Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 128

Pilato na Herode Wanaona Kuwa Yesu Hana Kosa

Pilato na Herode Wanaona Kuwa Yesu Hana Kosa

MATAYO 27:12-14, 18, 19 MARKO 15:2-5 LUKA 23:4-16 YOHANA 18:36-38

  • PILATO NA HERODE WANAULIZA YESU MAULIZO

Yesu hajaribu kumuficha Pilato kuwa yeye ni mufalme kabisa. Lakini, Ufalme wake haulete hatari kwa Utawala wa Roma. Yesu anasema hivi: “Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu. Kama Ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangepigana ili nisitiwe katika mikono ya Wayahudi. Lakini, kwa kweli, Ufalme wangu hautoke katika chanzo hiki.” (Yohana 18:36) Ndiyo, Yesu iko na Ufalme, lakini hauko wa ulimwengu huu.

Pilato haachie pale. Anauliza hivi: “Kwa hiyo, basi, wewe ni mufalme?” Yesu anapenda Pilato ajue kama amesema kweli wakati anajibu hivi: “Wewe mwenyewe unasema kwamba mimi ni mufalme. Nimezaliwa kwa ajili ya hili, na kwa ajili ya hili nimekuja katika ulimwengu, ili nitoe ushahidi juu ya ile kweli. Kila mutu mwenye kuwa upande wa ile kweli anasikiliza sauti yangu.”—Yohana 18:37.

Mbele ya hapo Yesu alikuwa amemuambia Tomasi hivi: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima.” Sasa Pilato anasikia kuwa jambo lenye lilifanya Yesu akuje duniani ni kutoa ushahidi juu ya “ile kweli,” zaidi sana kweli juu ya Ufalme wake. Yesu anaazimia kuwa muaminifu kwa ajili ya kweli hiyo hata kama hilo linamuomba kutoa uzima wake. Pilato anauliza hivi: “Kweli ni nini?” Lakini hangojee kupata maelezo zaidi. Anaona kuwa amesikia mambo ya kutosha ili kumuhukumu mutu huyo.—Yohana 14:6; 18:38.

Pilato anarudia ili kuongea na kikundi cha watu wenye wanangojea inje ya nyumba yake. Pengine Yesu iko pembeni yake wakati anaambia hivi wakubwa wa makuhani na wengine wenye kuwa pamoja nao: “Sipate kosa lolote kwa mutu huyu.” Watu hao wanakasirika kwa sababu ya uamuzi huo, kwa hiyo, wanakazia hivi: “Anachochea watu kwa kufundisha katika Yudea yote, kuanzia Galilaya na hata mupaka hapa.”—Luka 23:4, 5.

Pilato anapaswa kushangazwa na Wayahudi hao wenye kushikilia mawazo yenye hayana musingi. Wakati wakubwa wa makuhani na wazee wanaendelea kulalamika, Pilato anauliza Yesu hivi: “Hausikie mambo yote yenye wanashuhudia juu yako?” (Matayo 27:13) Yesu hajibie jambo lolote. Pilato anashangaa kwa sababu Yesu anabakia kimya wakati anashitakiwa mambo ya uongo.

Wayahudi wanasema kuwa Yesu ‘alianzia Galilaya.’ Wakati Pilato anafuatilia jambo hilo, anavumbua kuwa kwa kweli, Yesu ni mutu wa Galilaya. Hilo linamupatia Pilato wazo juu ya namna anaweza kuepuka daraka la kumuhukumu Yesu. Herode Antipa (mwana wa Herode Mukubwa) anatawala Galilaya, na iko katika Yerusalemu katika kipindi hiki cha Pasaka. Kwa hiyo, Pilato anamutuma Yesu kwa Herode. Ni Herode Antipa ndiye alitoa amri ili Yohana Mubatizaji akatwe kichwa. Kisha, wakati alisikia kuwa Yesu iko anafanya miujiza, Herode alikuwa na wasiwasi kuwa pengine Yesu ni Yohana mwenye amefufuka.—Luka 9:7-9.

Sasa Herode anafurahi kwa sababu anatumainia kumuona Yesu. Haiko kwa sababu anapenda kumusaidia Yesu ao anapenda kujua kabisa ikiwa mambo yenye wanamushitakia ni ya kweli. Herode anapenda tu kumuona, na ‘anatamani kumuona anafanya alama fulani.’ (Luka 23:8) Hata hivyo, Yesu hafanye mambo yenye Herode alipenda afanye. Kwa kweli, wakati Herode anamuuliza maulizo, Yesu hajibie jambo lolote. Kwa sababu ya kasirani, Herode na maaskari wake wanamutendea Yesu “kwa zarau.” (Luka 23:11) Wanamuvalisha nguo ya heshima na wanamuchekelea. Kisha Herode anamurudisha Yesu kwa Pilato. Herode na Pilato walikuwa maadui zamani, lakini sasa wanakuwa marafiki.

Wakati Yesu anarudishwa, Pilato anaita wakubwa wa makuhani, viongozi Wayahudi na watu na kusema hivi: “Nilimuuliza mbele yenu lakini sikupata jambo lolote lenye kuhakikisha mashitaka yenye munaleta juu yake. Kwa kweli, hata Herode hakupata jambo lolote, kwa maana alimurudisha kwetu, na muangalie! Mutu huyu hakufanya jambo lolote lenye kustahili kifo. Kwa hiyo nitamupatia azabu na kumufungua.”—Luka 23:14-16.

Pilato anapenda kumuachilia Yesu, kwa sababu anaelewa kuwa ni wivu ndio unachochea makuhani wamulete kwake. Wakati Pilato anajaribu kumuachilia Yesu, anapata jambo lingine ya kumuchochea kufanya hivyo. Wakati anakaa kwenye kiti cha hukumu, bibi yake anamutumia ujumbe huu: “Usiingie katika mambo ya mutu huyo mwenye hana kosa, kwa maana niliteseka sana leo katika ndoto [inawezekana ndoto yenye kutoka kwa Mungu] kwa sababu yake.”—Matayo 27:19.

Pilato anajua kama anapaswa kumuachilia mutu huyo mwenye hana kosa; lakini atafanya hivyo namna gani?