Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 90

“Ufufuo na Uzima”

“Ufufuo na Uzima”

YOHANA 11:17-37

  • YESU ANAFIKA KISHA LAZARO KUFA

  • “UFUFUO NA UZIMA”

Kisha kutoka Perea, Yesu anafika karibu na Betania, kijiji chenye kuwa kwenye kilometre 3 mashariki mwa Yerusalemu. Maria na Marta, dada za Lazaro, wanamulia Lazaro. Watu wengi wamekuja ili kuwafariji.

Kisha, mutu fulani anamuambia Marta kwamba Yesu anafika, na Marta anakimbia ili kuenda kukutana naye. Marta anamuambia Yesu mambo yenye pengine yeye na dada yake wamekuwa wakifikiria kwa siku ine: “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.” Lakini, haimaanishe kama hana tumaini. Marta anasema: “Ninajua kwamba kila kitu chenye unamuomba Mungu, Mungu atakupatia.” (Yohana 11:21, 22) Anaona kuwa Yesu angali anaweza kusaidia ndugu yake.

Yesu anajibu: “Ndugu yako atafufuka.” Marta anawaza kama Yesu iko anazungumuzia ufufuo wa wakati wenye kuja hapa duniani, tumaini lenye Abrahamu na wengine walikuwa nalo. Na anaonyesha kwamba anaamini kuwa jambo hilo litatendeka kabisa. Anasema: “Ninajua atafufuka katika ufufuo katika siku ya mwisho.”—Yohana 11:23, 24.

Lakini, itawezekana Yesu amalize huzuni yao palepale? Anamukumbusha Marta kwamba Mungu amemupatia nguvu ya kushinda kifo, anasema: “Ule mwenye ananiamini, hata akikufa, ataishi tena; na kila mutu mwenye anaishi na ananiamini hatakufa hata kidogo.”—Yohana 11:25, 26.

Yesu hapendi kusema kama wanafunzi wake wenye kuwa wazima wakati huo hawatakufa hata kidogo. Hata yeye anapaswa kufa, kama vile aliambia mitume wake. (Matayo 16:21; 17:22, 23) Yesu anakazia kwamba kumuamini kunaweza kuongoza kwenye uzima wa milele. Kwa watu wengi uzima huo utawezekana kupitia ufufuo. Hata hivyo, wakati mupangilio huu wa mambo utafikia mwisho wake, inawezekana kwamba watu waaminifu wenye kuwa wazima hawatakufa hata kidogo. Katika hali hizo mbili, kila mutu mwenye anamuamini Yesu anaweza kuwa hakika kwamba hatakufa milele.

Lakini je, Yesu mwenye ametoka kusema, “mimi ndiye ufufuo na uzima,” anaweza kumusaidia Lazaro, mwenye sasa amekufa kumepita siku ine? Yesu anamuuliza Marta: “Unaamini jambo hilo?” Anajibu: “Ndiyo, Bwana, ninaamini kwamba wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, ule mwenye anakuja katika ulimwengu.” Akiwa na imani kwamba Yesu anaweza kufanya jambo fulani siku hiyo, Marta anaenda mbio mu nyumba na kumuambia dada yake hivi kwa siri: “Mwalimu iko hapa na anakuita.” (Yohana 11:25-28) Kisha kusikia hivyo, Maria anatoka mu nyumba, mara moja watu wanamufuata wakiwaza kwamba anaenda ku kaburi la Lazaro.

Lakini, Maria anaenda kwa Yesu, anaanguka kwenye miguu yake akilia, kisha anarudilia maneno yenye dada yake alisema: “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.” Wakati anaona Maria na watu wengi wako wanalia, Yesu anaumia katika moyo, anavurugika na anatoa hata machozi. Hilo linagusa watazamaji. Lakini wengine wanauliza: ‘Je, Yesu mwenye alifungua macho ya kipofu, hangezuia mutu huyu asikufe?’—Yohana 11:32, 37.