Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 1

Matukio Yanayoongoza Kwenye Huduma ya Yesu

“Huyo atakuwa mkuu.” —Luka 1:32

Matukio Yanayoongoza Kwenye Huduma ya Yesu

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 1

Wapokea Ujumbe Kutoka kwa Mungu

Malaika Gabrieli alileta ujumbe ambao ilikuwa vigumu kuuamini.

SURA YA 2

Yesu Aheshimiwa Kabla Hajazaliwa

Elisabeti na mtoto wake ambaye hakuwa amezaliwa walimheshimu Yesu jinsi gani?

SURA YA 3

Yule Atakayetayarisha Njia Azaliwa

Mara tu baada ya Zekaria kupata tena kimuujiza uwezo wake wa kuongea, alitoa unabii muhimu.

SURA YA 4

Maria​—Ana Mimba Lakini Hajaolewa

Je, Yosefu anamwamini Maria anaposema kwamba ana mimba, si kutokana na mwanamume, bali kupitia roho takatifu?

SURA YA 5

Yesu Alizaliwa Wapi na Wakati Gani?

Tunajuaje kwamba Yesu hakuzaliwa Desemba 25?

SURA YA 6

Mtoto Aliyeahidiwa

Yosefu na Maria wanapomleta Yesu hekaluni akiwa mchanga, Waisraeli wawili wenye umri mkubwa wanatabiri kuhusu maisha ya Yesu ya baadaye.

SURA YA 7

Wanajimu Wamtembelea Yesu

Kwa nini mwanzoni nyota ambayo waliona Mashariki haikuwaongoza kwa Yesu bali kwa Mfalme muuaji Herode?

SURA YA 8

Wanaokoka Kutoka kwa Mtawala Mwovu

Mambo matatu yaliyotabiriwa katika Biblia kumhusu Masihi yanatimizwa mwanzoni mwa maisha ya Yesu.

SURA YA 9

Maisha ya Utotoni Huko Nazareti

Yesu alikuwa na ndugu na dada wangapi?

SURA YA 10

Familia ya Yesu Yasafiri Kwenda Yerusalemu

Yosefu na Maria wanachanganyikiwa wanapokosa kumpata Yesu, naye anashangaa kwamba hawakutambua mara moja mahali ambapo wangempata

SURA YA 11

Yohana Mbatizaji Atayarisha Njia

Baadhi ya Mafarisayo na Masadukayo wanapomjia Yohana, anawashutumu. Kwa nini?