Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 4

Utumishi wa Yesu Katika Yudea

“Mumuombe Bwana wa Mavuno Atume Wafanyakazi.”​—Luka 10:2

Utumishi wa Yesu Katika Yudea

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 66

Iko Katika Yerusalemu kwa Ajili ya Sikukuu ya Tabenakulo

Ni nini yenye ilifanya wale wenye walikuwa wanamusikiliza Yesu waamini kuwa iko na pepo muchafu?

SURA YA 67

“Hakuna Mutu Mwenye Amekwisha Kusema Kama Mutu Huyu”

Tribinali yote kubwa ya Wayahudi wanamupinga Yesu, lakini mutu mumoja anapata ujasiri wa kumusemea.

SURA YA 68

Mwana wa Mungu Ni “Mwangaza wa Ulimwengu”?

Yesu alisema, “kweli itawaweka ninyi huru.” Huru kutoka nini?

SURA YA 69

Baba yao Ni Nani: Abrahamu ao Ibilisi?

Yesu anaonyesha namna ya kutambua watoto wa Abrahamu, na pia anaonyesha kuwa Baba yake ni nani kabisa.

SURA YA 70

Yesu Anaponyesha Mwanaume Mwenye Alizaliwa Kipofu

Wanafunzi wanauliza sababu gani mwanaume fulani alizaliwa kipofu. Alifanya zambi? Ni wazazi wake ndio walifanya zambi? Watu wanatenda kwa namna tofauti wakati Yesu anamuponyesha.

SURA YA 71

Wafarisayo Wanauliza Maulizo Mwanaume Mwenye Alikuwa Kipofu

Mawazo yenye kupatana na akili ya mwanaume mwenye alikuwa kipofu zamani yanakasirikisha Wafarisayo. Kama vile tu wazazi wake walikuwa wanaogopa, Wafarisayo wanamufukuza katika sinagogi.

SURA YA 72

Yesu Anatuma Wanafunzi 70 ili Waende Kuhubiri

Katika Yudea, Yesu anatuma wanafunzi 70 kama watangazaji wa Ufalme, wawili-wawili. Wanafunzi hao watapata watu wapi—katika masinagogi ao kwenye nyumba za watu?

SURA YA  73

Musamaria Anaonyesha Kuwa Yeye Ni Jirani wa Kweli

Namna gani Yesu anatumia mufano wa Musamaria mwema, ili kufundisha somo la maana sana?

SURA YA 74

Anafundisha Kuhusu Ukaribishaji-Wageni na Kuhusu Sala

Yesu anatembelea Maria na Marta kwenye nyumba yao. Anawafundisha nini kuhusu ukaribishaji-wageni? Na kisha, namna gani anafundisha wanafunzi wake kuhusu mambo yenye wanapaswa kumuomba Mungu?

SURA YA 75

Yesu Anaonyesha Siri ya Kupata Furaha

Yesu anajibia maadui wake kwa kuwaambia juu ya “kidole cha Mungu” na juu ya namna Ufalme wa Mungu umekwisha kuwafikia. Anaonyesha pia namna watu wanaweza kupata furaha ya kweli.

SURA YA 76

Anakula Pamoja na Mufarisayo

Yesu anafunua unafiki wa waandishi na Wafarisayo. Ni mizigo gani mizito wanakaza watu wabebe?

SURA YA 77

Yesu Anatoa Mashauri Kuhusu Utajiri

Yesu anatoa mufano wa mwanaume mumoja tajiri mwenye alijenga madepo makubwa zaidi. Anarudilia shauri gani kuhusu hatari za kutafuta utajiri?

SURA YA 78

Musimamizi-Nyumba Mwaminifu, Endelea Kuwa Tayari!

Yesu anaonyesha kuwa anahangaikia hali ya muzuri ya kiroho wanafunzi wake. Ili wakuwe na hali ya muzuri ya kiroho, musimamizi-nyumba huyo atakuwa na daraka gani? Sababu gani shauri la kuendelea kuwa tayari ni la maana sana?

SURA YA 79

Sababu Gani Uharibifu Uko Unakuja

Yesu anasema kuwa wale wenye iko anajikaza kusaidia wako katika hatari ya kuhabiriwa ikiwa hawatubu. Je, watajifunza somo la maana lenye Yesu anajikaza kuwafundisha kuhusu urafiki wao pamoja na Mungu?

SURA YA 80

Muchungaji Mwema na Mazizi ya Kondoo

Uhusiano kati ya muchungaji na kondoo unaonyesha muzuri namna Yesu anajisikia juu ya wanafunzi wake. Je, watatambua mafundisho yake na kufuata muongozo wake?

SEHEMU YA 81

Yesu na Baba Ni Kitu Kimoja, Lakini Haiko Mungu

Maadui fulani wa Yesu wanamushitaki kuwa iko anajifanya sawasawa na Mungu. Namna gani Yesu anapinga kwa hekima shitaka lao la uongo?