Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 62

Anafundisha Somo la Maana Kuhusu Unyenyekevu

Anafundisha Somo la Maana Kuhusu Unyenyekevu

MATAYO 17:22–18:5 MARKO 9:30-37 LUKA 9:43-48

  • YESU ANATABIRI TENA KIFO CHAKE

  • ANALIPA KODI NA SARAFU YENYE ILITOKA KATIKA KINYWA CHA SAMAKI

  • NI NANI MUKUBWA ZAIDI KATIKA UFALME?

Kisha kugeuzwa sura na kuponyesha kijana mwanaume mwenye alikuwa na pepo muchafu katika eneo la Kaisaria Filipi, Yesu anaenda upande wa Kapernaumu. Anasafiri kwa siri pamoja na wanafunzi wake tu, ili watu ‘wasijue.’ (Marko 9:30) Hilo linamupatia nafasi ingine ya kutayarisha wanafunzi wake kwa ajili ya kifo chake na kwa ajili ya kazi yenye watafanya kisha. Anaeleza hivi: “Mwana wa binadamu atasalitiwa katika mikono ya watu, na watamuua, na siku ya tatu (3) atafufuliwa.”—Matayo 17:22, 23.

Hilo halipaswe kuwa jambo mupya kwa wanafunzi wake. Yesu alikuwa amekwisha kusema kama atauawa, hata kama Petro alikataa kuamini kama hilo litatokea. (Matayo 16:21, 22) Na mitume wake tatu waliona vile anageuzwa sura na walisikia mazungumuzo kuhusu “kuondoka” kwa Yesu. (Luka 9:31) Sasa wanafunzi wake ‘wanahuzunika sana’ juu ya mambo yenye iko anasema, hata kama hawayaelewe muzuri. (Matayo 17:23) Hata hivyo, wanaogopa kumuuliza juu ya jambo hilo.

Mwishowe wanafika katika Kapernaumu, mahali kwenye Yesu anafanya utumishi wake mukubwa na kwenye mitume wake wengi walikomalia. Huko, wanaume wenye wanakusanya kodi ya hekalu wanamukaribia Petro. Pengine wanajaribu kumushitaki Yesu kuwa halipe kodi, kwa kuuliza hivi: “Mwalimu wenu halipake kodi [ya hekalu] ya drakma mbili?”—Matayo 17:24.

Petro anajibu, “Analipaka.” Wakati anarudia ndani ya nyumba, Yesu anajua tayari mambo yenye yametokea. Kwa hiyo, kuliko kungojea Petro azungumuzie jambo hilo, Yesu anauliza: “Unawaza nini, Simoni? Wafalme wa dunia wanapokea ushuru ao kodi ya kichwa kutoka kwa nani? Kutoka kwa wana wao ao kutoka kwa wageni?” Petro anajibu hivi: “Kutoka kwa wageni.” Kwa hiyo, Yesu anasema: “Basi, kwa kweli, wana hawapaswe kulipa kodi.”—Matayo 17:25, 26.

Baba ya Yesu ni Mufalme wa ulimwengu wote muzima na Ule mwenye watu wanaabudu katika hekalu. Kwa hiyo, kulingana na sheria, Mwana wa Mungu hapaswe kulipa kodi ya hekalu. Yesu anasema, “Lakini ili tusiwakwaze, uende kwenye bahari, utupe ndoano, na ukamate samaki wa kwanza mwenye atatokea, na wakati utafungua kinywa chake, utapata feza moja ya kichele [stateri, ao tetradrakma]. Uikamate na uwapatie kwa ajili yangu na kwa ajili yako.”—Matayo 17:27.

Kisha muda kidogo, wanafunzi wanakutana pamoja; na wanapenda Yesu awaambie ni nani atakuwa mukubwa zaidi katika Ufalme. Hivi karibuni wanaume hao waliogopa kumuuliza Yesu juu ya kifo chake, lakini sasa hawaogope kumuuliza juu ya wakati wao wenye kuja. Yesu anajua kile wako wanawaza. Wamekuwa wanabishana juu ya jambo hilo wakati walibakia nyuma yake katika safari yao ya kurudia Kapernaumu. Kwa hiyo, anauliza: “Mulikuwa munabishana juu ya jambo gani katika barabara?” (Marko 9:33) Juu ya haya, wanafunzi wananyamaza, kwa sababu walikuwa wanabishana ili kujua ni nani kati yao ni mukubwa zaidi. Mwishowe, mitume wanamuambia Yesu jambo lenye walikuwa wanazungumuzia. Wanamuuliza hivi: “Kwa kweli, nani ndiye mukubwa zaidi katika Ufalme wa mbinguni?”—Matayo 18:1.

Wanafunzi wameangalia namna Yesu anajiendesha na wamemusikiliza kwa muda wa karibu miaka tatu; kwa hiyo, inaweza kuwa vigumu kuelewa vile wanakuwa na mabishano hayo. Hata hivyo, hawakamilike. Na walikomalia katika dini yenye watu wanakazia mamlaka na cheo. Zaidi ya hilo, hivi karibuni Petro alisikia vile Yesu anamuahidi kumupatia “funguo” fulani za Ufalme. Je, hilo linaweza kumufanya ajione kuwa mukubwa kuliko wengine? Pengine Yakobo na Yohana wanajiona pia hivyo, kwa sababu walijionea kwa macho yao wenyewe namna Yesu anageuzwa sura.

Hata kama mambo yako namna gani, Yesu anatenda ili kuwarekebisha. Anaita mutoto mudogo, anamusimamisha katikati yao, na anaambia wanafunzi hivi: “Kama hamugeuke na kuwa kama watoto wadogo, hamutaingia hata kidogo katika Ufalme wa mbinguni. Kwa hiyo, kila mutu mwenye atajinyenyekeza kama mutoto huyu mudogo ndiye mukubwa zaidi katika Ufalme wa mbinguni; na kila mutu mwenye anamupokea mutoto mudogo kama huyu kwa sababu ya jina langu ananipokea mimi pia.”—Matayo 18:3-5.

Kwa kweli, hiyo ni njia ya muzuri zaidi ya kufundisha! Yesu hakasirikie wanafunzi wake na kuwaona kuwa wenye pupa na wenye kutafuta cheo. Lakini, anatumia mutoto ili kuwafundisha somo la maana. Watoto wadogo hawatafute cheo cha juu ao kupenda kujulikana. Kwa hiyo, Yesu anaonyesha wanafunzi wake kama wanapaswa kujiona kama watoto. Kisha Yesu anamalizia somo hilo kwa kuambia wanafunzi wake hivi: “Mwenye anajiendesha kama mudogo zaidi katikati yenu ninyi wote ndiye mukubwa.”—Luka 9:48.