Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 50

Wanatayarishwa Kuhubiri Hata Katika Mateso

Wanatayarishwa Kuhubiri Hata Katika Mateso

MATAYO 10:16–11:1 MARKO 6:12, 13 LUKA 9:6

  • YESU ANAZOEZA NA KUTUMA MITUME WAKE

Yesu anatolea mitume wake maagizo ya muzuri juu ya namna ya kufanya kazi ya kuhubiri wakati wanaenda wawili-wawili. Lakini anafanya zaidi ya hilo. Kwa upendo anawaonya juu ya wapinzani: “Muangalie! Ninawatuma ninyi kama kondoo katikati ya imbwa wa pori . . . Mufanye angalisho na watu, kwa maana watawapeleka ninyi kwenye tribinali ndogo na kuwapiga mijeledi katika masinagogi yao. Na mutapelekwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu.”—Matayo 10:16-18.

Ndiyo, wafuasi wa Yesu wanaweza kukutana na upinzani mukali, lakini anawatia moyo kwa kuwatolea ahadi hii: “Wakati watawapeleka, musihangaike juu ya mambo yenye mutasema ao namna mutayasema, kwa sababu mutapewa mambo ya kusema saa hiyo; kwa maana wenye kusema haiko ninyi tu, lakini ni roho ya Baba yenu ndiyo inasema kupitia ninyi.” Yesu anaongeza hivi: “Ndugu atamutoa ndugu yake ili auawe, na baba atamutoa mutoto wake, na watoto wataasi wazazi na kufanya wauawe. Na mutachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu, lakini ule mwenye atavumilia mupaka mwisho ataokolewa.”—Matayo 10:19-22.

Kwa sababu kazi ya kuhubiri ni ya maana sana, Yesu anakazia kuwa ni jambo la lazima wanafunzi wake wakuwe wenye busara ili waendelee kuwa na uhuru wa kufanya kazi hiyo. Anasema hivi: “Wakati wanawatesa katika muji mumoja, mukimbilie katika muji mwingine; kwa maana kwa kweli ninawaambia ninyi, hamutamaliza kuzunguka miji ya Israeli mupaka Mwana wa binadamu afike.”—Matayo 10:23.

Kwa kweli, maagizo hayo, maonyo, na vitia-moyo vyenye Yesu alitolea mitume wake 12 vilikuwa vya muzuri sana! Lakini inapendeza kujua kama maneno yenye Yesu alisema yanahusu pia wale wote wenye watafanya kazi hiyo kisha yeye kufa na kufuliwa. Hilo linaonekana wazi katika maneno yenye kusema kama “watu wote watawachukia” wanafunzi wake; hawatachukiwa tu na watu wenye mitume wako wanaenda kuhubiria. Zaidi ya hilo, Biblia haionyeshe kama mitume walipelekwa kwa magavana na kwa wafalme katika muda huo mufupi wenye walihubiri katika Galilaya ao kutolewa ili wauawe na watu wa familia.

Ni wazi kwamba Yesu anafikiria wakati wenye kuja wakati anaambia mitume wake mambo hayo. Fikiria maneno yake yenye kusema kama wanafunzi wake hawatakuwa wamemaliza muzunguko wao wa kuhubiri “wakati Mwana wa binadamu atafika.” Yesu iko anaonyesha kama wanafunzi wake hawatamaliza kuhubiri juu ya Ufalme wa Mungu mbele Mufalme Yesu Kristo mwenye utukufu afike kama muamuzi mwenye amewekwa na Mungu.

Wakati wanafanya kazi ya kuhubiri, mitume hawapaswe kushangaa wakati wanapata upinzani, kwa sababu Yesu anasema hivi: “Mwanafunzi hamupite mwalimu wake, wala mutumwa hamupite bwana wake.” Maneno ya Yesu yako wazi. Anatendewa mubaya na kuteswa kwa sababu ya kuhubiri Ufalme wa Mungu, wao pia watakutana na mambo hayo. Hata hivyo, Yesu anawaambia hivi: “Musiogope wale wenye wanaua mwili lakini hawawezi kuua nafsi; lakini, muogope ule mwenye anaweza kuharibu vyote viwili, nafsi na mwili katika Gehena.”—Matayo 10:24, 28.

Katika jambo hili, Yesu ni mufano kwetu. Bila kuogopa, alivumilia kifo kuliko kuvunja ushikamanifu wake kwa ule mwenye kuwa na nguvu zote, ni kusema, Yehova. Ni Mungu Mweza-Yote ndiye iko na uwezo wa kuua “nafsi” ya mutu (tumaini la mutu kwa ajili ya uzima) ao kumufufua ili afurahie uzima wa milele. Kwa kweli maneno hayo yalipaswa kutia nguvu mitume wake!

Yesu anaonyesha kuwa Mungu anahangaikia kwa upendo wanafunzi wake kwa kutumia mufano huu: “Ndege shomoro wawili (2) wanauzishwa kwa feza moja ya kichele ya samani kidogo, haiko vile? Lakini hakuna hata mumoja wao mwenye ataanguka chini bila Baba yenu kujua. . . . Basi musiogope; ninyi ni wa maana kuliko ndege shomoro wengi.”—Matayo 10:29, 31.

Ujumbe wa Yesu utagawanya watu wa familia, ni kusema, watu fulani wa familia watakubali ujumbe huo na wengine wataukataa. Yesu anaeleza hivi: “Musiwaze nilikuja kuleta amani katika dunia.” Ndiyo, ili mutu wa familia akubali kweli ya Biblia, inamuomba ujasiri. Yesu anasema hivi: “Kila mutu mwenye anamupenda baba ao mama kuliko mimi hanistahili; na kila mutu mwenye anamupenda mwana ao binti kuliko mimi hanistahili.”—Matayo 10:34, 37.

Hata hivyo, watu fulani watapokea wanafunzi wake muzuri. Anasema hivi: “Kila mutu mwenye anamupatia mumoja wa hawa wadogo kikombe tu cha maji ya baridi ya kunywa kwa sababu ni mwanafunzi wangu, kwa kweli ninawaambia ninyi, hatapoteza zawabu yake.”—Matayo 10:42.

Kisha kupata maagizo hayo ya Yesu, maonyo, na vitia-moyo, mitume wanaenda “katika eneo lote kutoka kijiji mupaka kijiji, wakitangaza habari njema na kuponyesha watu kila mahali.”—Luka 9:6.