Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 4

Huduma ya Yesu ya Baadaye Huko Yudea

“Mwombeni Bwana wa mavuno awatume wafanyakazi.”​—Luka 10:2

Huduma ya Yesu ya Baadaye Huko Yudea

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 66

Akiwa Yerusalemu kwa Ajili ya Sherehe ya Vibanda

Ni nini kilichofanya wale waliomsikiliza Yesu waamini kwamba ana roho mwovu?

SURA YA 67

‘Hakuna Mtu Mwingine Ambaye Amewahi Kuzungumza Hivyo’

Kwa ujumla mahakama kuu ya Wayahudi inampinga Yesu, lakini mshiriki mmoja anajitahidi kumtetea.

SURA YA 68

Mwana wa Mungu​—“Nuru ya Ulimwengu”

Yesu alisema “kweli itawaweka nyinyi huru.” Huru kutokana na nini?

SURA YA 69

Je, Baba Yao Ni Abrahamu au Ni Ibilisi?

Yesu anazungumzia jinsi ya kuwatambua watoto wa Abrahamu, pia anamtambulisha Baba yake.

SURA YA 70

Yesu Amponya Mtu Aliyezaliwa Kipofu

Wanafunzi wanauliza kwa nini mtu huyo alizaliwa kipofu. Je, alifanya dhambi? Je, wazazi wake walifanya dhambi? Watu wana maoni yanayotofautiana baada ya Yesu kumponya mtu huyo.

SURA YA 71

Mafarisayo Wamhoji Mtu Aliyekuwa Kipofu

Sababu anazotoa mtu aliyekuwa kipofu zinawakasirisha Mafarisayo. Mafarisayo wanamfukuza kwenye sinagogi, kama wazazi wake walivyohofia.

SURA YA 72

Yesu Awatuma Wanafunzi 70 Wakahubiri

Huko Yudea, Yesu anawatuma wahubiri 70 wa Ufalme wakiwa wawili wawili. Wanafunzi watawapata wapi watu ili wawahubirie​—ni katika masinagogi au katika nyumba zao?

SURA YA 73

Msamaria Athibitika Kuwa Jirani wa Kweli

Yesu anatumiaje hadithi ya Msamaria mwenye ujirani, au “Msamaria Mwema,” kufundisha somo muhimu?

SURA YA 74

Masomo Kuhusu Ukarimu na Sala

Yesu anawatembelea Maria na Martha nyumbani kwao. Anawafundisha nini kuhusu ukarimu? Na baadaye anawafundisha wanafunzi wake wasali kuhusu nini?

SURA YA 75

Yesu Afunua Chanzo cha Furaha

Yesu anawajibu adui zake, kwa kuwaambia kuhusu “kidole cha Mungu” na jinsi Ufalme wa Mungu ulivyowafikia ghafla. Pia anaonyesha jinsi wanavyoweza kupata furaha ya kweli.

SURA YA 76

Kula Mlo Pamoja na Farisayo

Yesu anafunua unafiki wa kidini wa waandishi na Mafarisayo. Wanawatwika watu mizigo gani mizito?

SURA YA 77

Yesu Atoa Ushauri Kuhusu Utajiri

Yesu anatoa mfano wa tajiri ambaye alijenga maghala makubwa. Anarudia kutoa ushauri gani kuhusu hatari ya kutafuta utajiri?

SURA YA 78

Uwe Tayari, Msimamizi Mwaminifu!

Yesu aonyesha kwamba angependa wanafunzi wake walishwe vizuri kiroho. Msimamizi atatimiza jukumu gani ili walishwe vizuri kiroho? Kwa nini ushauri wa kuwa tayari ni muhimu sana?

SURA YA 79

Kwa Nini Kutakuwa na Uharibifu Wakati Ujao?

Yesu anasema kwamba wale ambao anajaribu kuwasaidia wataharibiwa ikiwa hawatubu. Je, watajifunza somo muhimu ambalo Yesu anataka kuwafundisha kuhusu uhusiano wao pamoja na Mungu?

SURA YA 80

Mchungaji Mwema na Mazizi ya Kondoo

Uhusiano wa mchungaji na kondoo wake unafafanua vizuri jinsi Yesu anavyohisi kuhusu wanafunzi wake. Je, watatambua mafundisho yake na kufuata mwongozo wake?

SURA YA 81

Yesu na Baba Ni Kitu Kimoja, Lakini Yeye Si Mungu

Baadhi ya watu wanaomkosoa Yesu, wanamshtaki kwamba anajilinganisha na Mungu. Yesu anapingaje kwa ustadi mashtaka yao ya uwongo?