Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 72

Yesu Anatuma Wanafunzi 70 ili Waende Kuhubiri

Yesu Anatuma Wanafunzi 70 ili Waende Kuhubiri

LUKA 10:1-24

  • YESU ANACHAGUA WANAFUNZI 70 NA ANAWATUMA WAENDE KUHUBIRI

Sasa, tuko kwenye mwisho wa mwaka wa 32 wakati wetu; karibu miaka tatu imepita tangu Yesu abatizwe. Hivi karibuni, yeye na wanafunzi wake wamekuwa kwenye Sikukuu ya Tabenakulo katika Yerusalemu. Inawezekana hawajaenda mbali na muji huo. (Luka 10:38; Yohana 11:1) Kwa kweli, Yesu anafanya miezi sita yenye inabakia ya utumishi wake katika Yudea ao ngambo ingine ya Muto Yordani katika wilaya ya Perea. Ni lazima kazi ya kuhubiri ifanywe pia katika maeneo hayo.

Mwanzoni, kisha Pasaka ya mwaka wa 30 wakati wetu, Yesu alihubiri miezi fulani katika Yudea na kusafiri kupitia Samaria. Kisha, karibu na Pasaka ya mwaka wa 31 wakati wetu, Wayahudi walijaribu kumuua katika Yerusalemu. Kwa mwaka moja na nusu wenye ulifuata, Yesu alifundisha zaidi sana upande wa kaskazini, katika Galilaya. Wakati huo, Watu wengi wakakuwa wafuasi wake. Katika Galilaya, Yesu alizoeza mitume wake na aliwatuma na maagizo haya: “Muhubiri na kusema: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’” (Matayo 10:5-7) Sasa anapanga kampanye ya kuhubiri katika Yudea.

Ili kuanza kampanye hiyo, Yesu anachagua wanafunzi 70 na anawatuma wawili-wawili. Kwa hiyo, kuko vikundi 35 vya wahubiri wa Ufalme katika eneo kwenye “mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi wako kidogo.” (Luka 10:2) Wanapaswa kumutangulia katika maeneo kwenye pengine Yesu ataenda. Wanafunzi hao 70 wanapaswa kuponyesha wagonjwa na kueneza ujumbe uleule wenye Yesu amekuwa akihubiri.

Wanafunzi hao hawatakaza uangalifu wao juu ya kufundisha katika masinagogi. Yesu anawaambia waende kwenye nyumba za watu. Anawapatia muongozo huu: “Kila mahali munaingia katika nyumba, museme kwanza: ‘Nyumba hii ikuwe na amani.’ Na kama hapo kuko rafiki wa amani, amani yenu itakaa juu yake.” Wanapaswa kutangaza ujumbe gani? Yesu anasema hivi: “Muwaambie: ‘Ufalme wa Mungu umewakaribia ninyi.’”—Luka 10:5-9.

Maagizo yenye anapatia wanafunzi 70 ni kama yale alitoa wakati alituma mitume 12 kumepita karibu mwaka moja. Anawaonya kuwa haiko watu wote ndio watawapokea muzuri. Lakini, mambo yenye watajikaza kufanya yatatayarisha wale wenye kuwa na mioyo mizuri ili wakati Yesu atafika muda mufupi kisha hapo, wakuwe na hamu ya kumuona Bwana na kukubali mafundisho yake.

Kisha muda kidogo, wanafunzi hao 70 wenye ni wahubiri wa Ufalme wanarudia kwenye Yesu iko. Wanamuambia hivi kwa furaha: “Bwana, hata pepo wachafu wanatiishwa kwetu wakati tunatumia jina lako.” Bila shaka ripoti hiyo inamufurahisha Yesu, kwa kuwa anasema hivi: “Ninaona Shetani tayari ameanguka kama umeme wa radi kutoka mbinguni. Muangalie! Nimewapatia mamlaka ya kukanyanga nyoka na nge.”—Luka 10:17-19.

Kwa kusema hivyo, Yesu anawahakikishia kama watapata ushindi juu ya vitu vyenye kuumiza; kwa njia ya mufano, watakanyanga nyoka na nge. Zaidi ya hilo, wanaweza kuwa hakika kama wakati wenye kuja Shetani ataanguka kutoka mbinguni. Yesu anasaidia pia wanafunzi 70 kuona ni jambo gani ndilo la maana kabisa wakati wenye kuja. Anasema hivi: “Musifurahi kwa sababu roho waovu wanatiishwa kwenu, lakini mufurahi kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”—Luka 10:20.

Yesu iko na furaha kubwa, na mbele ya watu anamusifu Baba yake kwa sababu ametumia watumishi hao wanyenyekevu kwa njia hiyo ya ajabu. Yesu anageukia wanafunzi wake na kuwaambia hivi: “Yenye furaha ni macho yenye yanaona mambo yenye munaona. Kwa maana ninawaambia ninyi, manabii wengi na wafalme walitamani kuona mambo yenye munaona lakini hawakuyaona, na kusikia mambo yenye munasikia lakini hawakuyasikia.”—Luka 10:23, 24.