Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 81

Yesu na Baba Ni Kitu Kimoja, Lakini Haiko Mungu

Yesu na Baba Ni Kitu Kimoja, Lakini Haiko Mungu

YOHANA 10:22-42

  • “MIMI NA BABA NI KITU KIMOJA”

  • YESU ANAPINGA SHITAKA LA KWAMBA IKO ANAJIFANYA KUWA MUNGU

Yesu amekuja Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Kutolea Mungu Hekalu (ao, Hanuka). Sikukuu hiyo inafanywa ili kukumbuka kutolewa tena kwa hekalu kwa Yehova. Kwa zaidi ya miaka mia moja mbele ya hapo, Antioko IV Epifane, Mufalme wa Siria alijenga mazabahu juu ya mazabahu kubwa ya hekalu la Mungu. Kisha, watoto wa makuhani Wayahudi walikomboa Yerusalemu, na wakamutolea tena Yehova hekalu hilo. Tangu wakati huo, kila mwaka kunakuwa sikukuu kwenye siku ya 25 ya mwezi wa Kislevu, mwezi wenye unapatana na kipindi cha mwisho cha Mwezi wa 11 na kipindi cha mwanzo-mwanzo cha Mwezi wa 12.

Wakati huo, ni kipindi cha baridi. Yesu iko anatembea katika hekalu katika mistari ya nguzo za Sulemani. Hapo Wayahudi wanamuzunguka na kumuuliza: “Utaendelea kutuhangaisha mupaka wakati gani? Kama wewe ndiye Kristo, tuambie waziwazi.” (Yohana 10:22-24) Yesu atatenda namna gani? Anawajibu hivi: “Niliwaambia, lakini hamuamini.” Yesu hakuwaambia moja kwa moja kuwa yeye ndiye Kristo, kama vile aliambia mwanamuke Musamaria kwenye kisima. (Yohana 4:25, 26) Lakini, alionyesha kuwa yeye ni nani wakati alisema: “Mbele ya Abrahamu akuwe, mimi nilikuwa.”—Yohana 8:58.

Yesu anapenda watu wafikie kutambua wao wenyewe kuwa yeye ni Kristo kwa kulinganisha miujiza yake na mambo yenye yalitabiriwa kuwa Kristo atafanya. Ndiyo sababu nyakati zingine aliambia wanafunzi wake wasiambie mutu yeyote kuwa yeye ndiye Masiya. Lakini sasa anaambia waziwazi maadui wake Wayahudi hivi: “Kazi zenye ninafanya katika jina la Baba yangu, hizo zinatoa ushahidi juu yangu. Lakini hamuamini.”—Yohana 10:25, 26.

Sababu gani hawaamini kuwa Yesu ndiye Kristo? Anasema hivi: “Hamuamini, kwa sababu ninyi hamuko kondoo wangu. Kondoo wangu wanasikiliza sauti yangu, na ninawajua, na wananifuata. Mimi ninawapatia uzima wa milele, na hawataharibiwa hata kidogo, na hakuna mutu mwenye atawanyanganya kutoka katika mukono wangu. Kile Baba yangu amenipatia ni kikubwa zaidi kuliko vitu vingine vyote.” Kisha Yesu anawaonyesha ni kwa kiasi gani iko na urafiki wa sana pamoja na Baba yake, kwa kusema hivi: “Mimi na Baba ni kitu kimoja.” (Yohana 10:26-30) Yesu iko duniani na Baba yake iko kule mbinguni, kwa hiyo haiko anataka kusema kuwa yeye na Baba yake wako kabisa-kabisa mutu mumoja. Lakini, wako mutu mumoja katika maana ya kuwa wako wanatumika katika umoja ili kutimiza kusudi moja.

Maneno ya Yesu yanawakasirikisha Wayahudi hivi kwamba wanakamata tena majiwe ili kumuua. Hilo halimuogopeshe Yesu. Anasema hivi: “Niliwaonyesha kazi nyingi za muzuri kutoka kwa Baba. Kati ya kazi hizo, munataka kunipiga majiwe kwa sababu ya kazi gani?” Wanamujibu hivi: “Hatutake kukupiga majiwe kwa sababu umefanya kazi ya muzuri, lakini kwa sababu umekufuru; kwa maana . . . unajifanya kuwa mungu.” (Yohana 10:31-33) Yesu hajasemaka kuwa yeye ni mungu, sasa sababu gani wanaleta shitaka hilo?

Kwa kweli, Yesu iko anasema kuwa iko na nguvu zenye Wayahudi wanaamini kuwa zinatoka tu kwa Mungu. Kwa mufano, kuhusu “kondoo” alisema hivi: “Ninawapatia uzima wa milele,” jambo lenye mwanadamu hawezi kufanya. (Yohana 10:28) Wayahudi wanasahau kuwa Yesu alisema waziwazi kama alipokea mamlaka kutoka kwa Baba yake.

Ili kupinga shitaka lao la uongo, Yesu anawauliza hivi: “Je, haiandikwe katika Sheria yenu [kwenye Zaburi 82:6], ‘Mimi nilisema: “Ninyi ni miungu”’? Kama aliita ‘miungu’ wale wenye neno la Mungu lilihukumu . . . je, munaniambia mimi mwenye Baba alitakasa na kutuma katika ulimwengu, ‘Unamutukana Mungu,’ kwa sababu nilisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu’?”—Yohana 10:34-36.

Ndiyo, Maandiko yanaita “miungu” hata waamuzi wanadamu wenye wanatenda bila haki. Sasa, sababu gani Wayahudi wanaweza kusema kuwa Yesu amekosea kwa kusema “Mimi ni Mwana wa Mungu”? Anazungumuzia jambo fulani lenye linapaswa kuwasadikisha. Anasema hivi: “Kama sifanye kazi za Baba yangu, musiniamini. Lakini kama ninazifanya, hata kama hamuniamini mimi, muamini kazi hizo, ili mufikie kujua na muendelee kujua kwamba Baba iko katika umoja na mimi na mimi niko katika umoja na Baba.”—Yohana 10:37, 38.

Wakati wanasikia hivyo, wanajaribu kumukamata Yesu, lakini anawaponyoka tena. Anatoka Yerusalemu na anavuka Muto Yordani na kuenda mahali kwenye Yohana alianza kubatiza watu kumepita karibu miaka ine. Inaonekana haiko mbali na mupaka wa kusini wa Bahari ya Galilaya.

Watu wengi wanamufuata Yesu na kusema: “Yohana hakufanya alama hata moja, lakini mambo yote yenye Yohana alisema juu ya mutu huyu yalikuwa ya kweli.” (Yohana 10:41) Kwa hiyo, Wayahudi wengi wanakuwa na imani katika Yesu.