Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 58

Anazidisha Mikate na Kuonya Juu ya Chachu

Anazidisha Mikate na Kuonya Juu ya Chachu

MATAYO 15:32–16:12 MARKO 8:1-21

  • YESU ANAKULISHA WANAUME 4 000

  • ANAONYA JUU YA CHACHU YA WAFARISAYO

Watu wengi sana wamemufuata Yesu katika eneo la Dekapoli, upande wa mashariki mwa Bahari ya Galilaya. Wamekuja ili kusikia mafundisho yake na kuponyeshwa, na wamekuja pia na vikapu vya chakula.

Lakini kisha wakati fulani, Yesu anaambia wanafunzi wake: “Ninasikilia hawa watu wengi huruma, kwa sababu tayari wamekaa pamoja na mimi siku tatu (3), na hawana chakula. Nikiwaacha waende nyumbani kwao wakiwa na njaa, watazimia katika barabara, na wamoja kati yao wametoka mbali.” Wanafunzi wanauliza: “Mutu anaweza kupata wapi mikate ya kutosha ili kushibisha watu hawa mahali hapa kwenye hakuna watu?”—Marko 8:2-4.

Yesu anawauliza hivi: “Muko na mikate ngapi?” Wanafunzi wanajibu: “Saba (7) na samaki wadogo wachache.” (Matayo 15:34) Kisha Yesu anaambia watu wakae chini. Anachukua mikate hiyo na samaki, anasali kwa Mungu, na anapatia wanafunzi wake ili wagawie watu. Jambo la kushangaza ni kwamba, wote wanakula na kushiba. Mikate na samaki vyenye vimebakia vinajaza vikapu saba, hata kama wanaume 4 000 hivi, na pia wanamuke na watoto, wamekula!

Kisha Yesu kuacha watu waende, yeye na wanafunzi wake wanachukua mashua na kuenda Magadani, eneo lenye kuwa pembeni ya Bahari ya Galilaya, upande wa mangaribi. Katika eneo hili, Wafarisayo wenye kusindikizwa na watu fulani wa chama cha Masadukayo wanapima kumujaribu Yesu, kwa kumuomba awaonyeshe alama fulani kutoka mbinguni.

Yesu anatambua nia yao, na anawajibu hivi: “Wakati mangaribi inafika, ninyi munasema, ‘Hali ya hewa itakuwa muzuri, kwa maana anga liko mwekundu,’ na asubui munasema: ‘Leo kutakuwa baridi kali na mvua, kwa maana anga liko mwekundu lakini liko na mawingu mazito.’ Munajua namna ya kufasiria hali ya anga, lakini hamuwezi kufasiria alama za nyakati.” (Matayo 16:2, 3) Kisha Yesu anaambia Wafarisayo na Wasadukayo kama hawatapewa alama fulani isipokuwa tu alama ya Yona.

Yesu na wanafunzi wake wanaingia katika mashua na wanaenda Betsaida pembeni ya bahari, upande wa kaskazini-mashariki. Katika safari yao, wanafunzi wanatambua kuwa walisahau kuleta mikate ya kutosha. Wako tu na mukate moja. Kwa kufikiria mazungumuzo yake ya hivi karibuni pamoja na Wafarisayo na Wasadukayo wenye kuunga Herode mukono, Yesu anatoa onyo hili: “Mufungue macho na mufanye angalisho na chachu ya Wafarisayo na chachu ya Herode.” Wanafunzi wake wanawaza kwa kukosea kama Yesu anasema hivyo kwa sababu wamesahau kuleta mikate. Yesu anatambua kuwa hawaelewe, kwa hiyo anasema hivi: “Juu ya nini munabishana kwa sababu hamuna mikate”—Marko 8:15-17.

Hivi karibuni, Yesu alitolea maelfu ya watu mikate. Kwa hiyo, wanafunzi walipaswa kujua kama Yesu hahangaikie ukosefu wa mikate. Anauliza hivi: “Je, hamukumbuke wakati nilivunja ile mikate tano (5) kwa ajili ya wale wanaume elfu tano (5 000), mulikusanya vitunga ngapi vyenye kujaa vipande?” Wanajibu: “Kumi na mbili (12).” Yesu anaongeza hivi: “Wakati nilivunja ile mikate saba (7) kwa ajili ya wale wanaume elfu ine (4 000), ni vitunga vikubwa ngapi vyenye kujaa vipande vyenye muliokota?” Wanajibu: “Saba (7).”—Marko 8:18-20.

Yesu anauliza: “Sababu gani hamuelewe kwamba sikuongea na ninyi juu ya mikate?” Anaongeza hivi: “Mufanye angalisho na chachu ya Wafarisayo na Wasadukayo.”—Matayo 16:11.

Mwishowe, wanafunzi wake wanaelewa. Chachu inatumiwa ili kuchachisha na kufanya mukate uvimbe. Yesu anatumia chachu katika maneno yake ili kufananisha uharibifu. Iko anaonya wanafunzi wake wafanye angalisho na “mafundisho ya Wafarisayo na Wasadukayo,” yenye yanaweza kuharibu.—Matayo 16:12.