SEHEMU YA 4
Huduma ya Yesu ya Baadaye Huko Yudea
“Mwombeni Bwana wa mavuno awatume wafanyakazi.”—Luka 10:2
KATIKA SEHEMU HII
SURA YA 66
Akiwa Yerusalemu kwa Ajili ya Sherehe ya Vibanda
Ni nini kilichofanya wale waliomsikiliza Yesu waamini kwamba ana roho mwovu?
SURA YA 67
‘Hakuna Mtu Mwingine Ambaye Amewahi Kuzungumza Hivyo’
Kwa ujumla mahakama kuu ya Wayahudi inampinga Yesu, lakini mshiriki mmoja anajitahidi kumtetea.
SURA YA 68
Mwana wa Mungu—“Nuru ya Ulimwengu”
Yesu alisema “kweli itawaweka nyinyi huru.” Huru kutokana na nini?
SURA YA 69
Je, Baba Yao Ni Abrahamu au Ni Ibilisi?
Yesu anazungumzia jinsi ya kuwatambua watoto wa Abrahamu, pia anamtambulisha Baba yake.
SURA YA 70
Yesu Amponya Mtu Aliyezaliwa Kipofu
Wanafunzi wanauliza kwa nini mtu huyo alizaliwa kipofu. Je, alifanya dhambi? Je, wazazi wake walifanya dhambi? Watu wana maoni yanayotofautiana baada ya Yesu kumponya mtu huyo.
SURA YA 71
Mafarisayo Wamhoji Mtu Aliyekuwa Kipofu
Sababu anazotoa mtu aliyekuwa kipofu zinawakasirisha Mafarisayo. Mafarisayo wanamfukuza kwenye sinagogi, kama wazazi wake walivyohofia.
SURA YA 72
Yesu Awatuma Wanafunzi 70 Wakahubiri
Huko Yudea, Yesu anawatuma wahubiri 70 wa Ufalme wakiwa wawili wawili. Wanafunzi watawapata wapi watu ili wawahubirie—ni katika masinagogi au katika nyumba zao?
SURA YA 73
Msamaria Athibitika Kuwa Jirani wa Kweli
Yesu anatumiaje hadithi ya Msamaria mwenye ujirani, au “Msamaria Mwema,” kufundisha somo muhimu?
SURA YA 74
Masomo Kuhusu Ukarimu na Sala
Yesu anawatembelea Maria na Martha nyumbani kwao. Anawafundisha nini kuhusu ukarimu? Na baadaye anawafundisha wanafunzi wake wasali kuhusu nini?
SURA YA 75
Yesu Afunua Chanzo cha Furaha
Yesu anawajibu adui zake, kwa kuwaambia kuhusu “kidole cha Mungu” na jinsi Ufalme wa Mungu ulivyowafikia ghafla. Pia anaonyesha jinsi wanavyoweza kupata furaha ya kweli.
SURA YA 76
Kula Mlo Pamoja na Farisayo
Yesu anafunua unafiki wa kidini wa waandishi na Mafarisayo. Wanawatwika watu mizigo gani mizito?
SURA YA 77
Yesu Atoa Ushauri Kuhusu Utajiri
Yesu anatoa mfano wa tajiri ambaye alijenga maghala makubwa. Anarudia kutoa ushauri gani kuhusu hatari ya kutafuta utajiri?
SURA YA 78
Uwe Tayari, Msimamizi Mwaminifu!
Yesu aonyesha kwamba angependa wanafunzi wake walishwe vizuri kiroho. Msimamizi atatimiza jukumu gani ili walishwe vizuri kiroho? Kwa nini ushauri wa kuwa tayari ni muhimu sana?
SURA YA 79
Kwa Nini Kutakuwa na Uharibifu Wakati Ujao?
Yesu anasema kwamba wale ambao anajaribu kuwasaidia wataharibiwa ikiwa hawatubu. Je, watajifunza somo muhimu ambalo Yesu anataka kuwafundisha kuhusu uhusiano wao pamoja na Mungu?
SURA YA 80
Mchungaji Mwema na Mazizi ya Kondoo
Uhusiano wa mchungaji na kondoo wake unafafanua vizuri jinsi Yesu anavyohisi kuhusu wanafunzi wake. Je, watatambua mafundisho yake na kufuata mwongozo wake?
SURA YA 81
Yesu na Baba Ni Kitu Kimoja, Lakini Yeye Si Mungu
Baadhi ya watu wanaomkosoa Yesu, wanamshtaki kwamba anajilinganisha na Mungu. Yesu anapingaje kwa ustadi mashtaka yao ya uwongo?