Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 135

Yesu Mwenye Amefufuliwa Anatokea Wengi

Yesu Mwenye Amefufuliwa Anatokea Wengi

LUKA 24:13-49 YOHANA 20:19-29

  • YESU ANATOKEA KATIKA BARABARA YA KUENDA EMAU

  • ANAFUNGULIA WANAFUNZI WAKE MAANDIKO TENA NA TENA

  • TOMASI ANAACHA KUWA NA MASHAKA

Ni Siku ya Yenga tarehe 16 mwezi wa Nisani, wanafunzi wamevunjika moyo. Hawaelewe sababu gani kaburi liko wazi. (Matayo 28:9, 10; Luka 24:11) Wakati fulani siku hiyo, Kleopa na mwanafunzi mwingine wanatoka Yerusalemu ili kuenda Emau yenye kuwa kwenye umbali wa kilometre 11 kutoka Yerusalemu.

Wakati wako wanatembea, wanazungumuzia mambo yenye yametokea. Kisha mutu fulani anajiunga nao. Anawauliza hivi: “Ni mambo gani haya yenye munazungumuzia kati yenu wakati muko munatembea?” Kleopa anajibu hivi: “Je, wewe ni mugeni na unakaa peke yako Yerusalemu na kwa hiyo haujue mambo yenye yalifanyika mule siku hizi?” Mutu huyo anauliza hivi: “Mambo gani?”—Luka 24:17-19.

Wanasema hivi: “Mambo yenye kuhusu Yesu Munazareti. . . . Sisi tulitumaini kama mutu huyo ndiye angekomboa Israeli.”—Luka 24:19-21.

Kleopa na mwenzake wanaanza kumuelezea mambo yenye yalitokea siku hiyo. Wanasema kuwa wanamuke fulani walienda kwenye kaburi kwenye Yesu alizikwa na wakakuta kaburi liko wazi na kuwa wanamuke hao walijionea tukio la ajabu, ni kusema, malaika wenye walitokea na kusema kuwa Yesu ni mwenye kuishi. Wanasema kuwa wengine walienda pia kwenye kaburi na “wakalikuta kama vile wale wanamuke walikuwa wamesema.”—Luka 24:24.

Kwa kweli, wanafunzi hao wawili wanachanganyikiwa kabisa na mambo yenye yalikuwa yametokea. Mutu huyo anajibu kwa mamlaka ili kuwasaidia wabadilishe mawazo yao ya mubaya, anasema hivi: “Ninyi wenye kukosa akili na wenye mioyo mizito kuamini mambo yote yenye manabii walisema! Je, haikukuwa lazima Kristo apatwe na mambo haya na aingie katika utukufu wake?” (Luka 24:25, 26) Anaanza kuwafasiria Maandiko mengi yenye kuhusu Kristo.

Mwishowe wote watatu wanafika karibu na Emau. Wanafunzi hao wawili wanapenda kusikia mambo mengi zaidi, kwa hiyo wanaambia mutu huyo hivi: “Kaa pamoja na sisi, kwa sababu mangaribi imekaribia na karibuni muchana utaisha.” Anakubali kubakia pamoja nao, na wanakula chakula. Wakati mutu huyo anasali, na kuvunja mukate, na kuwapatia, wanatambua kuwa ni Yesu, lakini anapotea. (Luka 24:29-31) Sasa wanajua kabisa kuwa Yesu ni mwenye kuishi!

Wanafunzi hao wawili wanazungumuzia kwa furaha sana mambo yenye wamejionea. Wanasema hivi: “Je, mioyo yetu haikukuwa inawaka wakati alikuwa anazungumuza na sisi katika barabara, na wakati alikuwa anatufasiria Maandiko waziwazi?” (Luka 24:32) Wanarudia haraka Yerusalemu, huko wanakutana na mitume na watu wengine wenye kuwa pamoja nao. Mbele Kleopa na mwenzake waseme mambo yenye waliona, wanasikia wengine wanasema hivi: “Kwa kweli Bwana alifufuliwa, na alimutokea Simoni!” (Luka 24:34) Kisha wao wawili wanaeleza namna Yesu aliwatokea. Ndiyo, wao pia walimuona kwa macho yao.

Sasa Yesu anawatokea katika chumba, wote wanashituka! Hilo linaonekana kuwa jambo lenye kushangaza kwa sababu walifunga mulango juu ya kuogopa Wayahudi. Lakini, Yesu anasimama katikati yao. Anasema hivi kwa utulivu: “Mukuwe na amani.” Lakini wanaogopa. Kama vile walifanya mwanzoni ‘wanawazia kwamba wanaona roho.’—Luka 24:36, 37; Matayo 14:25-27.

Ili kuwahakikishia kuwa haiko maono ao jambo fulani lenye wanawazia tu, lakini iko na mwili wa mwanadamu, Yesu anawaonyesha mikono na miguu yake na anasema hivi: “Sababu gani munaogopa, na sababu gani mashaka yametokea katika mioyo yenu? Muangalie mikono na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe; muniguse na muone, kwa maana roho haina nyama na mifupa kama vile munaona mimi niko navyo.” (Luka 24:36-39) Wanafurahi sana na wanashangaa lakini wangali na mashaka kwa kiasi fulani.

Ili kuwasaidia zaidi waone kuwa ni yeye kabisa, anawauliza hivi: “Muko na chakula hapa?” Anakubali kipande cha samaki yenye kuchomwa na anakula. Kisha anasema hivi: “Haya ndiyo maneno yangu yenye niliwaambia wakati nilikuwa ningali pamoja na ninyi [mbele ya kifo changu], kwamba mambo yote yenye yaliandikwa juu yangu katika Sheria ya Musa na katika Manabii, na Zaburi yanapaswa kutimizwa.”—Luka 24:41-44.

Yesu alikuwa amesaidia Kleopa na mwenzake kuelewa Maandiko, na anafanya hivyo pia kwa wale wenye kukusanyika hapo. Anasema hivi: “Haya ndiyo yameandikwa: kwamba Kristo atateseka na atafufuliwa kutoka kwa wafu siku ya tatu (3), na kwa musingi wa jina lake kutubu kwenye kuongoza kwenye musamaha wa zambi kungehubiriwa katika mataifa yote—kuanzia Yerusalemu. Ninyi munapaswa kuwa mashahidi wa mambo haya.”—Luka 24:46-48.

Kwa sababu fulani, mutume Tomasi haiko pamoja nao. Siku zenye kufuata, wengine wanamuambia hivi kwa furaha: “Tumeona Bwana!” Tomasi anajibu: “Kama sione katika mikono yake alama za misumari na kama sitie kidole changu katika alama hizo za misumari na kutia mukono wangu katika ubavu wake, sitaamini hata kidogo.”—Yohana 20:25.

Kisha siku munane, wanafunzi wanakusanyika tena katika nyumba na wanafunga mulango, lakini wakati huu Tomasi iko pamoja nao. Yesu anatokea katikati yao katika mwili wa nyama na anawasalimia hivi: “Mukuwe na amani.” Yesu anamugeukia Tomasi na kusema hivi: “Tia kidole chako hapa, uone mikono yangu, na ulete mukono wako uguse ubavu wangu, na uache kuwa na mashaka lakini uamini.” Tomasi anasema hivi: “Bwana wangu na Mungu wangu!” (Yohana 20:26-28) Ndiyo, sasa hana tena mashaka kuwa Yesu ni mwenye kuishi, na ni kiumbe wa roho mwenye kumuwakilisha Mungu.

Yesu anasema hivi: “Kwa sababu umeniona, je, umeamini? Wenye furaha ni wale wenye hawajaona lakini wanaamini.”—Yohana 20:29.