Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 53

Mutawala Mwenye Kuwa na Mamlaka Juu ya Nguvu za Asili

Mutawala Mwenye Kuwa na Mamlaka Juu ya Nguvu za Asili

MATAYO 14:22-36 MARKO 6:45-56 YOHANA 6:14-25

  • WATU WANAPENDA KUMUFANYA YESU KUWA MUFALME

  • YESU ANATEMBEA JUU YA MAJI, NA ANATULIZA UPEPO

Uwezo wa Yesu wa kukulisha maelfu ya watu kwa njia ya muujiza umeshangaza sana watu. Wanafikia kusema kama “kwa kweli huyu ndiye Nabii mwenye alipaswa kuja katika ulimwengu,” ni kusema, Masiya, na kama anaweza kabisa kuwa mutawala muzuri. (Yohana 6:14; Kumbukumbu la Torati 18:18) Kwa hiyo, watu wanafanya mupango ili kumukamata Yesu na kumufanya mufalme.

Lakini, Yesu anatambua mupango wa watu hao. Anaacha watu waende na anaambia wanafunzi wake warudie katika mashua yao. Ili waende wapi? Wanapaswa kuenda upande wa Betsaida na kisha katika Kapernaumu. Lakini Yesu yeye, anaenda kwenye mulima usiku huo ili kusali peke yake.

Katika mwangaza wa mwezi, muda mufupi mbele ya usiku kucha, Yesu anaona mashua kwa mbali. Mawimbi ya bahari yako yanapigwa-pigwa na upepo mukali, na mitume wako ‘wanakazana sana kupiga makasia, kwa kuwa upepo ulikuwa unawatokea kwa mbele.’ (Marko 6:48) Yesu anashuka kutoka kwenye mulima na anaanza kutembea juu ya mawimbi na kuenda kule wanafunzi wake wako. Mupaka sasa, “walikuwa wamepiga makasia karibu kilometre tano (5) ao sita (6).” (Yohana 6:19) Wakati wanafunzi wanamuona Yesu anatembea juu ya bahari na kuwakaribia, wanaogopa na kusema kwa sauti kubwa: “Haya ni maono!”—Marko 6:49.

Yesu anawatuliza kwa kuwaambia hivi: “Mukuwe hodari! Ni mimi; musiogope.” Lakini Petro anamuambia: “Bwana, kama ni wewe, uniamuru nikuje kwenye uko juu ya maji.” Yesu anajibu: “Kuja!” Kwa hiyo, Petro anatoka katika mashua na kuanza kabisa kutembea juu ya maji na kuenda kwenye Yesu iko. Lakini, wakati Petro anaangalia ile zoruba yenye upepo, anaogopa na kuanza kuzama. Anasema kwa sauti kubwa: “Bwana, niokoe!” Yesu ananyoosha mukono wake, anamukamata Petro na kusema hivi: “Wewe mwenye imani kidogo, sababu gani umekuwa na mashaka?”—Matayo 14:27-31.

Petro na Yesu wanapanda katika mashua, na upepo unatulia. Wanafunzi wanashangaa, lakini wanapaswa kabisa kushangaa? Ikiwa walielewa “maana ya ile mikate,” muujiza wenye Yesu alifanya saa fulani mbele ya hapo wakati alikulisha maelfu ya watu, hawangepaswa kushangaa kuona Yesu anatembea juu ya maji na kutuliza upepo. Sasa wanamuinamia Yesu, na kusema: “Kwa kweli wewe ni Mwana wa Mungu.”—Marko 6:52; Matayo 14:33.

Muda kidogo kisha hapo wanafika Genesareti, eneo lenye kupendeza na lenye udongo wa muzuri, kusini mwa Kapernaumu. Wanatia nanga kwenye mashua na kisha wanaenda kwenye inchi kavu. Watu wanamutambua Yesu, na wote pamoja na watu wengine wa maeneo ya pembeni, wanamuletea Yesu wagonjwa. Wakati watu hao wanagusa tu sehemu ya chini ya nguo yake ya inje, wanapona kabisa.

Wakati huo, watu wenye walijionea namna Yesu alikulisha maelfu ya watu kwa njia ya muujiza wanatambua kuwa Yesu ameondoka. Kwa hiyo, wakati mashua za kidogo-kidogo zenye zinatoka Tiberia zinafika, watu hao wanapanda katika mashua hizo na kuenda Kapernaumu ili kumutafuta Yesu. Wakati wanamupata, wanamuuliza hivi: “Rabi, ulifika hapa wakati gani?” (Yohana 6:25) Kama vile tutaona, Yesu anawakemea, na iko na sababu ya muzuri ya kufanya hivyo.