Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 114

Mufalme Yesu Kristo Anahukumu Kondoo na Mbuzi

Mufalme Yesu Kristo Anahukumu Kondoo na Mbuzi

MATAYO 25:31-46

  • YESU ANATOA MUFANO WA KONDOO NA MBUZI

Kwenye Mulima wa Mizeituni, Yesu anatoka tu kuzungumuzia mifano ya talanta na ya mabikira kumi. Namna gani anamalizia jibu lake kwa ulizo la mitume lenye kuhusu alama ya kuwapo kwake na ya umalizio wa mupangilio wa mambo? Anafanya hivyo kwa kutoa mufano wake wa mwisho, ule wa kondoo na mbuzi.

Anaanza kwa kufasiria maneno yenye kupatana na mufano wake. Anawaambia hivi: “Wakati Mwana wa binadamu atakuja katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, basi atakaa kwenye kiti chake cha ufalme chenye utukufu.” (Matayo 25:31) Bila shaka, mutu wa maana katika mufano huu haiko mwengine, ni Yesu. Mara nyingi alijiita mwenyewe “Mwana wa binadamu.”—Matayo 8:20; 9:6; 20:18, 28.

Mufano huu utatimia wakati gani? Ni wakati Yesu “atakuja katika utukufu wake” pamoja na malaika zake na kukaa kwenye “kiti chake chenye utukufu.” Amekwisha kuzungumuzia kuhusu “Mwana wa binadamu akikuja juu ya mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mwingi” pamoja na malaika zake. Hilo litatokea wakati gani? “Kisha tu taabu ya siku hizo.” (Matayo 24:29-31; Marko 13:26, 27; Luka 21:27) Kwa hiyo, mufano huu unapaswa kutimia wakati Yesu atakuja katika utukufu wake. Kisha, atafanya nini?

Yesu anaeleza hivi: “Wakati Mwana wa binadamu atakuja . . . , mataifa yote yatakusanywa mbele yake, na atatenganisha watu mumoja na mwingine, kama vile muchungaji anatenganisha kondoo na mbuzi. Na ataweka kondoo kwenye mukono wake wa kuume, lakini mbuzi kwenye mukono wake wa kushoto.”—Matayo 25:31-33.

Kuhusu kondoo, Yesu anasema: “Kisha Mufalme ataambia wale wenye kuwa kwenye mukono wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi wenye mumebarikiwa na Baba yangu, muriti Ufalme wenye ulitayarishwa kwa ajili yenu tangu kuwekwa musingi wa ulimwengu.’” (Matayo 25:34) Sababu gani kondoo wanakubaliwa na Mufalme?

Mufalme anaeleza hivi: “Kwa maana nilikuwa na njaa, mukanipatia chakula; nilikuwa na kiu, mukanipatia kitu cha kunywa. Nilikuwa mugeni, mukanikaribisha muzuri; nilikuwa uchi, mukanivalisha. Nilikuwa mugonjwa mukanihangaikia. Nilikuwa katika gereza mukanitembelea.” Wakati kondoo hao, ni kusema, “wale wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa,” wanauliza, namna gani walitenda mambo mazuri, Yesu anawajibu hivi: “Kwa kadiri mulitendea vile mumoja wa wadogo zaidi kati ya hawa ndugu zangu, mulinitendea mimi.” (Matayo 25:35, 36, 40, 46) Hawafanye mambo haya ya muzuri mbinguni, kwa sababu huko hakuna wagonjwa na wenye njaa. Mambo hayo ya muzuri yanapaswa kuwa matendo yenye walifanyia ndugu za Kristo hapa duniani.

Mambo yako namna gani kuhusu mbuzi wenye kuwa kwenye mukono wa kushoto? Yesu anasema: “Kisha [Mufalme] ataambia wale wenye kuwa kwenye mukono wake wa kushoto: ‘Mutoke muende mbali na mimi, ninyi wenye mumelaaniwa, muende katika moto wa milele wenye ulitayarishwa kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake. Kwa maana nilikuwa na njaa, lakini hamukunipatia chakula; nilikuwa na kiu, lakini hamukunipatia kitu cha kunywa. Nilikuwa mugeni, lakini hamukunikaribisha; nilikuwa uchi, lakini hamukunivalisha; nilikuwa mugonjwa na nilikuwa katika gereza, lakini hamukunihangaikia.’” (Matayo 25:41-43) Mbuzi wanastahili kabisa hukumu hiyo kwa sababu walishindwa kutendea muzuri ndugu za Kristo wenye kuwa duniani namna inapaswa.

Mitume wanajifunza kwamba maamuzi yenye yatafanywa wakati huo wa hukumu yatakuwa na matokeo ya milele. Yesu anawaambia hivi: “Halafu [Mufalme] atawajibu na kusema: ‘Kwa kweli ninawaambia ninyi, kwa kadiri hamukutendea vile mumoja wa hawa wadogo zaidi, hamukunitendea mimi.’ Hawa wataangamizwa milele, lakini wale wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa wataingia katika uzima wa milele.”—Matayo 25:45, 46.

Jibu la Yesu kwa ulizo la mitume linatolea wafuasi wake mambo mengi ya kufikiria, linawasaidia kuchunguza matendo na mambo yenye kuwa katika mioyo yao.