neno hilo. Na matokeo ni gani? ‘Wanazaa matunda.’ Kwa sababu ya hali zao, kama vile uzee ao afya, wote hawawezi kufanya sawasawa; mumoja anazaa mara 100 zaidi, mwingine mara 60 zaidi, na mwingine mara 30 zaidi. Ndiyo, baraka za kumutumikia Mungu zinakuja kwa “watu wenye, kisha kusikia neno kwa moyo muzuri na mwema, wanalichunga na kuzaa matunda kwa uvumilivu.”—Luka 8:15.

Maneno haya yanapaswa kushangaza zaidi sana wanafunzi hao wenye wamemutafuta Yesu ili awafasirie mafundisho yake! Sasa wanaelewa mifano hiyo muzuri zaidi. Yesu anapenda wanafunzi wake waelewe mifano yake ili wao pia waweze kufundisha wengine kweli. Anauliza hivi: “Watu hawalete taa ili kuiweka chini ya kitunga ao chini ya kitanda, haiko vile? Je, hawailete ili kuiweka juu ya kinara cha taa?” Kwa hiyo, Yesu anatoa shauri hili: “Kila mutu mwenye kuwa na masikio ya kusikiliza, asikilize.”—Marko 4:21-23.

WANABARIKIWA NA MAFUNDISHO MENGI ZAIDI

Kisha kupokea mafasirio ya Yesu kuhusu mufano wa mupandaji, wanafunzi wanapenda kujua mengi zaidi. Wanamuomba: “Tuelezee maana ya ule mufano wa magugu katika shamba.”—Matayo 13:36.

Wakati wanaomba jambo hilo, wanaonyesha kuwa wako tofauti na watu wengine wenye walikuwa kwenye bahari. Ni wazi kuwa, watu hao wako wanasikia lakini hawana tamaa ya kujua maana ya mifano hiyo na matumizi yayo. Wanafurahia tu mafundisho ya juu-juu yenye kutolewa katika mifano hiyo. Yesu anaonyesha tofauti kati ya watu hao wenye walikuwa wanamusikiliza pembeni ya bahari na wanafunzi wake wenye kupenda kujua ambao wamekuja kwake ili awafundishe mambo mengi zaidi, kwa kusema:

“Mukuwe waangalifu juu ya mambo yenye munasikia. Kwa kipimo chenye munapimia, ninyi pia mutapimiwa, ndiyo, mutaongezewa mengi zaidi.” (Marko 4:24) Wanafunzi wako wanakazia uangalifu mambo yenye Yesu iko anawaambia. Wako wanamupimia kipimo, ni kusema, wanapendezwa sana na mafundisho yake na kumusikiliza kwa uangalifu, na wanabarikiwa na mafundisho mengi zaidi, na mafasirio zaidi. Kwa hiyo, ili kujibia ulizo la wanafunzi wake kuhusu mufano wa ngano na magugu, Yesu anaeleza hivi:

“Mupandaji wa mbegu ya muzuri ni Mwana wa binadamu; shamba ni ulimwengu. Na mbegu ya muzuri, ni wana wa Ufalme, lakini magugu ni wana wa ule muovu, na adui mwenye alipanda magugu ni Ibilisi. Mavuno ni umalizio wa mupangilio wa mambo, na wavunaji ni malaika.”—Matayo 13:37-39.

Kisha kuzungumuzia kila sehemu ya mufano wake, Yesu anaonyesha matokeo. Anasema kuwa katika umalizio wa mupangilio wa mambo, wavunaji, ao malaika, watatenganisha Wakristo wa uongo wenye kufananishwa na magugu na “wana [wa kweli] wa Ufalme.” “Wale wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa” watakusanywa na watafikia kungaa “katika Ufalme wa Baba yao.” Na ni nini itafikia “wana wa ule muovu”? Watu hao wataharibiwa, ndiyo sababu “watalia na kusaga meno yao.”—Matayo 13:41-43.

Kisha Yesu anabariki wanafunzi wake kwa kuwatolea mifano ingine tatu. Kwanza, anasema hivi: “Ufalme wa mbinguni ni kama hazina yenye ilifichwa katika shamba, yenye mutu fulani aliona na kuficha tena; na kwa sababu ya furaha yake, akaenda na kuuzisha vitu vyake vyote na kununua shamba hilo.”—Matayo 13:44.

Anaendelea kwa kusema hivi: “Ufalme wa mbinguni ni kama mufanyabiashara musafiri mwenye kutafuta lulu ya muzuri. Wakati aliona lulu moja yenye samani kubwa, alienda na mara moja akauzisha vitu vyake vyote na kuinunua.”—Matayo 13:45, 46.

Katika mifano yote mbili, Yesu anakazia wazo la kuwa mutu iko tayari kujitoa kwa ajili ya mambo ya maana kabisa. Mufanyabiashara huyo anauzisha “vitu vyake vyote” ili apate lulu moja yenye samani kubwa. Wanafunzi wa Yesu wanaweza kuelewa mufano huo kuhusu lulu yenye samani kubwa. Na mwanaume mwenye anapata hazina yenye kufichwa katika shamba ‘anauzisha vitu vyake vyote’ ili kupata shamba hilo. Katika hali zote mbili, kitu fulani cha maana sana kinapatikana, kitu chenye mutu anapaswa kupata na kuchunga muzuri. Hilo linaweza kulinganishwa na nguvu zenye mutu anafanya ili kutimiza uhitaji wake wa kiroho. (Matayo 5:3) Watu fulani kati ya wale wenye kumusikiliza Yesu wamekwisha kuonyesha kuwa wako tayari kujikaza sana ili kutimiza mahitaji yao ya kiroho na kuwa wafuasi wake wa kweli.—Matayo 4:19, 20; 19:27.

Mwishowe, Yesu analinganisha Ufalme wa mbinguni na wavu wenye unakusanya samaki wa kila namna. (Matayo 13:47) Wakati samaki wanatenganishwa, samaki wazuri wanawekwa katika vyombo lakini wale wenye hawafae wanatupwa. Yesu anasema kama itakuwa hivyo katika umalizio wa mupangilio wa mambo; malaika watatenganisha waovu kutoka kati ya watu wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa.

Yesu mwenyewe alikuwa anafanya aina fulani ya uvuvi wa kiroho wakati alialika wanafunzi wake wa kwanza ili wakuwe “wavuvi wa watu.” (Marko 1:17) Lakini, anasema kuwa mufano wake kuhusu wavu utatimia wakati wenye kuja, “katika umalizio wa mupangilio wa mambo.” (Matayo 13:49) Kwa hiyo, mitume na wanafunzi wengine wenye kumusikiliza Yesu wanaelewa kuwa mambo yenye kupendeza sana yangali yatakuja.

Wale walisikia mifano yenye Yesu alitoa wakati alikuwa katika mashua walipata utajiri mwingi wa kiroho. Yesu anaonyesha kuwa iko tayari ‘kufasiria wanafunzi wake mambo yote wakati wako peke yao.’ (Marko 4:34) Iko “kama mutu fulani, bwana wa nyumba, mwenye anatosha katika depo yake ya hazina vitu vipya na vya zamani.” (Matayo 13:52) Wakati Yesu anatoa mifano hiyo, haiko juu ya kuonyesha kuwa iko na uzoefu wa kufundisha. Lakini, iko anatolea wanafunzi wake mafundisho ya kweli yenye kuwa kama hazina yenye samani kubwa. Kwa kweli, Yesu ni “mufundishaji wa watu wote” mukubwa zaidi.