Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 85

Wanafurahi Wakati Mutenda-Zambi Anatubu

Wanafurahi Wakati Mutenda-Zambi Anatubu

LUKA 15:1-10

  • MUFANO WA KONDOO MWENYE AMEPOTEA NA WA FEZA YA KICHELE YA DRAKMA YENYE IMEPOTEA

  • MALAIKA MBINGUNI WANAFURAHI

Mara nyingi katika utumishi wake, Yesu amekazia kuwa unyenyekevu ni sifa ya maana. (Luka 14:8-11) Anapenda kabisa kupata wanaume na wanamuke wenye wako na tamaa ya kumutumikia Mungu kwa unyenyekevu. Mupaka sasa, pengine wamoja kati yao wangali wanajulikana kuwa watenda-zambi.

Wafarisayo na waandishi wanaona kuwa watu kama hao, watu wenye wanaona kuwa hawastahili, ndio wanapendezwa na Yesu na ujumbe wake. Wananungunika kwa kusema hivi: “Mutu huyu anakaribisha watenda-zambi na anakula pamoja nao.” (Luka 15:2) Wafarisayo na waandishi wanajiona kuwa watu wa hali ya juu na wanaona watu wa kawaida kama vile uchafu wenye kuwa chini ya miguu yao. Ili kuonyesha kuwa wanazarau watu hao, viongozi wanatumia neno la Kiebrania ‛am ha·’aʹrets, ni kusema, “watu wa udongo” ili kuwazungumuzia.

Lakini, Yesu yeye anatendea watu wote kwa heshima, upole, na huruma. Wengi kati ya watu wa hali ya chini, kutia ndani wamoja wenye kujulikana kuwa watenda-zambi, ndio wako na hamu ya kumusikiliza Yesu. Lakini, Yesu anajisikia namna gani wakati wanamulaumu kwa sababu ya kusaidia watu hao wa hali ya chini, na anatenda namna gani?

Jibu linakuwa wazi wakati anatoa mufano wenye kugusa moyo, kama ule wenye alitoa mbele ya hapo, wakati alikuwa katika Kapernaumu. (Matayo 18:12-14) Wakati Yesu anaeleza mambo, anafanya ionekane kama vile Wafarisayo wako wanafanya mambo yenye kuwa sawa na kama wako salama katika zizi la Mungu. Lakini, anafanya ionekane kuwa watu wa hali ya chini ni watu wenye wamepotea njia. Yesu anasema hivi:

“Ni nani kati yenu mwenye kuwa na kondoo mia moja (100), na wakati anapoteza mumoja, hataacha wale makumi kenda na kenda (99) katika jangwa na kuenda kutafuta ule mwenye alipotea mupaka amupate? Na wakati anamupata, anamubeba kwenye mabega yake na kufurahi. Na wakati anafika nyumbani, anaita marafiki wake na majirani wake pamoja, akiwaambia, ‘Mufurahi pamoja na mimi, kwa maana nimemupata kondoo wangu mwenye alikuwa amepotea.’”—Luka 15:4-6.

Yesu anafasiria mufano huo namna gani? Anaeleza hivi: “Ninawaambia ninyi kwamba kwa njia ileile, kutakuwa furaha kubwa mbinguni kwa sababu ya mutenda-zambi mumoja mwenye anatubu, kuliko kwa watu makumi kenda na kenda (99) wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa, wenye hawana lazima ya kutubu.”—Luka 15:7.

Maneno ya Yesu juu ya kutubu yanapaswa kushangaza Wafarisayo. Wanajiona kuwa watu wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa na wanafikiri kuwa hawana lazima ya kutubu. Wakati wamoja kati yao walimulaumu Yesu miaka mbili hivi mbele ya hapo kwa sababu alikuwa anakula na wakusanya-kodi na watenda-zambi, Yesu alijibu hivi: “Sikukuja kuita watu wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa, lakini nilikuja kuita watenda-zambi.” (Marko 2:15-17) Wafarisayo hao wenye kujiona kuwa watu wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa wanashindwa kuona kuwa wako na lazima ya kutubu. Kwa hiyo, hawafanye kukuwe furaha mbinguni. Ni tofauti kabisa wakati watenda-zambi wanatubu kikweli.

Ili kukazia maneno yake yenye kusema kwamba, kunakuwa furaha kubwa mbinguni wakati watenda-zambi wanatubu, Yesu anatoa mufano mwingine. Anasema hivi: “Ni mwanamuke gani mwenye kuwa na feza kumi (10) za vichele vya drakma, mwenye ikiwa anapoteza feza moja ya kichele ya drakma, hatawasha taa na kufagia nyumba yake na kuitafuta kwa uangalifu mupaka aipate? Na wakati anaipata, anaita marafiki wake na majirani wake pamoja, na kuwaambia, ‘Mufurahi pamoja na mimi, kwa maana nimepata feza yangu ya kichele ya drakma yenye nilikuwa nimepoteza.’”—Luka 15:8, 9.

Namna Yesu anafasiria mufano huu inafanana na namna alifasiria mufano wenye alitoa kuhusu kondoo mwenye amepotea. Sasa, anasema hivi: “Vilevile, ninawaambia ninyi, malaika wa Mungu wanafurahi kwa sababu ya mutenda-zambi mumoja mwenye anatubu.”—Luka 15:10.

Waza, malaika wa Mungu wanapendezwa sana wakati watenda-zambi wanatubu! Hilo ni jambo la pekee kwa sababu watenda-zambi wenye wanatubu na kupata fasi katika Ufalme wa Mungu watakuwa na cheo cha juu zaidi kuliko malaika wenyewe! (1 Wakorintho 6:2, 3) Hata hivyo, malaika hawasikie wivu. Sasa, tunapaswa kujisikia namna gani wakati mutenda-zambi anatubu kabisa na kumurudilia Mungu?