Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 99

Yesu Anaponyesha Vipofu Wanaume na Anasaidia Zakayo

Yesu Anaponyesha Vipofu Wanaume na Anasaidia Zakayo

MATAYO 20:29-34 MARKO 10:46-52 LUKA 18:35–19:10

  • YESU ANAPONYESHA VIPOFU WANAUME KATIKA YERIKO

  • ZAKAYO MUKUSANYA-KODI ANATUBU

Yesu na watu wenye kusafiri pamoja naye wanafika Yeriko. Kutoka Yeriko mupaka Yerusalemu, ni safari ya siku moja. Yeriko inafanyizwa na miji mbili, muji wa zamani uko kwenye kilometre 1 na metre 600 hivi kutoka muji wa sasa wenye ulijengwa wakati wa Utawala wa Roma. Wakati Yesu na watu wengi sana wanaacha muji moja na kukaribia muji mwingine kati ya miji hiyo, vipofu wawili wenye kuombaomba wanasikia makelele ya watu. Mumoja wa vipofu hao anaitwa Bartimayo.

Wakati Bartimayo na kipofu mwenzake wanasikia kwamba Yesu iko anapita karibu yao, wanaanza kusema hivi kwa sauti kubwa: “Bwana, utusikilie huruma, Mwana wa Daudi!” (Matayo 20:30) Watu fulani, wanawaambia kwa ukali wanyamaze, lakini wao, wanaongeza kusema kwa sauti kubwa zaidi. Wakati Yesu anasikia fujo hiyo, anasimama. Anaomba watu wenye wako pamoja naye waite ule mwenye kusema kwa sauti kubwa. Watu hao wanaenda kwa watu hao wenye kuombaomba na wanamwambia mumoja kati yao hivi: “Usiogope! Simama; anakuita.” (Marko 10:49) Akiwa na furaha, kipofu huyo anatupa nguo yake ya inje, anasimama mara moja, na anaenda kwenye Yesu iko.

Yesu anauliza hivi: “Munataka niwafanyie nini?” Vipofu wote wawili wanamuomba: “Bwana, tunataka macho yetu yafunguliwe.” (Matayo 20:32, 33) Yesu anawasikilia huruma, kwa hiyo anagusa macho yao na anamuambia mumoja wao hivi: “Uende. Imani yako imekuponyesha.” (Marko 10:52) Vipofu hao wawili wanaona, na bila shaka wote wawili wanaanza kumutukuza Mungu. Kisha kuona jambo lenye linafanyika, watu wengine pia wanamusifu Mungu. Watu hao wenye, zamani walikuwa vipofu, wanaanza kumufuata Yesu.

Wakati Yesu anapita katikati ya Yeriko, watu wengi sana wanamuzunguka. Kila mutu anapenda kuona mwenye aliponyesha vipofu hao wawili. Watu wanamuzunguka Yesu kila upande, kwa hiyo, watu fulani wanashindwa hata kumuona. Zakayo pia anashindwa kumuona. Zakayo ni mukubwa wa wakusanya-kodi katika Yeriko na miji ya pembeni-pembeni. Hawezi kuona mambo yenye kufanyika, kwa sababu ni mufupi. Kwa hiyo, anakimbia mbele na kupanda kwenye Mufosardi-tini, muti wenye kuwa pembeni ya njia kwenye Yesu anapita. Kwenye muti, Zakayo anaona muzuri kila kitu. Wakati Yesu anakaribia na kuona Zakayo kwenye muti, anamuambia: “Zakayo, shuka haraka, kwa maana leo lazima nikae katika nyumba yako.” (Luka 19:5) Zakayo anashuka, na anaenda haraka ku nyumba ili kupokea mugeni wake wa pekee.

Wakati watu wanaona jambo lenye linatokea, wanaanza kulaumu. Wanaona kwamba haiko muzuri Yesu akaribishwe na mutu mwenye wanaona kuwa mutenda-zambi. Zakayo amekuwa tajiri kwa sababu ya kunyanganya feza za watu wakati anakusanya kodi.

Wakati Yesu anaingia ndani ya nyumba ya Zakayo, watu wanalalamika hivi: “Ameenda kutembelea mutenda-zambi katika nyumba yake.” Lakini, Yesu anaona ndani ya Zakayo nia ya kutubu, na havunjike moyo. Zakayo anasimama na anamuambia Yesu hivi: “Angalia! Bwana, nitapatia maskini nusu ya vitu vyangu, na kila kitu chenye nilinyanganya mutu yeyote, nitamurudishia mara ine.”—Luka 19:7, 8.

Ile ni njia ya muzuri yenye Zakayo anatumia ili kuonyesha kwamba anatubu kikweli! Pengine anaweza kufanya hesabu kupitia karatasi zake za mambo ya kodi na kuona ni feza ngapi alipokea kutoka kwa Wayahudi mbalimbali, na anaapa kuwarudishia feza hiyo mara ine. Anafanya hata zaidi ya mambo yenye kuombwa na sheria ya Mungu. (Kutoka 22:1; Mambo ya Walawi 6:2-5) Tena, Zakayo anaahidi kukamata nusu ya mali zake na kupatia maskini.

Yesu anafurahia sana ushuhuda huu wenye kuonyesha kwamba Zakayo ametubu na anamuambia hivi: “Leo wokovu umekuja katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Abrahamu. Kwa maana Mwana wa binadamu alikuja kutafuta na kuokoa wale wenye walipotea.”—Luka 19:9, 10.

Hivi karibuni, Yesu amekuwa akikazia uangalifu hali ya ‘wenye kupotea’ kupitia mufano wake wenye kuhusu mwana mupotevu. (Luka 15:11-24) Sasa anatoa mufano wa kweli wa mutu mwenye alipotea, na kisha akapatikana. Viongozi wa dini na wafuasi wao wanamulaumu Yesu na kumuchambua kwa sababu anahangaikia watu wenye kuwa kama Zakayo. Lakini, Yesu anaendelea kutafuta na kurudisha watoto hawa wa Abrahamu wenye walipotea.